Foreign Exchange Rates

DStv Advert_020324

DStv Advert_020324

SBT Tanzania Advert_291123

Wednesday 29 June 2022

MAKOROKOCHO COMEDY SHOW DANI YA DStv PEKEE


Tunausindikiza mwezi Juni kwa namna ya kipekee, kupitia usiku maalumu unaowaleta pamoja wakali wa vichekesho kutoka Tanzania, Uganda na Nigeria.

Ni marudio ya usiku wa Makarokocho Alhamis hii ambapo kwenye stage watakuwepo, Origino Comedy, Deogratious, Munga pamoja na Mzee Shayo kutoka Watu Baki bila kumsahau Salvador kutoka Uganda na Kevin Pam kutoka Nigeria.

Show nzima kuruka Live kupitia chaneli ya Maisha Magic POA 144, inayopatikana Ndani ya kifurushi cha Poa TShs 9,900/=

Piga *150*53# kulipia kwa urahisi.

VODACOM YAPELEKA HUDUMA ZAKE SABASABA

  • Yatoa punguzo la asilimia 10 kwa wateja wanaolipa kwa huduma ya lipa kwa simu pindi wanunuapo simu janja
Mkuu wa Mauzo Vodacom kanda ya Dar es salaam na Pwani, Brigitta Shirima (katikati) na Mkuu wa Kitengo cha Mauzo na Usambazaji Vodacom Tanzania PLC, George Lugata wakikata utepe kuzindua rasmi banda la kampuni ya Vodacom kwenye maonesho ya 46 ya kimataifa ya biashara sabasaba jijini Dar es salaam, ambapo mwaka huu kutakuwa na ofa na huduma mbalimbali ikiwemo punguzo la asilimia 10 kwa wateja wanaolipa kwa huduma ya lipa kwa simu. Kulia ni mtoa huduma wa kampuni hiyo Sarah Stephen.

Kampuni ya teknolojia na Mawasiliano nchini Vodacom Tanzania Plc, Leo imezindua rasmi banda lake kwenye maonesho ya 46 ya kimataifa ya biashara (sabasaba) jijini Dar es salaam.


Akizungumza kwenye uzinduzi huo, mkuu wa Mauzo wa kanda ya Dar es salaam na Pwani, Brigitta Shirima alisema, "Mwaka huu Vodacom tumekuja kivingine ambapo tunatoa wigo mpana wa huduma mbalimbali kwenye maonesho haya ili kuwapa wateja wetu na watanzania kwa ujumla waweze kufurahia huduma zetu, tuna huduma ya 4G ya kweli na punguzo kubwa la asilimia 10 % kama mteja atanunua simujanja kwa njia ya lipa kwa simu.


Tuna huduma kwa jamii kupitia asasi yetu ya Vodacom Tanzania Foundation ambapo tutatoa taarifa kuhusu huduma yetu ya m-mama inayowagusa kinamama kwa kuwapa usafiri pindi wanapopata dharura wakati wa kujifungua, pia tuna huduma ya E-Fahamu ambayo inatoa elimu kwa wanafunzi kwa njia ya kidijitali bila gharama yeyote.” 


Aliendelea kusema, kampuni hiyo itatoa huduma ya M-Pesa inayowezesha kufanya huduma mbalimbali za fedha kidijitali kwa simu, VodaBima inayowezesha kupata huduma mbalimbali za bima ya magari na afya, pia wateja wetu watapata huduma ya Paisha App inayowezesha kupata mahitaji mbalimbali mtandaoni.

AFRICAN DEVELOPMENT BANK, TANZANIA SIGN $125.2 MILLION LOAN AGREEMENT TO ADDRESS WATER SHORTAGES IN DODOMA REGION

Tanzanian Country Manager, Dr. Patricia Laverley, with the Finance and Planning Minister, Mwigulu Lameck Nchemba.

The African Development Bank and the Tanzanian government have signed a $125.2 million loan agreement for a project that will help address water shortages in three districts in the country’s Dodoma region.

