Foreign Exchange Rates

DStv Advert_090724

DStv Advert_090724

SBT Tanzania Advert_291123

Monday 23 June 2014

MFUKO WA SME IMPACT FUND (SIF) WAZINDULIWA RASMI TANZANIA

SME Impact Fund (SIF)-Mfuko wa wafanyabiashara wadogo na wa kati umezinduliwa rasmi (19 Juni, 2014) ndani ya hoteli ya New Africa, jijini Dar es salaam na kundi la kampuni za Match Maker Group. Mjasiriamali mkongwe na Mwenyekiti wa Private Sector Foundation (PSF) Dk. Reginald Mengi alikuwepo kama mgeni rasmi wa hafla hiyo.

Kundi la kampuni za Match Maker Group (MMG) lina miliki kampuni tanzu mbili ikiwemo Match Maker Associates Ltd (MMA) na Match Maker Fund Management (MMFM). Ambapo MMA Ltd ndio kampuni mama, yenye kushughulika na huduma za ushauri fasaha kibiashara kwa zaidi ya miaka kumi sasa.

“Match Maker Associates Ltd ndio msingi wa Match Maker Group, mimi na Henri Van Der Land tulisajili na kuendesha MMA mnamo mwaka 2003, kama kampuni ya sekta binafsi inayotoa huduma za ushauri fasaha na mafunzo ya biashara. Sasa miaka kumi baadae tumeshuhudia kukua vizuri kwa MMA Ltd upande wa bidhaa na wateja wake. MMA inatoa huduma zake hususani ndani ya nchi za Mashariki na Kusini mwa Afrika. Mpaka sasa, MMA Ltd imeshatoa huduma za ushauri fasaha na mafunzo ya biashara kwenye miradi 140 ndani ya nchi zaidi ya 15.”Alifafanua Bw Peniel Uliwa, Mkurugenzi Mshiriki wa MMG wakati akitoa hotuba kuwataarifu waalikwa juu ya MMG na SIF.

Match Maker Fund Management Ltd ilisajiliwa mwaka 2011 ikiwa na lengo la kuwezesha wajasiriamali wadogo na wa kati kukuza biashara zao. Kwa kuboresha viwango vya kazi na ubora wa huduma kwenye mlolongo wa sekta zao za biashara; wanapopata huduma tekelevu za ushauri fasaha kibiashara na huduma za kifedha kutoka MMFM. Mfuko wa ‘SME Impact Fund’ (SIF) umesajiliwa Uholanzi ambapo MMFM imepewa dhamana ya kutekeleza maslahi yake kibiashara nchini Tanzania.

“Chanzo cha kuwa na mfuko kama SIF kilitokana na malalamiko mbalimbali tuliyokuwa tunakumbana nayo kwenye shuguli zetu ndani ya MMA Ltd. Ambapo wafanyabiashara wadogo na wakati kwenye sekta ya kilimo walituambia wanashindwa kuendeleza kibiashara zao kutokana na ugumu wa upatikanaji wa mitaji ya kuendeleza biashara zao.  Hapa tukagundua kuna tatizo kubwa linalokosesha ukuaji kiuchumi kwa wajasiliamali hawa na vivyo kuwakosesha kufikia ndoto zao kibiashara. Basi tukaanza mchakato na hatimaye kuanzisha na kusajili MMFM Ltd”. Alielezea Bw Henri Van Der Land, Mkurugenzi mshiriki wa MMG mzawa wa Uholanzi anayekaa na kufanya kazi nchini Tanzania kwa zaidi ya miaka 20 sasa.
Mfuko wa ‘SME Impact Fund’ unatoa mikopo kwa wafanyabiashara na wajasiriamali wadogo na kati ndani ya minyororo ya thamani katika sekta ya kilimo. Ikiwemo wasindikaji mazao, viwanda vya maziwa, mafuta n.k. Mikopo inatolewa kwa wale wajasiriamali wanaoongeza thamani wenye uhitaji wa mtaji au uwekezaji zaidi kwenye biashara zao. Mikopo ya SIF huanzia toka millioni 100 TSHS mpaka Bilioni 1 TSHS, licha ya hii Mfuko wa SIF ndani ya timu ya MMFM hutoa huduma za ushauri fasaha wa biashara kwa wateja wao wote ili kuwawezesha kuendesha biashara zao kwa faida.

“MMG wamenipa taarifa kuwa kwenye utafiti wao kabla ya kubaini mfuko huu, waligundua kuna tabaka wanaloliita ‘missing middle’. La wafanyabiashara na wajasiriamali wadogo na wa kati nchini ambao hawapati huduma stahili kirahisi kwenye taasisi rasmi za fedha kama benki. Hili lilithibitishwa kwenye mikutano ya wawekezaji mbalimbali nchini iliyofanyika mwaka jana. Ambapo wajasiriamali wadogo na wa kati takriban 150, walipewa fursa ya kuelezea miradi yao kwa taasisi rasmi za fedha mbalimbali nchini na zaidi ya asilimia 80 ya hawa walifurahi sana kukutana na SIF.” Aliongezea mgeni rasmi Dk Reginald Mengi.

Hadi sasa SIF imeshatoa mikopo 9 yenye thamani ya 1.5 Billion Tshs (Euro 650,000) toka mwezi Julai mwaka jana. Kwenye uzinduzi wa mfuko huu baadhi ya wafanyabiashara hawa walikuwepo wakitoa shuhuda na taarifa fupi juu ya biashara zao; kupitia mkanda wa video uliyoonyeshwa kwa wageni wote kwenye uzinduzi huo.

Wajasiriamali wote waliopokea mikopo ya mfuko wa SIF ni watanzania na wameonyesha uzalishaji endelevu kwa technolojia za kisasa wakitazamia kuwa biashara zao zitatoa faida kwenye sekta nzima ya kilimo. Sambamba na vigezo vya SIF, wateja wake wanalazimika kufikia viwango vilivyowekwa kwenye kanuni za kiuchumi, mazingira na jamii za mfuko huu (SEEC).

“Naamini kabisa kwamba mfuko wa SIF ambao tunauzindua rasmi leo, umekuja nchini kwa muda muafaka. Ikiwa ni sambamba na kauli ya taifa ya Kilimo Kwanza na mikakati na miradi mingine ya kukuza biashara za sekta binafsi na za jamii nchini.” Aliongezea Dk Reginald Mengi kwenye hotuba yake kabla ya kuzinduliwa rasmi mfuko huu.

MMFM inawakaribisha wawekezaji binafsi na taasisi mbalimbali Tanzania, kuwekeza kwenye mfuko huu kauli iliyopewa msisitizo na mgeni rasmi. “Nawaalika wawekezaji Tanzania kuungana mkono na wawekezaji wa SIF ili kufanikisha mpango huu bora wa huduma za fedha na ushauri fasaha kibiashara.”  Alimalizia Dk Reginald Mengi.
Mfuko wa SIF unatarajia ndani ya miaka kumi ya uwepo wake, kuwa utatoa mikopo kwa zaidi ya wafanyabiashara 150 nchini. Ikitoa fursa za nyongeza za kazi kwenye sekta ya kilimo na chakula zipatazo 1000, ikiwemo na ongezeko la mapato kwa wakulima wadogo wapatao 50,000. Hii yote ikiambatana na utekelezaji wa mifumo bora ya kilimo kwa wadau hawa. Pia wawekezaji wote ndani ya mfuko wa SIF watategemea kupata marejesho ya mtaji wao na riba baada ya miaka kumi, wakati mfuko huu utasitishwa.

No comments:

Post a Comment