Foreign Exchange Rates

CRDB Bank Advert_070325

Selcom Pesa Advert_110225

Selcom Pesa Advert_110225

Standard Chartered Advert_300125

Standard Chartered Advert_300125

Monday, 19 January 2026

VODACOM YAZINDUA DUKA JIPYA DODOMA, KUBORESHA HUDUMA KWA WATEJA WA KANDA YA KATI

Afisa Mtendaji Mkuu wa Vodacom Tanzania PLC, Philip Besiimire (wa pili kushoto), akikata utepe kuashiria ufunguzi wa duka jipya kubwa la Vodacom jijini Dodoma, linalolenga kusogeza huduma karibu na wateja. Tukio hilo lilishuhudiwa na Mkuu wa Kanda ya Kati, Chiha Nchimbi (wa pili kulia), na Mdau wa Vodacom, Emmanuel Makaki (kushoto).
Mkurugenzi Mtendaji wa Vodacom Tanzania, Philip Besiimire (wa pili kushoto), akitazama bidhaa zilizopo ndani ya duka jipya kubwa la Vodacom mkoani Dodoma baada ya kulizindua. Kushoto ni Mkuu wa Vodacom Kanda ya Kati, Chiha Nchimbi.

Dodoma – Kampuni ya Vodacom Tanzania imezindua duka kubwa jipya la mfano (flagship store) jijini Dodoma, hatua inayolenga kusogeza huduma bora zaidi kwa wateja wa mkoa huo pamoja na mikoa mingine ya Kanda ya Kati.

Akizungumza wakati wa uzinduzi wa duka hilo, Mkurugenzi Mtendaji wa Vodacom Tanzania, Bw. Philip Besiimire, amesema duka hilo ni mkombozi kwa wakazi wa Dodoma na maeneo jirani kutokana na kuboreshwa kwa huduma mbalimbali, zikiwemo huduma maalumu kwa wateja wenye mahitaji maalumu. Ameeleza kuwa kwa mara ya kwanza, duka hilo limezingatia kikamilifu upatikanaji wa huduma kwa makundi mbalimbali ikiwemo viziwi, watu wenye ulemavu wa miguu, macho na wengineo, huduma ambazo hapo awali hazikuwepo kwa kiwango hicho.

Bw. Besiimire ameongeza kuwa uzinduzi wa duka hilo unaakisi dhamira ya Vodacom Tanzania ya kuendelea kuwekeza katika miundombinu na uzoefu wa wateja, sambamba na mahitaji yanayobadilika ya wateja wake, hususan katika miji inayokua kwa kasi kama Dodoma.

Kwa upande wao, wateja wa Vodacom wameipongeza kampuni hiyo kwa hatua hiyo, wakieleza kuwa duka jipya litawawezesha kupata huduma kwa urahisi na ufanisi zaidi. Wamesema kuwa ukubwa wa duka hilo na mpangilio wake wa kisasa, ukilinganisha na duka la awali, umeongeza faraja na kuboresha kwa kiasi kikubwa uzoefu wao wa kupata huduma.

Uzinduzi wa duka hilo kubwa la mfano Dodoma ni sehemu ya mkakati mpana wa Vodacom Tanzania wa kuimarisha huduma kwa wateja, kuongeza ujumuishi, na kuchangia maendeleo ya kijamii na kiuchumi katika maeneo mbalimbali nchini.

Mkurugenzi Mtendaji wa Vodacom Tanzania, Philip Besiimire (wa pili kulia), akisikiliza maelezo kutoka kwa mmoja wa watoa huduma wa duka jipya kubwa la Vodacom mkoani Dodoma baada ya kulizindua. Kulia ni mdau wa Vodacom, Emmanuel Makaki, Mkuu wa Vodacom Kanda ya Kati, Chiha Nchimbi, pamoja na wafanyakazi wa kampuni hiyo.
Mkurugenzi Mtendaji wa Vodacom Tanzania, Philip Besiimire (kushoto), akitazama moja ya simu zinazouzwa ndani ya duka jipya kubwa la Vodacom mkoani Dodoma baada ya kulizindua. Wanaoshuhudia ni wafanyakazi wa duka hilo.

Mkurugenzi Mtendaji wa Vodacom Tanzania, Philip Besiimire (wa pili kushoto), akizungumza na mtoa huduma wa dawati la wateja wenye mahitaji maalumu, Miraji Msita (kulia), baada ya kuzindua duka jipya kubwa la Vodacom mkoani Dodoma. Kushoto ni Mkuu wa Vodacom Kanda ya Kati, Chiha Nchimbi, mdau wa Vodacom, Emmanuel Makaki (kulia), pamoja na wafanyakazi wa kampuni hiyo.

No comments:

Post a Comment