The Dodoma Resilient and Sustainable Water Development and Sanitation Program (Phase I) will benefit more than two million residents in the Bahi, Chemba and Chamwino districts, which have suffered droughts and recorded high population growth.

Tanzania’s Minister of Finance and Planning, Mwigulu Nchemba, and the Bank’s Country Manager, Patricia N. Laverley, signed the loan agreement on 16 May in Dar es Salaam. The Bank had approved the loan on 16 March.

Nchemba said: "This has been a long-awaited project by the people of Dodoma. It is a project that the President, Samia Suluhu Hassan, wishes to see implemented. The signing of this loan agreement will bring great benefits to the people and also provide access to safe water for industrial use.”

The project entails the construction of the 470-meter Farkwa Water Dam, a 128,000 cubic meter-long clean-up, and a water treatment plant with a capacity of 128,000 cubic meters per day. Implementation will span five years.

BENKI YA NBC KUBORESHA MALIPO NA MAKUSANYO YA SERIKALI ZANZAIBAR

Mkurugenzi Mtendaji wa Benki ya NBC, Theobald Sabi (kushoto), na Mkurugenzi wa Wakala wa Serikali Mtandao Zanzibar, Said Seif Said, wakikabidhiana Mikataba ya Maridhiano baada ya Benki ya NBC kuingia makubaliano na taasisi hiyo kwa ajili ya kuweka mfumo wa ukusanyaji wa mapato na malipo ya Serikali ya Zanzibar. Hafla hiyo fupi ya utiaji saini ilifanyika katika Hoteli ya Golden Tulip Zanzibar Airport.
Mkurugenzi Mtendaji wa Benki ya NBC, Theobald Sabi (wa pili Kulia) na Mkurugenzi wa Wakala wa Serikali Mtandao Zanzibar, Said Seif Said (wa pili kushoto) wakionyesha Mikataba ya Maridhiano iliyoigiwa baina ya Benki hiyo na Taasisi ya e-GAZ kwa ajili ya kuweka mfumo wa ukusanyaji wa mapato na malipo ya serikali ya Zanzibar. Wengine katika picha ni Mkurugenzi wa Wateja Wakubwa wa NBC, James Meitaron na Haja Lissa Mkurugenzi wa Usimamizi wa Mifumo na Miundombinu ya TEHAMA Serikali ya Mapinduzi Zanzibar.
Mkurugenzi Mtendaji wa Benki ya NBC, Theobald Sabi (wa pili Kulia) na Mkurugenzi wa Wakala wa Serikali Mtandao Zanzibar, Said Seif Said (wa pili kushoto) wakionyesha Mikataba ya Maridhiano iliyoigiwa baina ya Benki hiyo na Taasisi ya e-GAZ kwa ajili ya kuweka mfumo wa ukusanyaji mapato na malipo ya serikali ya Zanzibar.

Jumanne, Juni 28, 2022 - Benki ya Taifa ya Biashara (NBC) imesaini Mkataba wa Maradhiano na Wakala wa Serikali Mtandao (e-government) Zanzibar, kwa ajili ya kuweka mfumo wa ukusanyaji mapato na malipo ya serikali ya Zanzibar. 

Akizungumza wakati wa hafla ya utiaji saini mkataba huo jijini Zanzibar, Mkurugenzi Mtendaji wa Benki ya NBC, Theobald Sabi alisema; “Benki ya NBC inaendelea kuwekeza katika mifumo ya TEHAMA ili kutoa masuluhisho ya kibenki kwa makundi yote ya wateja. Leo tunajivunia kuunga mkono juhudi za Serikali ya Zanzibar chini ya ya Rais Hussein Mwinyi, katika kuiboresha sekta ya fedha kwa kuingiza mifumo ya kidigitali ili kuongeza ufanisi hususan katika kuboresha makusanyo ya mapato ya serikali na malipo kwa wadau wake” alisema. 

Ushirikiano huu utaiwezesha serikali ya Zanzibar kukusanya mapato kwa wakati na kwa kuwapa wateja urahisi wa kufanya malipo ya Serikali kwa urahisi katika matawi ya Benki ya NBC, Mawakala, au kupitia huduma kwa njia ya mtandao kupitia simu za mkononi na kwa njia ya mtandao wa intaneti. 

