Foreign Exchange Rates

DStv Advert_090724

DStv Advert_090724

SBT Tanzania Advert_291123

Friday 6 August 2021

NMB IKIKABIDHI MSAADA DAR KWA SHULE YA WASIOONA

Mkuu wa Wilaya ya Ilala, Mhe. Ng'wilabuzu Ludigija (wa nne kulia) pamoja na Meneja wa NMB Kanda ya Dar es Salaam, Donatus Richard (wa tatu kulia) wakimkabidhi Mwenyekiti wa Jumuiya ya Maendeleo ya Wasioona Tanzania (TAB), Bw. Omar Itambu sehemu ya fimbo 500 za kuongozea wasioona zenye thamani ya shilingi milioni 14 jana jijini Dar es Salaam. Msaada huo umetolewa na Benki ya NMB, wengine wanaoshuhudia ni maofisa waandamizi wa NMB (kulia).
Mwenyekiti wa Jumuiya ya Maendeleo ya Wasioona Tanzania (TAB), Bw. Omar Itambu (mwenye kipaza sauti) akiishukuru Benki ya NMB mara baada ya kupokea sehemu ya fimbo 500 za kuongozea wasioona zenye thamani ya shilingi milioni 14 jana jijini Dar es Salaam. Msaada huo umetolewa na Benki ya NMB, wengine wanaoshuhudia ni maofisa waandamizi wa NMB (kulia).
Mkuu wa Wilaya ya Ilala, Mhe. Ng'wilabuzu Ludigija (mwenye skafu kushoto) akipokea sehemu ya msaada wa viti na meza za walimu toka kwa Meneja wa NMB Kanda ya Dar es Salaam, Donatus Richard (kulia) hafla iliyofanyika Shule ya Sekondari Mchikichini jana jijini Dar es Salaam. Katika hafla hilo NMB ilikabidhi msaada wa Viti 190, meza 60 na Madawati 100 kwa Shule za Sekondari Kipunguni na Mchikichini, pamoja na Shule ya Msingi Kibaga zote za jijini Dar es Salaam.
Mkuu wa Wilaya ya Ilala, Mhe. Ng'wilabuzu Ludigija (mwenye skafu kushoto) akikabidhi sehemu ya fimbo 500 za kuongozea wasioona zenye thamani ya shilingi milioni 14 kwa Mwenyekiti wa Jumuiya ya Maendeleo ya Wasioona Tanzania (TAB), Bw. Omar Itambu na viongozi wa TAB jana jijini Dar es Salaam. Msaada huo umetolewa na Benki ya NMB, wengine wanaoshuhudia ni maofisa waandamizi wa NMB (kulia).

No comments:

Post a Comment