Foreign Exchange Rates

DStv Advert_090724

DStv Advert_090724

SBT Tanzania Advert_291123

Wednesday 18 February 2015

BENKI YA NMB YAGAWA MSAADA WA MADAWATI NA MEZA ZA WALIMU WILAYANI HAI


Benki ya NMB imetoa msaada wa madawati 40 na meza za walimu wenye thamani ya sh. milioni 5 katika shule za msingi Mwaramu, iliyomo wilayani humo, huku msaada huo ukiwa umetokana na faida inayopata benki hiyo.

Akiongea baada ya kukabidhi msaada huo, meneja wa benki hiyo kanda ya kaskazini, Vicky Bishubo alisema benki hiyo imeamua kutoa msaada wa madawati hayo baada ya kuona shule nyingi zikikosa madawati na wanafunzi wake wakikaa chini kwenye sakafu.

Alisema kutokana na hali hiyo wanafunzi wengi wamekuwa hawazingatii masomo pindi wawapo darasani kwa sababu ya ukosefu wa vitendea kazi vya madarasani hususani madawati.

"Leo benki ya NMB imeamua kutoa msaada wa madawati 40, meza za walimu na viti wenye thamani ya shilingi milioni 5, tumeamua kufanya hivyo kutokana na uhitaji wa shule husika napenda niwahakikishie kuwa benki yenu imetenga zaidi ya shilingi bilioni 1 kwa ajili ya kuirudishia jamii faida kidogo inayopata’’alisema Bishubo

Bishubo aliongeza kuwa,benki hiyo iliamua kutoa msaada wa madawati hayo ya wanafunzi ili kuweza kutoa motisha kwa wanafunzi hao kuweza kusoma kwa bidii kwa madai kuwa kutokuwepo kwa vitendea kazi mashuleni ni moja ya sababu zinazopelekea wanafunzi wengi kufeli.

“Msaada huu wa madawati umetokana na faida kidogo ambazo benki inapata hivyo tumeona katika faida hizo ni jambo jema kutoa msaada wa aina hii kwa ajili ya kuweza kuendeleza watoto kielimu kwani wao ndiyo Taifa la kesho,” alisema Bishubo.

Naye Meneja wa NMB tawi la Hai Merdadi Malisa alisema benki hiyo imejipanga kusaidia jamii katika wilaya hiyo kwa kutoa msaada pindi inapohitajika na kuwataka wananchi kufungua akanti katika benki hilo ili kuiwezesha benki hiyo kupata faida zaidi.

Kwa upande wake Mkuu wa Hai, Novatus Makunga aliipongeza benki ya NMB kwa kutoa msaada huo na kuwataka wadau wengine wa elimu kuiga mfano wa benki hiyo kwa kutoa mchango kama huo ili kupunguza ya madawati wilayani huo.

Alisema wilaya ya Hai inakabiiwa na changamoto mbalimbali ikiwemo ya upungufu wa madawati hata hivyo alisema taitizo hilo lipo kwa baadhi ya shule za msingi na wilaya ipo kwenye mkakati wa kukabiliana nalo.

"Changamoto ya madawani ipo sana katika wilaya yetu ya Hai ila tunajitahidi kukabiliana nayo kwa kuwatumia wadau mbalimbali hususani nyie wa NMB, najua benki itakuwa imepokea maombi mengi lakini tunawapongeza kwa kuona umuhimu wa kutoa katika shule ya msingi Mwaramu iliyopo wilaya yangu", alisema.

Aliwataka wadau wengine wa elimu kuiga mfano wa benki ya NMB, kwa kuisaidia serikali kupunguza changamoto zilizopo kwenye shule mbalimbali hapa nchini hasa za msingi ambako ndiko tatizo kubwa lilipo.

"Kupatikana kwa madawati haya naimani kutaongeza ari ya ufaulu kwa wanafunzi sambamba na walimu kuongeza ari ya ufundishaji katika shule hii’’alisema Makunga

Habari hii kwa hisani ya libeneke la kaskazini blog

No comments:

Post a Comment