Akizungumza wakati wa hafla hiyo, Mkurugenzi Mkuu wa e-GAZ, Said Seif, alisema, “Tunafuraha kushirikiana na Benki ya NBC, moja ya Benki kubwa nchini Tanzania, katika kuweka mfumo wa kidigitali wa makusanyo na malipo ya Serikali hapa Zanzibar. Kama wakala uliopewa dhamana ya uwekaji mifumo ya digitali Zanzibar, tuna dhamira ya kuhakikisha kuwa tunashirikiana na wadau wote wenye uwezo katika kufikia kiwango cha juu kidijitali katika taasisi za umma hapa Zanzibar” alisema.

SELCOM NA NALA WANAUNGANA KURAHISHA NA KULETA UNAFUU MIAMALA YA PESA TANZANIA

Sameer Hirji, Mkurugenzi Mtendaji wa Selcom (kushoto), akiwa na Benjamin Fernandes, Mwanzilishi na Mkurugenzi Mtendaji wa NALA (kulia), wakitia saini mkataba wa ushirikiano kati ya kampuni hizo mbili katika kutoa huduma za kutuma fedha nchi za nje kwenda Tanzania.
Sameer Hirji, Mkurugenzi Mtendaji wa Selcom (kushoto), akizungumza na waandishi wa habari kwenye tukio hilo. Kulia ni Benjamin Fernandes, Mwanzilishi na Mkurugenzi Mtendaji wa NALA.
Benjamin Fernandes, Mwanzilishi na Mkurugenzi Mtendaji wa NALA akiwaonyesha waandishi wa habari jinsi ya kutuma pesa kutoka Tanzania kwenda nje ya Marekani na Uingereza wakati wa uzinduzi wa ushirikiano mpya kati ya Selcom na NALA jijini Dar es Salaam tarehe 28 Juni 2022. Kushoto ni Mkurugenzi Mkuu Sameer Hirji wa Selcom.

Dar Es Salaam, 28 Juni 2022: Selcom na NALA wameingia makubaliano ya kushirikiana na kuongeza nguvu ya kutuma fedha kutoka nchi za nje (Uingereza na Marekani) moja kwa moja kwenda kwenye mitandao yote ya simu za mkononi na akaunti za kibenki nchini Tanzania.

Selcom ambao ni watoaji huduma wakubwa wa malipo nchini Tanzania, wametangaza ushirikiano huo wa kimkakati na NALA, kampuni ya kivumbuzi ya yenye makao yake makuu nchini Uingereza, utakaowezesha kuchochea miamala ya moja kwa moja kutoka nchi hizo mbili wakati wowote.

Ushirikiano na Selcom unasaidia kuiweka NALA katika mstari wa mbele katika kasi ya mapinduzi ya utumaji pesa ndani na nje ya nchi. Kasi hii ya mapinduzi inapewa nguvu kutokana na kazi nzuri inayofanywa na Selcom katika ikolojia wa huduma za kifedha kama njia muhimu na uwezo wa NALA katika uvumbuzi bora wa bidhaa na huduma.

Kwa ushirikiano huu, watumiaji wa NALA nchini Uingereza na Marekani sasa wanaweza kuhamisha fedha kwenda benki kadhaa na kufanya miamala ya simu za mkononi nchini Tanzania kwa urahisi popote walipo. Hii pia itawapa watanzania waishio ughaibuni fursa ya kutuma mitaji nchini.

TIGO TANZANIA YAPATA MAGARI KUTOKA ISUZU TANZANIA


Tarehe 28 Juni 2022 - Specialized Rentals Limited (SRL) ni mtoa huduma bora anayechipukia katika nafasi ya ukodishaji wa uendeshaji wa vifaa vya moto nchini Tanzania, ikitoa magari bora zaidi na yenye kiwango tofauti cha magari yaliyozoeleka kwa mteja na vifaa hivi vya moto vina matumizi ya muda mfupi hadi muda mrefu na yanaendana na kasi kubwa zaidi inayomfaa na kumpa urahisi mtumiaji.

