Foreign Exchange Rates

DStv Advert_090724

DStv Advert_090724

SBT Tanzania Advert_291123

Monday 5 August 2024

TCB YASAINI MOU YA MIKOPO NA ZEEA KUSAIDIA WAJASIRIAMALI KUJIKWAMUA KIUCHUMI


Benki ya Biashara Tanzania (TCB) imesaini mkataba wa makubaliano (MOU) na Wakala wa serikali wa uwezeshaji wananchi kiuchumi zanzibar (ZEEA) Makubaliano haya ya kimkakati yanalenga kuanzisha mpango maalum wa mikopo utakaonufaisha makundi maalum wakiwemo wanawake na vijana wanaojihusisha na shughuli za kiuchumi visiwani Zanzibar. Mpango huu unakusudia kuchochea ukuaji wa biashara, ongezeko la ajira, na maendeleo ya kiuchumi katika ukanda huu wa Afrika Mashariki.


Akishuhudia kusainiwa kwa hati hizo jijini Dar es salaam Katibu Mkuu Ofisi ya Raisi Kazi Uchumi na Uwekezaji Zanzibar, Maryam Saadalla amesema tayari shilingi bilioni 2 zimeshakusanywa na Halmashauri Visiwani humo ili kuanza uwezeshaji akiitaka benki ya TCB kuhakikisha inafanya tathmini ya mikopo wanayotoa kwa makundi hayo ili ziweze kurejeshwa kwa wakati na wengine waweze kukopa .

Maryam Saadalla, Katibu Mkuu Ofisi ya Raisi Kazi Uchumi na Uwekezaji Zanzibar.

Kwa upande wake Afisa Mtendaji Mkuu wa TCB, Adam Mihayo amesema Mkataba huu wa makubaliano unathibitisha dhamira ya Benki ya TCB kuwezesha uchumi jumuishi na maendeleo ya kiuchumi kwa ujumla.


Kwa upande wake Mkurugenzi Mtendaji wa ZEEA, Juma Burhan Mohamed amesema wanalenga kuipatia Benki ya TCB kiasi cha shilingi bilioni 1.8 ili waanze utoaji wa mikopo hiyo ambayo itarejeshwa kwa kipindi cha miaka 2.

Lengo la mikopo hiyo ikiwa ni kuvifikia vikundi 75 vyenye wanachama kati ya watano (5) mpaka ishirini (20), ZEEA mpaka sasa imeshasajili vikundi 16 kutoka sekta mtambuka na kupokea maombi ya mkopo yanayofikia wastani wa shilingi milioni 150.

Kwa kutoa mikopo nafuu kwa makundi haya, TCB na Mpango huu wa mikopo umekusudiwa kutia chachu juhudi za kijasiriamali, kuwapa wajasiriamali uthubutu wa kuanzisha na kupanua biashara zao. Malengo ya uwezeshaji huu ni kuwa chanzo cha mabadiliko mengine kama kuimarisha biashara na uchumi.

No comments:

Post a Comment