Foreign Exchange Rates

DStv Advert_090724

DStv Advert_090724

SBT Tanzania Advert_291123

Friday 17 October 2014

BAYPORT TANZANIA YAZINDUA HUDUMA MPYA YA MIKOPO YA BIDHAA

Meneja wa Masoko na mawasiliano wa taasisi ya kifedha ya Bayport Tanzania, Ngula Cheyo (wa kwanza kushoto), akiwa kwenye picha ya pamoja na Meneja masoko wa Fair Deal Auto (pvt) Limited, wasambazaji wa pikipiki aina ya Boxer na Bajaji, Saimon Paul  pamoja na  Meneja Bishara wa Bayport, Thabit Mndeme (kulia), wakati wa utambulisho wa kuzindua huduma hiyo ya Mikopo ya bidhaa.

Meneja wa Masoko na mawasiliano wa taasisi ya kifedha ya Bayport Tanzania, Ngula Cheyo (wa kwanza kushoto), akifuatiwa na Meneja masoko wa Toyo,  Drima Makachwa (katikati) pamoja na  Meneja Bishara wa Bayport, Thabit Mndeme (kulia), kwenye uzinduzi huo.

Meneja wa Masoko na mawasiliano wa taasisi ya kifedha ya Bayport Tanzania, Ngula Cheyo (katikati) akiongea na wandishi wa habari (hawapo pichani) wakati wa utambulisho wa huduma ya Mikopo ya bidhaa.

Taasisi ya kifedha ya Bayport Tanzania, tarehe Oktoba 15, 2014 imezindua huduma mpya ijulikanayo kama Mikopo ya bidhaa ikiwa na lengo la kurahisisha utendaji kazi wa watumishi wa umma na wafanyakazi wote wa kampuni zilizoidhinishwa na Bayport. Uzinduzi huo ulifanyika katika ofisi za makao makuu ya Bayport, maeneo ya Moroco jijini Dar es Salaam mbele ya wandishi wa vyombo mbalimbali vya habari umeonyesha matumaini mapya ya watanzania wanaosumbukia usafiri katika vituo vyao vya kazi, hususani maeneo ya mikoani ambako mara kadhaa kumesikika malalamiko ya maisha magumu kwa watumishi wa umma. 


Akizungumza juu ya tukio hilo, Meneja Bishara wa taasisi hiyo Thabit Mndeme alisema kwamba ni wakati wa kukuza uchumi wa nchi kuhakikisha kuwa watu wanafanya kazi kwa bidii na shauku. Alisema wapo watumishi ambao wanaishi kwa tabu kutokana na changamoto ya usafiri na mahitaji mengine ya kijamii, hivyo kutokana na huduma hiyo mpya ya kukopeshwa pikipiki, boda boda itasaidia kwa kiasi chake. Pia alisema Bayport imekaa kuangalia namna gani watanzania wataendelea kufanya kazi kwa moyo na kukuza uchumi ambao uko sambamba na kuwakopesha fedha kama wanavyofanya kwa sasa na kuamua kuwakopesha tena na bidhaa za usafiri. Naye Meneja wa Masoko na mawasiliano wa taasisi hiyo Ngula Cheyo alisema kuwa mikopo mipya kwa sasa inapatikana kwa masaa 24, huku ikipatikana pia kwa mikoa na wilaya zote kwenye ofisi za Bayport zaidi ya 80, nchini. 

Bayport ni Taasisi ya kifedha isiyo ya kibenki inayoongoza katika utowaji wa mikopo barani Africa na Amerika ya kusini. Imeanzishwa mwaka 2001, na umiliki wake ukiwa Mauritius. (Na Andrew Chale).

No comments:

Post a Comment