Foreign Exchange Rates

DStv Advert_090724

DStv Advert_090724

SBT Tanzania Advert_291123

Friday 18 March 2022

NAIBU SPIKA AIPONGEZA NMB KUWAKUMBUKA WAMACHINGA

Afisa Mkuu wa Wateja Binafsi na Biashara Benki ya NMB, Filbert Mponzi, akimkabidhi Naibu Spika wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mussa Azzan Zungu, moja kati ya kompyuta mpakato 5 zilizotolewa na Benki ya NMB kwa ajili ya Shirikisho la Umoja wa Machinga Tanzania (SHIUMA). Kushoto ni Katibu wa Machinga Kariakoo, Thabit Maloka na kulia ni Meneja Mahusiano Biashara za Serikali Benki ya NMB, Mkunde Joseph.

Naibu Spika wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mussa Hassan Zungu ambaye pia ni Mbunge wa Jimbo la Ilala jijini Dar es Salaam, ameishukuru Benki ya NMB kwa kulikumbuka kundi la wafanyabishara ndogo ndogo nchini maarufu Wamachinga na kuwasaidia kukua.

Benki ya NMB ilimkabidhi Naibu Spika laptop 5 zenye thamani ya Tsh. Milioni 7.5 kusaidia upatikanaji wa database wa kundi hilo.
Baada ya kupokea vifaa hivyo, Mh. Mussa Hassan Zungu alivikabidhi kwa viongozi wa SHIUMA, tawi la Ilala kwa ajili ya matumizi ya kiofisi ikiwemo kuweka Kanzi Data(database), ili iwe rahisi kutambulika na kujua shughuli wanazofanya popote walipo nchini.

Zungu ameisifu NMB kuwa ni benki ya kipekee iliyoonyesha kwa vitendo kujali maisha ya wafanyabiashara wadogo, kwa kuwasaidia mitaji na kuangalia ukuaji wao.


Afisa Mkuu wa Wateja Binafsi NMB, Filbert Mponzi alisema vifaa hivyo ni mwendelezo wa makubaliano waliyoingia kati yao na SHIUMA, lengo ni kutengeneza Kanzi Data itakayowasaidia kujulikana kirahisi na kufikika.




Pia, angependea kuona Wamachinga wamesajiliwa, wawe rahisi kufikika.

Alibainisha kuwa pamoja na makabidhiano ya vifaa hivyo, NMB imeendelea kushirikiana na kundi hilo la wafanyabiashara wadogo tangu mwaka 2000. Kwa wastani, benki ya NMB hutoa mikopo ya thamani ya Sh Bil 50 kila mwezi kwa kundi hilo la wafanyabishara wadogo wakiwemo Wamachinga.

Kwa upande wake Katibu wa Wamachinga Kariakoo, Thabit Maloka aliyemwakilisha Mwenyekiti wa SHIUMA Taifa, alisema wamepata faraja kubwa kwa msaada huo kutoka NMB, wanaamini hayo ni matunda ya Serikali ya Awamu ya Sita chini ya Rais Samia Suluhu Hassan kutokana na ahadi aliyowapa kuwashika mkono.

Alibainisha kuwa wanaamini huo ni mwanzo tu, kwani wanajua mazuri yanakuja. Ambapo aliuomba uongozi wa NMB kufikiria kuongeza msaada zaidi ikiwemo kufanya ukarabati wa majeng ya ofisi zao za Ilala jijini Dar es Salaam pamoja na kuwapa mafunzo ya ujasiriamali.

Kompyuta hizo tano zinakwenda kujenga mifumo ya mawasiliano, ufuatiliaji na tathmini katika shughuli za Wamachinga pamojaa na kuwasaidia Wamachinga kuwa na mfumo mzuri wa kufanya biashara zao.

No comments:

Post a Comment