Hivi karibuni Specialized Rentals Limited imepewa Oda ya Ugavi wa Pickups 45 Mpya kabisa za ISUZU D-MAX kwa kampuni ya TIGO Tanzania (MIC TPLC), ambayo imeendeleza falsafa yake ya kutoa huduma bora kwa mteja.


Akizungumza katika hafla ya makabidhiano ya vifaa hivyo kwenye Ukumbi wa Maonyesho ya Al Mansour, Meneja Mkuu wa Kampuni ya Specialized Rentals Limited, Bw. Mihir Patwardhan alisema “Tunajisikia furaha kubwa kuchaguliwa na Tigo Tanzania kwa utaratibu huu adhimu. Shukrani zetu za dhati kwa Bw. Anurup Chatterjee na timu yake kwa kuweka imani tena katika huduma zetu bora tunazozitoa. Tuna uhakika wa kutumia uzoefu wetu tulionao ili kuhakikisha ufanisi unapatikana na unakuza biashara zetu na shughuli zetu zinazofanyika kwenye makampuni yetu zikidhi matakwa ya wateja wetu".


Bw. Patwardhan aliendelea na kuongeza, “Tunaishukuru Serikali ya Tanzania, kwa kuweka mkazo katika kujenga miundombinu ya barabara zenye viwango vya kimataifa nchini kote, hivyo kuwezesha na kuvutia uwekezaji nchini na miundombinu hii bora imekuwa kichocheo kinachohitajika kwa wawekezaji wa ndani na wa nje ya Nchi.

Kaimu Mkurugenzi Mkuu wa Tigo Tanzania Bw. Innocent Rwetabura alisema “Ushirikiano wetu wa kimkakati na Specialized Rentals Limited ambao wanaungwa mkono ipasavyo na kampuni maarufu ya Al Mansour (Isuzu) Tanzania unaonyesha dhamira yetu ya kuipa kampuni yetu ya Tigo Tanzania inayotoa huduma zake Tanzania nzima magari yenye uhakika na ufanisi zaidi ili kukuza jitihada za kuwafikia na kuwapatia wateja wetu wote bidhaa na huduma bora kote nchini”.



Bw. Anurup Chatterjee, Meneja Mkuu wa Kampuni ya Al Mansour – Isuzu alisema “Al Mansour kama mfanyabiashara aliyeidhinishwa wa ISUZU amewekeza dola milioni 1.5 katika soko la Tanzania tangu kuanzishwa kwake na uwekezaji huu pia unaonyesha imani ya ISUZU katika sekta ya vifaa vya moto hususani magari na soko lake limekuwa imara katika uchumi wa kikanda katika muongo huu na ujao”.

Monday 27 June 2022

JIUNGE NA UENDELEE KUBURUDIKA NA DStv


Ya Walimwengu - Ni Balaa baada ya kufumaniwa Wanawake wote wawili waamua kuhamia kwa mama mkwe 😂😂, mbona mazito...

Unakosaje sasa ni Jumatano hii ndani ya Maisha Magic Poa 144 muda ni ule ule saa 3:30 usiku.

Piga *150*53# kulipia kwa urahisi kifurushi cha Poa TShs 9,900/= tu ili usikose burudani hii ndani ya @dstvtanzania pekee.

