Wateja wataweza kununua mitungi ya gesi katika vituo vyote vya huduma za kujaza mafuta Dodoma, pamoja na mawakala wa uuzaji wa rejareja. Kampuni pia inatarajia kuzindua maduka mawili ya kisasa ya PumaGas ambayo yatatoa huduma za kisasa, yakiwa na huduma mbalimbali ikiwemo kujaza na kubadilisha mitungi ya gesi, kuhakikisha watu hawakwami katika shughuli zao za kila siku.
Kama hiyo haitoshi, kwa kuanza rasmi upatikanaji wa huduma hii mpya jijini Dodoma, wateja watapatiwa ofa mbalimbali pindi wanunuapo mitungi ya gesi ya ujazo tofauti kama vile 6kg, 15kg, na 38kg. Kwa kuongezea, pia kampuni inategemea kuzindua huduma ya uuzaji wa uuzaji wa nishati kwa wingi au ujazo mkubwa kuanzia 200kg mpaka 20,000kg.
No comments:
Post a Comment