Foreign Exchange Rates

CRDB Bank Advert_070325

Friday, 30 January 2026

MAGARI YA HUDUMA YA NMB "BANK ON WHEELS" YAFIKIA 15 KUCHOCHEA UJUMUISHAJI WA KIFEDHA

Msajili wa Hazina, Nehemiah Mchechu (wa pili kulia), akikata utepe kuashiria uzinduzi wa magari manane ya “Bank on Wheels” — matawi ya benki yanayotembea yatakayotoa huduma za kibenki mitaani, vijijini na katika minada — ikiwa ni sehemu ya dhamira ya Benki ya NMB ya kuwafikia Watanzania mahali walipo. Uzinduzi huo ulifanyika jijini Dar es Salaam. Wa tatu kutoka kulia ni Mkurugenzi Mtendaji na Afisa Mtendaji Mkuu wa Benki ya NMB, Ruth Zaipuna; kulia ni Mjumbe wa Bodi ya Wakurugenzi wa Benki ya NMB, Benson Mahenya; wa nne kutoka kulia ni Mjumbe wa Bodi ya Wakurugenzi wa Benki ya NMB, Prof. Sylvia Temu; na kushoto ni Afisa Mkuu wa Fedha wa NMB, Juma Kimori.
Msajili wa Hazina, Nehemiah Mchechu (kulia), na Mkurugenzi Mtendaji na Afisa Mtendaji Mkuu wa Benki ya NMB, Ruth Zaipuna (wa pili kulia), wakitoka katika hafla ya uzinduzi wa magari manane ya “Bank on Wheels” — matawi ya benki yanayotembea yatakayotoa huduma za kibenki mitaani, vijijini na katika minada — ikiwa ni sehemu ya dhamira ya benki hiyo ya kuwafikia Watanzania mahali walipo. Kushoto ni Afisa Mkuu wa Fedha wa NMB, Juma Kimori, na wa pili kushoto ni Mjumbe wa Bodi ya Wakurugenzi wa Benki ya NMB, Prof. Sylvia Temu.

Benki ya NMB imeendelea kuimarisha juhudi zake za ujumuishaji wa kifedha nchini baada ya idadi ya magari yake yanayotoa huduma za kifedha—maarufu kama Bank on Wheels—kufikia jumla ya magari 15.

Ongezeko hilo limetokana na uzinduzi rasmi wa magari mapya nane, yaliyobuniwa kama matawi yanayotembea ili kuhakikisha huduma za benki zinawafikia wananchi moja kwa moja, hususan katika maeneo yenye changamoto ya upatikanaji wa matawi ya kawaida kama vijijini, masokoni, minada ya mifugo na vituo vya biashara vya mbali.

Magari haya hayatoi tu huduma za kifedha, bali pia hutoa elimu ya kifedhaufunguaji wa akauntihuduma za mikopomalipo ya kidijitali pamoja na ushauri wa kibiashara, kwa urahisi na ukaribu zaidi kwa wananchi.

Uzinduzi wa Bank on Wheels unaonesha dhamira ya NMB katika kuimarisha ujumuishaji wa kifedha na kutekeleza mkakati wake wa kupeleka huduma za benki karibu zaidi na wananchi, kwa kutumia teknolojia na mbinu bunifu ili kuchochea maendeleo ya kiuchumi, hususan vijijini na katika jamii zisizo rasmi.

Hatua hiyo ilikuwa sehemu ya uzinduzi wa Ajenda 2030, Mpango Mkakati wa Kati wa NMB kwa kipindi cha 2026–2030, unaolenga, pamoja na mambo mengine, kupanua ujumuishaji wa kifedha na kuharakisha maendeleo ya kijamii na kiuchumi nchini.

Zoezi hilo lilisimamiwa na Msajili wa Hazina, Bw. Nehemiah Mchechu, aliyeipongeza NMB kwa mchango wake katika ujenzi wa taifa na kuboresha maisha ya Watanzania kupitia suluhisho bunifu na jumuishi za kifedha.

Akizungumza kabla ya uzinduzi huo, Mkurugenzi Mtendaji na Afisa Mtendaji Mkuu wa NMB, Bi. Ruth Zaipuna, alisema kuwa magari hayo yamebuniwa mahsusi ili kutoa huduma rasmi za kifedha moja kwa moja kwa jamii zisizo na matawi ya benki, ikiwemo vijiji vya mbali, masoko na maeneo ya biashara kama minada.

“Haya siyo magari tu, ni milango ya fursa. Yanawawezesha wakulima, wafanyabiashara wadogo, wafugaji na wajasiriamali kupata huduma za akiba, mikopo, malipo na ushauri wa kifedha bila usumbufu wa kusafiri umbali mrefu au gharama kubwa,” alisema Bi. Zaipuna.

Kupitia huduma hii, mfanyabiashara hahitaji kutumia siku nzima kusafiri kwenda benki kuweka fedha, wala mkulima kusubiri siku ya soko ijayo ili kufungua akaunti. Badala yake, benki inamfuata mteja moja kwa moja mahali alipo.

Aidha, Bi. Zaipuna aliongeza kuwa mpango huo unaakisi imani thabiti ya NMB kwamba ujumuishaji wa kifedha lazima uwafikie wananchi, hasa wale walioko katika sekta zisizo rasmi, ambazo ndizo mhimili wa ukuaji wa uchumi wa Tanzania.

Huduma ya Bank on Wheels pia imekuwa nyenzo muhimu katika kutoa elimu ya kifedha na kuwajumuisha wananchi katika mfumo rasmi wa kifedha, sambamba na kutekeleza mkakati wa Village Banking, unaolenga kupeleka huduma za benki karibu na wananchi.

Mkakati huo ni miongoni mwa nguzo kuu za Ajenda 2030, inayolenga kupanua wigo wa huduma za kifedha, kuhamasisha ujasiriamali na kuharakisha mabadiliko ya kijamii na kiuchumi nchini.

Kupitia magari haya ya huduma, wananchi wanawezeshwa kufungua akauntikufanya miamala ya fedhakukopa, pamoja na kusajili huduma za kidijitali, kwa urahisi na usalama zaidi.

No comments:

Post a Comment