#DStvEwaaaaaah

BENKI YA NBC YAFUNGUA MILANGO ZAIDI KWA WAFANYABIASHARA WA TANZANIA NA AFRIKA KUSINI

Mkurugenzi Mtendaji wa Benki ya NBC, Bw. Theobald Sabi akizungumza na wajumbe wa Jukwaa la Wafanyabiashara wa Afrika Kusini na Tanzania wakati wa Mkutano wa Jukwaa hilo uliofanyika jijini Dar es Salaam hivi karibuni.
Mwenyekiti wa Jukwaa la Wafanyabiashara wa Afrika Kusini, Bw. Manish Thakrar (katikati) akizungumza na wajumbe wa jukwaa hilo wakati wa Mkutano wa Jukwaa hilo uliofanyika jijini Dar es Salaam hivi karibuni .
Mkurugenzi Mtendaji wa Benki ya NBC, Bw. Theobald Sabi (kushoto) akibadilishana mawazo na Mwenyekiti wa Jukwaa la Wafanyabiashara wa Afrika Kusini, Bw. Manish Thakrar wakati wa Mkutano wa Jukwaa hilo uliofanyika jijini Dar es Salaam hivi karibuni.
Wajumbe wa Jukwaa la Wafanyabiashara wa Afrika Kusini na Tanzania wakifuatilia Mkutano wa Jukwaa hilo uliofanyika jijini Dar es Salaam hivi karibuni.

Benki ya Taifa ya Biashara (NBC) imesisitiza kuhusu utayari wake katika kufanikisha ustawi wa biashara baina ya Tanzania na Afrika kusini kupitia huduma zake hususani kwa katika uwekezaji wa biashara na kilimo.

Msimamo huo wa benki hiyo umetolewa na Mkurugenzi Mtendaji wa Benki hiyo Bw. Theobald Sabi wakati akizungumza kwenye Mkutano wa Jukwaa la Wafanyabiashara wa Afrika Kusini uliofanyika jijini Dar es Salaam hivi karibuni .

Bw. Sabi alisema kwa muda mrefu sasa benki hiyo imekuwa mdau mkubwa wa wafanyabiashara kati ya Afrika Kusini na Tanzania ambapo kupitia mkutano huo aliweza kuelezea huduma mbalimbali zinazotolewa na benki hiyo kwa wafanyabiashara hao ikiwemo huduma za huduma za mikopo ya biashara na kilimo.

“Jukumu letu kama benki kubwa hapa nchini ni kuhakikisha tunatoa masuluhisho ya kibiashara kwa wafanyabiashara wetu ili waweze kufanya shughuli zao kiushindani ndani na nje ya nchi. Tumekuwa tukitoa huduma mbalimbali kwao ikiwemo mikopo ya aina mbalimbali ikiweo ya biashara na kilimo, bima kupitia benki sambmba na kuhusumia mnyororo wote wa biashara ikiwemo kuhifadhi fedha, kutuma na kupokea fedha kutoka ndani nan je ya nchini,’’ alisema.

Friday 24 June 2022

THE GEITA GOLD MINE KILIMANJARO CHALLENGE AGAINST HIV/AIDS, TO KICK OFF ON 15TH OF JULY 2022

Some of the cyclists who will be participating in the GGML Kili Challenge campaign by climbing Mount Kilimanjaro with the aim of raising funds to fund the eradication of HIV and AIDS.

The Geita Gold Mine Limited (GGML) - Kilimanjaro HIV/AIDS Challenge against HIV/AIDS, will kick off on 15th of July 2022 at Machame Gate and arriving back at Mweka Gate on 21st of July 2022.

On his statement to media, The Manager for Kilimanjaro Challenge Against HIV and AIDs Trust, Manace Ndoroma, said the Challenge has grown from humble beginnings since its inception in 2002 to a multinational event, hosting over 500 climbers from 6 continents and over 20 countries, which has raised more that 2 million dollars to date.

“You too can play your part by joining our team of climbers and cyclers in 2022 helping us raise funds for this truly noble event. Please take time to think of how a small gesture on your part could be life-changing for someone else.

He added, “the impact of HIV/AIDS on the population of Tanzania is devastating as many frail elders have to take over the care of young children after the death of their parents as a result of this disease. Many of these families do not have the financial means to support these children, and many are left without food, water or medical care.”

NMB BANK REACHES AGREEMENT WITH ZANZIBAR GOVERNMENT TO MAINTAIN FORODHANI GARDEN

Mkuu wa Biashara ya kadi NMB, Philbert Casmir akiongea kwenye mkutano huo kwenye hoteli ya Serena Inn mjini Zanzibar.

Mkuu wa wilaya ya Mjini Unguja, Rashid Simai Msaraka (katikati waliokaa) katika picha ya pamoja na maofisa wa Benki ya NMB baada ya mazungumzo na waandishi wa habari kwenye ukumbi wa Hoteli ya Serena Inn mjini Zanzibar.

