Dar es Salaam, Tanzania — 28 Novemba 2025. Kampuni inayoongoza kwa huduma za mawasiliano nchini, Vodacom Tanzania PLC, imezindua rasmi msimu wa Sikukuu za Mwisho wa Mwaka kwa kuungana na wateja na wafanyabiashara kuwasherehekea kupitia zawadi na matukio ya kijamii. Uzinduzi huo umefanyika katika eneo la Magomeni Sokoni jijini Dar es Salaam, ambako zaidi ya makapu 20 ya sikukuu yenye mahitaji muhimu yaligawiwa kwa wateja na wakazi wa eneo hilo.
Furaha Ya Msimu Yaendelea Nchi Nzima
Utoaji huu wa makapu ya sikukuu ni sehemu ya kampeni pana ya msimu, ambapo Vodacom inatarajia kutembelea mikoa mingine ikiwemo Mwanza, Dodoma, Arusha na Mbeya. Lengo ni kuhakikisha kwamba wateja kutoka maeneo mbalimbali ya nchi wanapata kuguswa na upendo wa msimu huu kupitia zawadi na matukio ya kukutanisha jamii.
Ujumbe Kutoka Vodacom
Akizungumza katika hafla hiyo, Brigita Shirima, Mkurugenzi wa Biashara na Masoko wa Vodacom Tanzania, alisema:
“Kupitia kampeni hii, tunarudisha kwa jamii huku tukiwasherehekea wateja wetu ambao wamekuwa nasi siku zote. Tunataka kila mteja na mfanyabiashara afurahie msimu wa sikukuu na kuhisi thamani ya kushirikiana na Vodacom.”
.jpeg)








.jpeg)




.jpg)




.jpeg)
.jpeg)




.jpeg)


.jpeg)




.jpeg)

