Foreign Exchange Rates

DStv Advert_090724

DStv Advert_090724

SBT Tanzania Advert_291123

Tuesday 11 September 2018

BENKI YA NBC YAZINDUA KLABU YA WAFANYABIASHARA MJINI MOSHI NA ARUSHA

Mkuu wa Wilaya ya Moshi, Kippi Warioba (wa kwanza kushoto), Mwenyekiti wa Wafanyabiashara wa Moshi, Patrick Boisafi, Meneja wa NBC Kanda ya Kaskazini, Salma Yatera na Mkuu wa Kitengo cha Wafanyabiashara Wadogo na wa Kati wa NBC, Evance Luhimbo wakizindua Klabu ya Wafanyabiashara ya NBC Mjini Moshi hivi karibuni.
Mkuu wa Wilaya ya Moshi, Kippi Warioba (wa pili kushoto mstari wa nyuma), wafanyabiashara, maofisa wa Benki ya NBC na wa serikali pamoja na wahudhuriaji wengine wakijipiga ‘selfie’ mbele ya bango maalumu kuashiria uzinduzi rasmi wa Klabu ya Wafanyabiashara ya NBC iliyopewa jina la NBC B-Club, mjini Moshi Mkoani Kilimanjaro hivi karibuni.
Ofisa Elimu Mkuu wa Mlipakodi wa Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA), Rose Mahendeka (kushoto), akitoa elimu kuhusu masuala mbalimbali ya kodi kwa wafanyabiashara wa mjini Moshi katika semina iliyoandaliwa na benki ya NBC iliyofanyika pamoja na uzinduzi wa Klabu ya Wafanyabiashara wa benki hiyo iliyopewa jina la NBC B-Club, mjini humo mkoani Kilimanjaro hivi karibuni. Klabu hiyo itasaidia utatuzi wa changamoto mbalimbali zinazowakabili wafanyabiashara wadogo na wa kati.
Mkuu wa Kitengo cha Wateja Wadogo na wa Kati wa Benki ya NBC, Evance Luhimbo (kulia), akisalimiana na mmoja wa wafanyabiashara wa Moshi, Rakesh Vara katika semina iliyoandaliwa na benki hiyo ikifanyika pamoja na uzinduzi wa Klabu ya Wafanyabiashara wa benki hiyo iliyopewa jina la NBC B-Club, mjini Moshi mkoani Kilimanjaro hivi karibuni. Klabu hiyo itasaidia utatuzi wa changamoto mbalimbali zinazowakabili wafanyabiashara wadogo na wa kati. 
Meneja Mahusiano wa NBC, William Kallaghe, akizungumza katika semina iliyoandaliwa na NBC kwa wafanyabiashara na wateja wao mjini Arusha iliyofanyika pamoja na uzinduzi wa Klabu ya Wafanyabiashara ya NBC mjini humo hivi karibuni. 
Mkuu wa Wilaya ya Arusha, Gabriel Diqarro, akishikana mikono na Meneja wa Benki ya NBC Tawi la Arusha, Mirage Msuya (kulia) wakati wa uzinduzi wa Klabu ya Wafanyabiashara ya NBC Mkoani Arusha hivi karibuni. Wanaongalia kutoka kushoto ni Meneja wa Kanda ya Arusha wa Benki ya NBC Salma Yatera pamoja na Mkuu wa kitengo wa benki hiyo. 
Meneja wa NBC Kanda ya Kaskazini, Salma Yatera (kulia), akiselebuka pamoja na baadhi ya wafanyabiashara wa mjini Moshi, kusherehekea uzinduzi wa Klabu ya Wafanyabiashara ya NBC mjini humo hivi karibuni.

No comments:

Post a Comment