NMB Bank has reached an agreement with Zanzibar Government to maintain Forodhani garden in Zanzibar as part of its efforts to support the island’s environmental conservation drive and blue economy agenda.

The Forodhani garden maintenance project seeks to enhance tourists experience and better reflect the area’s renowned reputation, and will enable the garden to woo more visitors annually while contributing to revitalization of the tourism industry.

Speaking to journalists in Zanzibar on Thursday on the sidelines of the upcoming Zanzibar Boat Race sponsored by NMB Bank scheduled to take place this Saturday, the Zanzibar Urban District Commissioner, Rashid Simai Msaraka said NMB Bank has been a good development partner to the Zanzibar government adding that the bank has been instrumental in supporting various development initiatives in the Isles.

He noted that the Sixth Phase Government under President Samia Suluhu Hassan and President Hussein Mwinyi has always prioritized working closely with the private sector and urged more companies to support government’s development initiatives.

VODACOM YASHIRIKI MKUTANO MKUU WA MWAKA WA ISACA

Mkurugenzi wa IT wa Vodacom Tanzania Plc, Athuman Mlinga (katikati), akizungumza kwenye mdahalo na kuwasilisha mada kuhusu Utawala na Uhakika wa TEHAMA. Vodacom Tanzania imeshiriki katika mkutano wa mwaka wa ISACA Tanzania jijini Arusha, ambapo wataalam wa masuala ya usalama wa mtandao na teknolojia walikutana kujadili namna ambavyo kila mmoja anaweza kushiriki katika kuimarisha usalama wa mifumo yake. Wengine kushoto ni Mkaguzi mkuu wa hesabu za ndani TASAC, Ahadi Chacha na Mshauri wa IT KPMG, James Chotamawe
Mkuu wa Idara ya Usalama wa Mtandao wa Vodacom Tanzania Plc, Joel Kazoba akizungumza kwenye mkutano wa mwaka wa ISACA Tanzania uliowakutanisha jumuiya ya usalama wa mtandao na teknolojia na kujadili umuhimu wa ulinzi wa data, Kazoba alisisitiza kuwa Vodacom inaendeleza teknolojia salama inayowezesha wateja pamoja na kuwaunganisha kwenye maisha bora ya baadaye.




NMB YAZINDUA KIFURUSHI MAALUM KWA AJILI YA WALIMU

Afisa Mkuu Wateja Binafsi na Biashara Benki ya NMB, Filbert Mponzi (watatu kushoto) akimpa maelezo Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. Jenista Mhagama mara baada ya kuzindua Mpango maalum 'Mwalimu Spesho' uliyozinduliwa Jijini Dodoma hivi karibuni. Wapili kushoto ni Mkuu wa Idara ya Wateja Binafsi, Aikansia Muro na Meneja Kanda ya Kati Nsolo Mlozi.

Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais Utumishi na Utawala Bora, Mhe. Jenista Mhagama ametoa Rai kwa benki ya NMB kuhakikisha inawafikia watumishi wengi zaidi wakiwemo walimu ili kuwasaidia kujiendeleza kimaisha.

Kauli hiyo aliitoa jana wakati akizungumza na walimu wa Shule za Msingi na Sekondari wa kanda ya Kati Jijini Dodoma katika siku ya Mwalimu iliyoandaliwa na benki ya NMB ikienda sambasamba na uzinduzi wa Mpango wao Maalum wa "Mwalimu Spesho." 

Afisa Mkuu Wateja Binafsi na Biashara Benki ya NMB, Filbert Mponzi (kushoto) akishirikiana na Waziri wa nchi Ofisi ya Rais Utumishi wa Umma na utawala Bora, Mhe. Jenista Mhagama kutoa kitambaa ikiwa ni ishara ya kuzindua Mpango maalum wa ‘Mwalimu Spesho’ iliyozinduliwa hivi karibuni Jijini Dodoma.

Mpango huo ni kwa ajili ya walimu kupata mikopo na huduma mbalimbali zinazotolewa na benki hiyo nchini huku walimu wakipongeza huduma hizo.

