Foreign Exchange Rates

DStv Advert_090724

DStv Advert_090724

SBT Tanzania Advert_291123

Friday 2 October 2020

BENKI YA NCBA YAONGEZA ZAIDI HUDUMA ZAKE NCHINI, YAFUNGUA MATAWI MAWILI JIJINI MWANZA LEO

Mkuu wa Mkoa wa Mwanza Mhe. John Mongella, akizungumza na waandishi wa habari jijini Mwanza, wakati wa uzinduzi wa matawi mawili ya Benki ya NCBA yaliyopo barabara ya Nyerere na Kenyatta jijini humo leo. Kushoto ni Mkurugenzi Mkuu wa Benki ya NCBA Tanzania Limited, Margaret Karume.
Mkuu wa Mkoa wa Mwanza, Mhe. John Mongella akikata utepe kuzindua rasmi tawi la Benki ya NCBA lililopo mtaa Kenyatta jijini Mwanza leo. Jumla ya matawi mawili yalizinduliwa jijini humo. Wengine kushoto ni Mkurugenzi Mkuu wa Benki ya NCBA Tanzania, Margaret Karume, Katibu Tawala wa Mkoa huo, Mhe. Emmanuel Tutuba (kulia) na nyuma ni Mkurugenzi wa jijini la Mwanza, Mhe. Wakili Kiomoni Kibamba.
Mkurugenzi Mkuu wa Benki ya NCBA Tanzania, Margaret Karume, akizungumza na waandishi wa habari jijini Mwanza wakati wa uzinduzi wa matawi yao yaliyopo barabara ya Nyerere na Kenyatta. Kushoto ni Mkuu wa Mkoa wa Mwanza, Mhe. John Mongella na Katibu Tawala wa Mkoa huo, Mhe. Emmanuel Tutuba.

No comments:

Post a Comment