Foreign Exchange Rates

DStv Advert_020324

DStv Advert_020324

SBT Tanzania Advert_291123

Thursday 16 August 2018

MAKAMU WA RAIS MHE. SAMIA SULUHU HASSAN AWASILI MJINI WINDHOEK, NAMIBIA KUSHIRIKI MKUTANO WA 38 WA WAKUU WA NCHI NA SERIKALI WA SADC

Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Samia Suluhu Hassan amewasili tarehe 15 Agosti 2018 katika uwanja wa ndege wa kimataifa wa Hosea Kutako mjini Windhoek, Namibia ambapo atamwakilisha Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. John Pombe Magufuli katika Mkutano wa Wakuu wa Nchi na Serikali wa Jumuiya ya Maendeleo ya Kusini mwa Afrika (SADC) utakaofanyika tarehe 17 na 18 Agosti 2018. 
Makamu wa Rais, Mhe. Samia Suluhu Hassan akizungumza na mawaziri wa Serikali ya Namibia waliowasili kumpokea katika uwanja wa ndege wa kimataifa wa Hosea Kutako mjini Windhoek, Namibia. wa kwanza kulia ni Naibu Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa, Mhe. Christine Hoebes na wa kwanza kushoto ni Waziri wa Elimu ya juu, Mafunzo na Ubunifu, Mhe. Dkt Itah Kandjii-Murangi.
Makamu wa Rais Mhe. Samia Suluhu Hassan akisalimiana na Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Mhe. Balozi Dkt. Augustine Mahiga mara baada ya kuwasili katika uwanja wa ndege wa Kimataifa wa Hosea Kutako mjini Windhoek, Namibia.

Bofya hapa kwa picha zaidi

No comments:

Post a Comment