Waziri alisema mpango huo mzuri usiishie kwa walimu 5,000 badala yake angetamani uwafikie walimu wengi na watumishi ili kuwajengea uwezo hasa walimu ambao ndiyo chanzo cha kuwaandaa viongozi, wataalamu wa baadae.

Alitaka NMB kusimama na walimu wakati wote ili kuwajengea uwezo akieleza kuwa jumla ya walimu 6800 wamepandishwa madaraja hivyo ni fursa kwao kuingia kwenye mikopo kwa benki ambayo inajulikana na uendeshaji wake mzuri kuliko kukopa kwenye taasisi ambazo zinawaumiza.


Afisa Mkuu wa Wateja Binafsi na Biashara, Filbert Mponzi alisema walikusanya walimu viongozi 350 kwa ajili ya kubadilishana mawazo kuboresha zaidi huduma za kibenki na kujadiliana kuhusu fursa zilizopo kwa ajili ya kundi la Walimu nchini.

“Tunaamini, walimu hawa zaidi ya 350, watasaidia kupeleka elimu watakayoipata hapa kwa wenzao na hata familia zao na jamii kwa ujumla juu ya huduma nzuri zinazotolewa na benki ya NMB, lengo ni kumfanya mwalimu kuwa na maisha mazuri wakati wote,” alisema Mponzi.

FURAHIA MSIMU MPYA WA KIPINDI CHA MASKANI POA


Furahia msimu mpya wa kipindi cha Maskani Poa ambacho kwa sasa kitaongozwa na @officialshilole pamoja na @officialbabalevo kitakachoruka kila siku za Ijumaa saa 3 usiku ndani ya Maisha Magic Poa 144 kupitia kifurushi cha Poa kwa TShs. 9,900/= tu kupitia @dstvtanzania pekee.

Piga *150*53# kulipia kifurushi chako mapema!

#UsichukuliePoaVituVyaPoa

#DStvEwaaaaah

BENKI YA LETSHEGO YAZINDUA RASMI AINA MBILI ZA MIKOPO

Mkurugenzi Mtendaji wa Benki ya Letshego Tanzania - Omar Msangi (katikati) akizungumza katika mkutano na wanahabari uliyofanyika makao makuu ya benki hiyo. Kulia ni Leah Phill - Meneja Mikopo ya Biashara na Denis Simon - Meneja wa Mikopo ya Watumishi wa Umma (kushoto).

Dar es Salaam Tanzania, June 21, 2022 – Benki ya Letshego Tanzania wamezindua rasmi aina mbili za Mikopo ambayo ni MKOPO FASTA wa Biashara na Mikopo ya Watumishi wa Umma katika mkutano na wanahabari uliyofanyika makao makuu ya benki hiyo.

Akizungumza katika uzinduzi huo mbele ya wanahabari Mkurugenzi Mtendaji wa Benki ya Letshego Tanzania Ndugu Omar Msangi alisema “Mikopo hiyo ambayo ni hitaji kubwa kwa wafanyabiashara na Watumishi wa Umma wa Tanzania ni Mikopo rafiki inatolewa muda mfupi ili kuwawezesha wafanyabiashara na watumishi wa umma kutatua changamoto na kufanya maboresho ya shughuli zao kwa kadri ya mahitaji yao”.



Akizungumzia juu ya Manufaa ya Mikopo hiyo Ndugu Omar Msangi alisema “itawaongezea wateja tija na uwezo wa kuboresha biashara na maisha yao na pia kutatua changamoto zao pasipo kuwa na wasiwasi wa kutokuwa na fedha za kutosha katika Biashara na shughuli zao za Kimaendeleo”. Pia aliongeze kwa kusema “MKOPO FASTA wa biashara utatolewa ndani ya saa 72 baada ya mteja kukamilisha fomu yake ya maombi wakati Mikopo ya wafanyakazi itatolewa ndani ya saa 48 baada ya mteja kukamilisha fomu yake ya maombi hivyo kumuwezesha mteja kutimiza malengo yake kwa wakati”.

