Foreign Exchange Rates

CRDB Bank Advert_070325

Selcom Pesa Advert_110225

Selcom Pesa Advert_110225

Standard Chartered Advert_300125

Standard Chartered Advert_300125

Saturday, 11 October 2025

STANBIC YATOA MSAADA WA VIFAA TIBA VYENYE THAMANI YA SH. MIL. 60 KWA HOSPITALI YA TUMBI

Mkuu wa Kitengo cha Wateja Binafsi na Wateja Maalumu wa Benki ya Stanbic, Omari Mtiga, akizungumza wakati wa hafla ya makabidhiano ya vifaa tiba.
Mkuu wa Kitengo cha Wateja Binafsi na Wateja Maalumu wa Benki ya Stanbic, Omari Mtiga (mwenye fulana ya bluu), akipeana mkono na Mganga Mfawidhi wa Hospitali ya Rufaa ya Tumbi, Dkt. Amani Malima, wakati wa makabidhiano ya vifaa tiba vyenye thamani ya zaidi ya shilingi milioni 60 kutoka Benki ya Stanbic, ikiwa ni sehemu ya maadhimisho ya Wiki ya Huduma kwa Wateja na pia ya maadhimisho ya Miaka 30 ya benki hiyo tangu ianze kutoa huduma nchini.

Pwani, Oktoba 10, 2025 — Benki ya Stanbic imekabidhi msaada wa vifaa tiba vyenye thamani ya Shilingi milioni 60 kwa Hospitali ya Rufaa ya Mkoa wa Pwani – Tumbi, ikiwa ni sehemu ya juhudi zake za kuboresha huduma za afya nchini.

Msaada huo, unaojumuisha kompyuta, vitanda, viti vya wagonjwa (wheelchairs), matoroli, na vifaa vya usafi, ulikabidhiwa na Mkuu wa Kitengo cha Wateja Binafsi na Wateja Maalumu wa Stanbic BankBw. Omari Mtiga, kwa niaba ya benki hiyo, na kupokelewa na Mganga Mkuu wa Hospitali ya TumbiDk. Amani Malima.

Akizungumza wakati wa hafla hiyo ya makabidhiano, Bw. Mtiga alisema kuwa msaada huo ni sehemu ya mpango endelevu wa uwajibikaji wa kijamii (CSR) wa Stanbic Bank, unaolenga kurudisha fadhila kwa jamii, sambamba na maadhimisho ya Miaka 30 ya Kukua Pamoja tangu benki hiyo ianze kutoa huduma nchini Tanzania.

Tunatambua mchango mkubwa wa sekta ya afya katika ustawi wa jamii. Kupitia msaada huu, tunalenga kusaidia hospitali kutoa huduma bora zaidi kwa wagonjwa na kuongeza ufanisi wa watoa huduma. Hii ni moja ya njia tunazosherehekea miaka 30 ya kukua pamoja na Watanzania,” alisema Bw. Mtiga.

Kwa upande wake, Mganga Mkuu wa Mkoa wa Pwani, Dk. Kusirya Ukio, aliishukuru benki hiyo kwa mchango huo, akibainisha kuwa vifaa hivyo vitasaidia kuongeza ufanisi katika utoaji wa huduma kwa wagonjwa.

Msaada huu umekuja wakati muafaka, kwani hospitali inakabiliwa na changamoto ya upungufu wa baadhi ya vifaa muhimu. Tunawashukuru Stanbic Bank kwa moyo huu wa kizalendo,” alisema Dk. Ukio.

Hafla hiyo pia ilikuwa sehemu ya maadhimisho ya Wiki ya Huduma kwa Wateja 2025, inayoongozwa na kaulimbiu “Mission Possible”, ambapo wafanyakazi wa Stanbic Bank walijitolea kufanya usafi katika baadhi ya maeneo ya hospitali kama sehemu ya mchango wao kwa jamii.

Mkuu wa Kitengo cha Huduma kwa Wateja wa Benki ya Stanbic, Mariam Maumba, akiongoza wafanyakazi wa benki hiyo katika zoezi la kufanya usafi katika Hospitali ya Rufaa ya Tumbi, Kibaha, mkoani Pwani, ikiwa ni sehemu ya maadhimisho ya Wiki ya Huduma kwa Wateja.

No comments:

Post a Comment