Foreign Exchange Rates

DStv Advert_020324

DStv Advert_020324

SBT Tanzania Advert_291123

Wednesday 26 January 2022

DIPLOMATIC SHERRY PARTY IKULU JIJINI DAR ES SALAAM

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan akiongea na Mabalozi wanaoziwakilisha nchi zao hapa nchini pamoja na Wawakilishi wa Mashirika ya Kimataifa katika Sherehe za Mwaka Mpya 2022 kwa Mabalozi (Diplomatic Sherry Party) Ikulu – Dar es Salaam.
Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Balozi Liberata Mulamula akitoa hotuba yake wakati wa Sherehe za Mwaka Mpya 2022 kwa Mabalozi (Diplomatic Sherry Party) Ikulu – Dar es Salaam.
Kiongozi wa Mabalozi nchini ambaye pia ni Balozi wa Visiwa vya Comoro nchini Mhe. Dkt. Ahmada El Badaoui Mohamed akihutubia wakati wa Sherehe za Mwaka Mpya 2022 kwa Mabalozi (Diplomatic Sherry Party) Ikulu – Dar es Salaam.
Sehemu ya Uongozi wa Wizara ya mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki ukifuatilia hotuba ya Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan wakati wa Sherehe za Mwaka Mpya 2022 kwa Mabalozi (Diplomatic Sherry Party) Ikulu – Dar es Salaam.

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan hivi karibuni aliwaalika Mabalozi wanaoziwakilisha nchi zao hapa nchini pamoja na Wawakilishi wa Mashirika ya Kimataifa katika Sherehe za Mwaka Mpya 2022 kwa Mabalozi (Diplomatic Sherry Party) Ikulu – Dar es Salaam.

Pamoja na mambo mengine, katika sherehe hizo Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan alisema Sera Mpya ya Mambo ya Nje itaendelea kuzingatia Diplomasia ya Uchumi na kuakisi maendeleo mapya kama vile uchumi wa bluu, mabadiliko ya tabianchi, uchumi wa kidigitali pamoja kukuza lugha ya Kiswahili kama lugha ya kidiplomasiana kibiashara. 

Awali, Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Balozi Liberata Mulamula aliwahakikishia Mabalozi wanaowakilisha nchi zao hapa nchini pamoja na Waakilishi wa Mashirika ya Kimataifa kuwa Tanzania chini ya Uongozi wa Rais Samia Suluhu Hassan imeendelea kuimarisha uhusiano wake kila wakati.

No comments:

Post a Comment