Foreign Exchange Rates

DStv Advert_090724

DStv Advert_090724

SBT Tanzania Advert_291123

Monday 20 October 2014

WAFANYAKAZI WA NBC WAJITOLEA MUDA WAO KUFANYA KAZI ZA KIJAMII

Mmoja wa wafanyakazi wa benki ya NBC, Noela Ishebabi (kulia) akitoa mada kuhusu umuhimu wa kuweka akiba kwa wanafunzi wa shule ya Msingi Maweni, Kigamboni nje kidogo ya Jiji la Dar es Salaam mwishoni mwa wiki iliyopita ikiwa ni sehemu ya mpango wa wafanyakazi wa benki hiyo kujitolea muda wao kufanya kazi za kijamii  iitwayo ‘Make a Difference Day’.

Meneja mikopo kitengo cha makampuni wa benki ya NBC, Gamali Mongi  (kushoto) akizungumza kuhusu umuhimu wa kuweka akiba kwa wanafunzi wa shule ya Msingi Maweni, Kigamboni nje kidogo ya Jiji la Dar es Salaam mwishoni mwa wiki iliyopita ikiwa ni sehemu ya mpango wa wafanyakazi wa benki hiyo kujitolea muda wao kufanya kazi za kijamii  iitwayo ‘Make a Difference Day’.

Mmoja wa wafanyakazi wa benki ya NBC, Yuda Mayunga (kulia) akizungumza kuhusu umuhimu wa kuweka akiba kwa wanafunzi wa shule ya Msingi Maweni, Kigamboni nje kidogo ya Jiji la Dar es Salaam mwishoni mwa wiki ikiwa ni sehemu ya mpango wa wafanyakazi wa benki hiyo kujitolea muda wao kufanya kazi za kijamii  iitwayo ‘Make a Difference Day’.

Mmoja wa wafanyakazi wa benki ya NBC, Kulwa Kissinza (kushoto) akizungumza kuhusu umuhimu wa kuweka akiba kwa wanafunzi wa shule ya Msingi Maweni, Kigamboni nje kidogo ya Jiji la Dar es Salaami ikiwa ni sehemu ya mpango wa wafanyakazi wa benki hiyo kujitolea muda wao kufanya kazi za kijamii  uitwao ‘Make a Difference Day’.

Mkuu wa Kitengo cha Marejesho ya mikopo mikubwa wa Benki ya NBC, Faith Majiwa (wa tatu kushoto) akikata utepe kuashiria makabidhiano ya meza mbili za walimu na viti vyake vilivyotolewa na benki hiyo kwa walimu wa Shule ya Msingi Maweni, Kigamboni nje kidogo ya Jiji la Dar es Salaam. Wengine kutoka kulia ni mwalimu mkuu msaidizi wa shule hiyo, Martha Silavwe na Mkuu wa Kitengo cha Mikopo Mikubwa, Tonny Minns. Katika hafla hiyo pia wafanyakazi wa NBC walitoa elimu ya masuala ya kifedha kwa wanafunzi wa shule hiyo ikiwa ni sehemu ya mpango wa wafanyakazi wa benki hiyo kujitolea muda wao kufanya kazi za kijamii  iitwayo ‘Make a Difference Day’.

Mkuu wa Kitengo cha Mikopo Mikubwa wa Benki ya NBC, Tony Minns (kushoto) akilakiwa na baadhi ya wanafunzi wa shule ya msingi Maweni wakati wafanyakazi wa idara hiyo walipotembelea shule hiyo kutoa elimu ya masuala ya kifedha kwa wanafunzi wa shule hiyo ikiwa ni sehemu ya mpango wa wafanyakazi wa benki hiyo kujitolea muda wao kufanya kazi za kijamii  iitwayo ‘Make a Difference Day’.

Baadhi ya wanafunzi wa shule ya msingi Maweni wakisoma vipeperushi vyenye maelezo ya huduma zitolewazo na benki ya NBC wakati wa hafla hiyo. Kutoka kushoto ni, Sililo Ngairo, Doto Emanuel na Nuru Hamadi. (PICHA NA PETER MGONGO).

No comments:

Post a Comment