Foreign Exchange Rates

DStv Advert_020324

DStv Advert_020324

SBT Tanzania Advert_291123

Wednesday 23 September 2015

SHIRIKA LA NYUMBA LA TAIFA LAZINDUA RASMI MAUZO YA NYUMBA ZA MAKAZI SHANGANI, MTWARA

Kaimu Mkurugenzi wa Mauzo na Masoko wa Shirika la Nyumba la Taifa, Tuntufye Mwambusi akizungumza na waandishi wa habari (hawapo pichani) wakati wa uzinduzi wa mauzo ya nyumba za makazi za Shangani mjini Mtwara.
Nyumba za makazi za Shangani Mtwara kama zinavyoonekana sasa.
Nyumba za makazi za Shangani Mtwara kama zinavyoonekana sasa.
Nyumba za makazi za Shangani Mtwara kama zinavyoonekana zitakapokamilika.
Nyumba za makazi za Shangani Mtwara kama zinavyoonekana zitakapokamilika.
Nyumba za makazi za Shangani Mtwara kama zinavyoonekana zitakapokamilika.
Nyumba za makazi za Shangani Mtwara kama zinavyoonekana zitakapokamilika.
Kwa mara nyingine tena Shirika la Nyumba la Taifa (NHC) Jumatano, 16, Septemba, 2015, limezindua rasmi mauzo ya nyumba katika mradi wake mpya wa Shangani, Mtwara. Ujenzi wa mradi huo ulianza rasmi mwezi Novemba mwaka 2013 na unatarajiwa kukamilika rasmi mwisho wa mwezi ujao, ikiwa ni miezi 24 baada ya kuanza ujenzi. Mradi unatarajiwa kugharimu kiasi cha zaidi ya Sh 4.8 bilioni mpaka utakapomalizika.

Mradi huu upo katika eneo tulivu la Shangani Mkoani Mtwara takribani kilomita moja kutoka katikati ya mji na upo karibu kabisa na bahari ya Hindi. Mradi huu una nyumba 30 za kuuzwa zilizopo kwenye majengo matatu ya ghorofa 5 ukiwa na huduma zote muhimu za kijamii. Usalama pia umezingatiwa kwa wakazi na wanunuzi wa Mradi huu kwa kuweka uzio mkubwa

Nyumba 10 kati ya hizi 30 zimeshafanyiwa booking na Benki Kuu ya Tanzania (BOT). kila nyumba ina vyumba vitatu vya kulala, kimoja kati ya hivyo ni cha kulala kinachojitegemea, sebule iliyoungana na eneo la kula chakula, choo cha umma na jiko kubwa la kisasa. Nyumba hizo zina ukubwa wa aina mbili yaani zile za ukubwa wa mita za mraba 117.2 (sq.m) na zingine za ukubwa wa mita za mraba 182.6

Sifa za ziada za mradi huu ni kuwa na eneo maalum la kukusanyia taka na eneo kubwa la ziada la maegesho ya magari pamoja na Club House.

Kila nyumba itauzwa kwa bei ya TZS 190,127,000 bila VAT na TZS 224,349,860 ikiwa na VAT. Tunawahamasisha na kuwakaribisha Watanzania wote walio nchini na wanaoishi nje ya nchi wafanye mawasiliano na ofisi zetu za Makao Makuu ya Shirika, ofisi zetu za mikoa, au kupitia barua pepe na kukamilisha taratibu mapema kwa ajili ya kuweza kuingia kwenye mchakato.

Uzinduzi wa mauzo ya nyumba za mradi huu ni mfululizo wa uzinduzi wa miradi ya NHC unaolenga kutimiza malengo ya mkakati wa Shirika wa miaka kumi 2015/16 – 2020/25.

Ukiwa mdau na mnunuzi mtarajiwa, ama una ndugu/rafiki anayehitaji kununua nyumba katika mradi huu, tafadhali waweza tumia akaunti nambari 1001962018 iliyopo Bank ABC au wasiliana na kitengo cha mauzo simu namba 0754 444 333; barua pepe: sales@nhctz.com na pia tembelea tovuti ya shirika www.nhctz.com kwa maelezo zaidi.

IMETOLEWA NA:
KITENGO CHA MAWASILIANO NA HUDUMA KWA JAMII
SHIRIKA LA NYUMBA LA TAIFA

No comments:

Post a Comment