Foreign Exchange Rates

DStv Advert_020324

DStv Advert_020324

SBT Tanzania Advert_291123

Tuesday 22 December 2020

BENKI YA NMB YAZIDI KUWANOGESHA WATEJA WAKE MSIMU HUU WA SIKUKUU!

Mkuu wa Biashara ya Kadi wa Benki ya NMB - Philbert Casmir akionyesha baadhi ya zawadi zinazotolewa kwa wateja katika kampeni ya MastaBata Siyo Kikawaida zikiwemo; Friji, TV Simu na vinginevyo.
Baadhi ya wafanyakazi wa Benki ya NMB wakifurahia 'NMB Fri-Yay'.

Benki ya NMB imeendelea kuhakikisha wateja wake wanafurahia na kufaidika na huduma zake ikiwemo kutoa elimu juu ya umuhimu wa matumizi ya mifumo ya kidigitali katika kupata huduma kwa usalama wa fedha zao.

Akifafanua zaidi, Mkuu wa Biashara ya Kadi wa Benki ya NMB - Philbert Casmir amesema kuwa, Benki hiyo imekuja kivingine Msimu huu wa Sikukuu kwa kuhakikisha wateja wake wanafaidika kupitia kampeni zake za 'NMB Fri-Yay' na MastaBata Siyo Kikawaida.

“NMB inatambua kila siku lazima wateja wetu wafanye huduma mbalimbali ikiwemo kupata chakula, kujaza mafuta katika magari yao na kufurahia, na kupitia 'NMB Fri-Yay' kila ijumaa ya mwisho wa mwezi kila anayelipa kupitia kadi zao za NMB Mastercard na Mastercard QR atapata punguzo hadi la asilimia 15, wakinunua bidhaa katika vituo vya mafuta vilivyoainishwa na hiyo ni pamoja na sehemu za vyakula na maeneo ya starehe ambayo tumeingia ubia na wafanyabiashara katika Mikoa ya Dar es Salaam, Arusha, Moshi, Dodoma, Mwanza na Zanzibar. Tunaimani kampeni hizi zitawapeleka wateja katika njia ya kidigitali na kutunza miamala yao ya kibenki."

Amesema hiyo yote ni katika kuwatoa wateja katika mfumo wa matumizi ya fedha taslimu katika kufanya manunuzi na kutumia mfumo wa kadi katika kufanya malipo ya huduma njia ambayo ni rahisi na salama zaidi.

Ameeleza kuwa, katika msimu huu wa sikukuu, wanahakikisha wateja wao wanafurahia sikukuu za mwisho wa mwaka kwa kununua bidhaa na kutembelea sehemu mbalimbali kupitia kampeni ya 'MastaBata sio kikawaida' kampeni iliyoifanya benki hiyo kuendelea kuwa kinara kwa kuwazawadia wateja wao.

"Kupitia kampeni hii tunatoa zawadi kwa wateja wetu pamoja na kutoa elimu ya kuacha matumizi za fedha taslimu njia ambayo ni gharama na si salama na kugeukia matumizi ya kadi katika kufanya huduma." Amesema Philbert.

Ameeleza kuwa kampeni ya 'MastaBata Sio Kikawaida' ni ya muda wa miezi mitatu ikiwa na zawadi za wiki, mwezi na zawadi za mshindi wa jumla. Nayo pia ikiwalenga wanaotumia kadi za NMB Mastacard na Mastacard QR kufanya manunuzi.

"Katika zawadi za wiki, kila wiki kuna washindi 40 wanajishindia laki moja kila mmoja, zawadi za mwezi ni simu ya kisasa aina ya Samsung Galaxy note 20 na zawadi kubwa ya mwisho ya kumalizia kampeni ni kuwapeleka wateja wetu kutembelea vivutio mbalimbali zikiwemo mbuga za wanyama za Serengeti, Ngorongoro na Visiwa vya karafuu visiwani Zanzibar." Amesema.

Aidha amesema kuwa hiyo ni katika kudumisha utalii wa ndani wateja watapata huduma za hadhi ya nyota tano.

"Na tumeiita 'MastaBata Sio Kikawaida' kwa sababu mteja mwingine anaweza asisafiri au tayari ameshatembelea maeneo ya vivutio basi atakuwa na machaguo, gharama ileile ya kusafiri atachagua zawadi nyingine nyingi zikiwemo Televisheni ya kisasa, jokofu, Microwave, Kompyuta mpakato na simu za mkononi na hii yote ni katika kuwazawadia wateja wetu na kujenga uelewa wa umuhimu wa kutumia kadi za NMB Mastercard na Mastercard QR inayopatikana kupitia NMB Mkononi." Amesema.

NMB ina wateja zaidi ya milioni tatu wenye kadi na inawasihi waendelee kuzitumia ili waweze kunufaika na hizi ofa hasa msimu huu wa Sikukuu lakini wajijengee mazoea ya kutotumia pesa taslimu (keshi).

No comments:

Post a Comment