Foreign Exchange Rates

DStv Advert_020324

DStv Advert_020324

SBT Tanzania Advert_291123

Friday 26 January 2024

WAZIRI WA FEDHA NA WA KILIMO WATETA NA UJUMBE WA NMS INFRASTRUCTURE

Waziri wa Fedha Mhe. Dkt. Mwigulu Lameck Nchemba (Mb), akizungumza kuhusu umuhimu wa uwekezaji katika sekta ya kilimo wakati wa mkutano na ujumbe kutoka Kampuni ya NMS Infrastructure kutoka nchini Uingereza, ikiongozwa na Mratibu wa Kampuni hiyo kwa nchi za Afrika Mashariki, Bw. Tom Vaughan (hayupo pichani), jijini Dodoma. Kulia ni Waziri wa Kilimo, Mhe. Hussein Bashe.
Mkurugenzi wa Maendeleo ya Biashara wa Kampuni ya NMS Infrastructure anayesimamia nchi za Kusini mwa Jangwa la Sahara, Bw. Alistair Johnston (katikati), akizungumza jambo wakati wa Mkutano na Waziri wa Fedha Mhe. Dkt. Mwigulu Lameck Nchemba (Mb) na Waziri wa Kilimo, Mhe. Hussein Bashe (Mb), jijini Dodoma (hawapo pichani), kulia ni Mratibu wa Kampuni hiyo kwa nchi za Afrika Mashariki, Bw. Tom Vaughan.
Waziri wa Kilimo, Mhe. Hussein Bashe, akizungumza jambo kuhusu mpango wa Serikali wa kuongeza nguvu ya uwekezaji katika sekta ya kilimo hususan katika kuongeza uzalishaji na mnyororo wa thamani katika mazao ya kilimo, wakati wa mkutano na ujumbe wa Kampuni ya NMS Infrastructure ya nchini Uingereza, ikiongozwa na Mratibu wa Kampuni hiyo kwa nchi za Afrika Mashariki, Bw. Tom Vaughan (hayupo pichani), jijini Dodoma. Kushoto ni Waziri wa Fedha Mhe. Dkt. Mwigulu Lameck Nchemba (Mb).
Katibu Mkuu wa Wizara ya Fedha, Dkt. Natu El-maamry Mwamba, na Katibu Mkuu wa Wizara ya Kilimo, Bw. Gerald Mweli, wakisikiliza kwa makini wasilisho la Kampuni ya NMS Infrastructure ya nchini Uingereza, kutoka kwa Mratibu wa Kampuni hiyo kwa nchi za Afrika Mashariki, Bw. Tom Vaughan (hayupo pichani), kwenye mkutano wa Ujumbe wa Kampuni hiyo na Waziri wa Fedha Mhe. Dkt. Mwigulu Lameck Nchemba (Mb) na Waziri wa Kilimo, Mhe. Hussein Bashe (Mb), jijini Dodoma.
Baadhi ya wajumbe kutoka Wizara ya Fedha, wakiwa katika mkutano wa Waziri wa Fedha, Mhe. Dkt. Mwigulu Lameck Nchemba (Mb), Waziri wa Kilimo, Mhe. Hussein Bashe (Mb) na Ujumbe wa Kampuni ya NMS Infrastructure ya nchini Uingereza, ulioangazia uwekezaji kwenye sekta ya Kilimo, uliofanyika jijini Dodoma.
Kamishna wa Idara ya Usimamizi wa Madeni, Wizara ya Fedha, Bw. Japhet Justine, akizungumza jambo wakati wa mkutano kati ya Waziri wa Fedha, Mhe. Dkt. Mwigulu Lameck Nchemba (Mb), Waziri wa Kilimo, Mhe. Hussein Bashe (Mb) na Ujumbe wa Kampuni ya NMS Infrastructure ya Uingereza, jijini Dodoma.
Waziri wa Fedha, Mhe. Dkt. Mwigulu Lameck Nchemba (Mb) na Waziri wa Kilimo, Mhe. Hussein Bashe (Mb) wakiwa katika mkutano na Ujumbe wa Kampuni ya NMS Infrastructure ya Uingereza, ulioangazia uwekezaji kwenye sekta ya kilimo, jijini Dodoma.

No comments:

Post a Comment