
Benki ya NMB imeshiriki na kudhamini Jukwaa la Kujadili Masuala ya Maji lililofanyika jijini Dar es Salaam, ikiwa ni sehemu ya maadhimisho ya Wiki ya Maji yanayoendelea nchini. Jukwaa hilo limewaleta pamoja wadau mbalimbali wa sekta ya maji ili kujadili mustakabali wa usimamizi, uhifadhi, na uendelezaji wa rasilimali za maji.
Katika hafla hiyo, Katibu Mkuu Kiongozi na Katibu wa Baraza la Mapinduzi Zanzibar, Mhandisi Zena Ahmed Said, aliongoza mkutano huu wa wadau, ambapo benki ya NMB iliwakilishwa na Meneja Mahusiano Mwandamizi wa Huduma za Serikali, Irene Masaki. Katika mkutano huo, Bi. Irene alieleza jinsi NMB inavyojikita katika kusaidia miradi ya maendeleo, ikiwemo sekta ya maji, kupitia huduma zake za kifedha zinazolenga taasisi za umma na sekta binafsi.
No comments:
Post a Comment