Foreign Exchange Rates

DStv Advert_090724

DStv Advert_090724

SBT Tanzania Advert_291123

Tuesday 21 February 2023

PROMOSHENI YA PILSNER YA ‘KAPU LA WANA’ YAKABIDHI PIKIPIKI, ZAWADI KWA WASHINDI MIKOA 3

Washindi wa promosheni ya bia ya Pilsner Lager ya kampuni ya bia ya Serengeti Breweries ijulikanayo kama 'Kapu la Wana' kutokea kanda ya Kaskazini wakionesha zawadi zao zikiwemo televisheni na simu janja baada ya hafla ya makabidhiano ya zawadi hizo yaliyofanyika siku ya jumamosi bar ya Kili time mjini Arusha.

Mshindi wa promosheni ya bia ya Pilsner Lager ya kampuni ya bia ya Serengeti Breweries ijulikanayo kama 'Kapu la Wana' kutokea kanda ya Kusini, Justine Mwaipaja akionesha zawadi ya televisheni aliyoshinda baada ya kushirikia kwenye promosheni hiyo. Hafla ya makabidhiano ya zawadi yalifanyika kwenye bar ya Kiteputepu Uyole, Mbeya.

Washindi wa promosheni ya bia ya Pilsner Lager ijulikanayo kama ‘Kapu la Wana’ inayoendeshawa na kampuni ya bia ya Serengeti Breweries Limited (SBL), wakionyesha zawadi zao wakati wa hafla ya makabidhiano iliyofanyika mkoani Mwanza siku ya Jumamosi. Kushoto ni Neema Abdallah, (mshindi wa televisheni), kulia ni Neema Mathias (mshindi wa pikipiki), wa pili kulia ni Hassan Joel (mshindi wa simu). Makabidhiano hayo yalifanywa na Meneja Masoko wa SBL kanda ya Ziwa, Ronald Lyatuu (wa pili kushoto).

Dar es Salaam, Jumamosi Februari 18, 2023: Kampuni ya Bia ya Serengeti (SBL) kupitia promosheni ya bia yake ya Pilsner Lager ijulikanayo kama ‘Kapu la Wana’ imekabidhi zawadi kwa washindi 7 wa droo ya kwanza ya promosheni hiyo kutoka mikoa ya Arusha, Mwanza na Mbeya. Zawadi hizo ni pamoja na pikipiki, televisheni na simu janja.

Katika washindi 7, washindi 3 walijishindia televisheni, washindi wengine 3 walijishindia simu janja na mmoja alishinda pikipiki. Makabidhiano ya zawadi hizo yalifanyika kanda ya Ziwa, Kaskazini na Kusini ambapo promosheni hiyo inafanyika.

Waliojishindia simu janja ni Agatha Mvwango (Mbeya), Eli Elias (Arusha) na Hassan Joel (Mwanza), washindi 3 wa televisheni ni Justine Mwaipaja (Mbeya), Neema Abdallah (Mwanza) na Selina Panga (Arusha). Mshindi wa zawadi ya pikipiki ni Neema Mathias (Mwanza).

Akizungumza kwenye makabidhiano ya pikipiki kwa mmoja wa washindi wa promosheni ya ‘Kapu la Wana’, yaliyofanyika Spears Bar eneo la Magu jijini Mwanza Meneja Masoko wa SBL kanda ya Ziwa, Ronald Lyatuu alimpongeza mshindi wa pikipiki na kusema kuwa promosheni hiyo ilianzishwa kwa dhumuni la kuwawezesha wanywaji wa bia hiyo ambao ni wachapa kazi kwa kuwapa zawadi mbalimbali baada ya kushiriki kwenye promosheni hiyo, “hii ni mara ya pili tunafanya promosheni hii na kupitia promosheni hii tunataka kuwapa wateja wetu nafasi ya kuboresha maisha yao kwa namna moja au nyingine, kwa mfano mshindi wa hii pikipiki anaweza kuamua kutumia pikipiki hii kumuongozea kipato au vyovyote atakavyoamua kulingana na mahitaji yake.”

Alitoa wito kwa wanywaji wa bia hiyo walio kanda ya Ziwa, Kusini na Kaskazini kuendelea kushiriki kwenye promosheni hiyo na kuwa kwenye nafasi ya kujishindia zawadi mbalimbali kupitiia promosheni hiyo itakayofanyika kwa muda wa wiki 8. Promosheni hiyo iliyozinduliwa Februari 02 itatoa zawadi za simu janja, televisheni, pikipiki na zawadi ya gari kutolea mwishoni mwa promosheni.

Akielezea jinsi ya kushiriki, Marando alisema, “mteja atahitaji kununua bia ya Pilsner, halafu atapata kadi ya kukwangu, ikwangue, kama zawadi ni bidhaa kama fulana, kofia, n.k utazawadiwa papo hapo na kama zawadi uliyoikwangua ni nambari maalum, itume kupitia ujumbe mfupi wa maneno (SMS) kwa namba 15320 mfano: Andika Kapu 4321 Iringa (Acha nafasi. Utapokea ujumbe mfupi wa maneno (SMS) kudhibitisha ushiriki wako.”

Kwa upande wake, mshindi wa pikipiki, Neema Mathias alishukuru SBL na kuwapongeza kwa kuandaa promosheni ya ‘Kapu la Wana’ ambayo ni maalum kwa kuwawezesha watanzania wanaotaka kuboresha maisha yao, “nimefurahi sana kuwa mshindi wa hii pikipiki, natarajia kuitumia inisaidie kujiongezea kipato, nawashukuru sana SBL kwa kutuletea promosheni hii kwani kupitia zawadi hii naamini naenda kubadilisha maisha yang una familia yangu kiuchumi.”

Kwa upande wa washindi wa mkoa wa Arusha, makabidihianao ya zawadi za simu janja na televisheni yalifanyikia Kili Time Bar, eneo la Ngusero. Na kwa washindi kwa Mbeya, makabidhiano ya zawadi za televisheni na simu janja yalifanyikia Kiteputepu Bar, iliyopo eneo la Roma Kyela mjini.

Hii ni mara ya pili bia ya Pilsner imekuja na promosheni hii ya ‘Kapu la Wana’ na imetenga zaidi ya Tsh. 36 milioni kwa washindi 22 wa kampeni hiyo.

Kwa mawasiliano zaidi, wasiliana na:

Rispa Hatibu
Meneja Mawasiliano, SBL
Simu: 0685 260 901
Barua Pepe: RISPA.HATIBU@diageo.com

No comments:

Post a Comment