Foreign Exchange Rates

DStv Advert_090724

DStv Advert_090724

SBT Tanzania Advert_291123

Sunday 13 March 2022

VODACOM YANYAKUA TUZO YA "WOMAN OF THE FUTURE"

Wafanyakazi wa Kampuni ya Vodacom Tanzania PLC wakiwa kwenye picha ya pamoja mara baada ya kunyakua tuzo ya "Woman of the Future" waliyoshinda kwenye maadhimisho ya siku ya wanawake duniani ambapo kampuni hiyo ilishinda kwa kuajiri zaidi ya asilimia 40 ya wanawake kwenye Menejimenti yake. Kampuni ya Mwananchi Communications Ltd waliandaa tuzo za "Rising Woman" zenye lengo la kuwezesha wanawake kuvunja upendeleo kwenye ajira nchini.

Mkurugenzi wa Biashara Vodacom Tanzania PLC, Linda Riwa (kulia), Mkurugenzi wa Rasilimali watu Vodacom Tanzania PLC, Vivienne Penessis (katikati ) na Meneja wa Mawasiliano Vodacom Tanzania PLC, Alex Bitekeye wakiwa kwenye picha ya pamoja mara baada ya kukabidhiwa tuzo ya "Woman of the Future" waliyonyakua kwenye maadhimisho ya siku ya wanawake duniani ambapo kampuni ya Vodacom ilishinda kwa kuwa na zaidi ya asilimia 40 ya wanawake katika menejimenti. Tuzo hizo za The Citizen "Rising Woman" ziliandaliwa na kampuni ya Mwananchi communications Ltd.




No comments:

Post a Comment