MKOPO FASTA ni maalum kwa ajili ya wafanyabiashara wadogo, wa kati na wakubwa, ambapo, ndani ya masaa 72, mfanyabiashara atapata mkopo wa hadi shilingi milioni 50, huku muda wa kurudisha mkopo ukifika hadi miezi 12.



Kwa upande mwingine, Mikopo ya watumishi wa umma inatolewa ndani ya saa 48 ambapo mwajiriwa wa serikali au taasisi ya umma anaweza kukopa hadi shilingi milioni 60 atakazozirejesha taratibu kwa hadi miezi 84.

Bi. Leah Phili, Meneja wa Mikopo ya biashara alisema “Mkopo Fasta kwa wafanyabiashara utawasaidia wafanyabiashara kuimarisha na kuboresha biashara zao. Ili tuweze kuboresha maisha kama dhima yetu inavyosema, tumejipanga kuhahikisha wateja wetu wanapata hela ndani saa 72 baada ya kukamilisha nyaraka muhimu za maombi ya MKOPO FASTA. Tunawakaribisha wafanyabiashara wote kutembelea matawi yetu au kutupigia simu kwa maelezo zaidi kuhusu huduma hii na pia kufanya maombi ya MKOPO FASTA.



Pia, Ndugu Denis Simon; Meneja wa Mikopo ya watumishi wa Umma alisema mikopo ya watumishi wa Umma inatolewa ndani ya Masaa 48 baada ya mteja kukamilisha tararibu zote za maombi ikiwepo kujaza fomu ya maombi na kuirudisha kwa afisa wa benki au tawi lolote lililo karibu nae.

Thursday 23 June 2022

NMB YASAIDIA UKUSANYAJI WA TRILIONI 8.6 ZA SERIKALI

Afisa Mtendaji Mkuu wa NMB, Ruth Zaipuna akimkabidithi Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam, Mhe. Amos Makalla nakala ya ripoti ya NMB ya mwaka 2021.

Benki ya NMB kupitia mifumo yake mbali mbali ya malipo imesaidia Serikali kukusanya trilioni 8.6 kupitia mfumo wa Kielektroniki wa Malipo ya Serikali (GePG) kwa miaka mitatu kuanzia mwaka 2019 hadi 2021.

Hayo yalisemwa na Afisa Mtendaji Mkuu wa Benki ya NMB Ruth Zaipuna wakati wa warsha iliyoandaliwa na benki hiyo kwa watendaji mbalimbali wa Mkoa wa Dar es Salaam na kuhudhuriwa na Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam Mhe. Amos Makalla, Wakuu wa Wilaya, madiwani, watendaji na waweka hazina.


Zaipuna alisema benki yake imeendelea kuwekeza kwenye teknolojia jambo ambalo limesaidia kusogeza huduma za kifedha karibu na wananchi huku akisisitiza kuwa benki yake imejizatiti kuendelea kutoa bidhaa zinazokidhi mahitaj ya wateja wake.

“Ubunifu ni kitu pekee ambacho kimetusaidia kupiga hatua na ule uwekezaji ambao tuliufanya kwenye teknolojia ulituwezesha kuwa benki ya kwanza kuunga mifumo yetu na Mfumo wa Kielektroniki wa Malipo ya Serikali (GePG) na hadi sasa zaidi ya taasisi 1,100 tayari zimeunga mifumo yake kwenye mifumo ya NMB ya ukusanyaji wa mapato,” alisema.


Zaipuna alisema ukusanyaji wa mapato kupitia mfumo wa kielektroniki umekuwa ukongezeka kutoka 2.1 trilion mwaka 2019 hadi 3.7 trilioni mwaka jana.

“Fedha hizi zilikusanywa kupitia mifumo yetu ya NMB mkononi, NMB Wakala, Lipa Namba, intaneti nk. Tunaendelea kuwekeza kuhakikisha kuwa mtandao wetu upo vizuri na kuhakikisha usalama wa malipo,” Alisema.

Aidha, Zaipuna alisema benki yake imekuwa mstari wa mbele katika kuchangia maendeleo ya jamii nchini kote nakuongeza kuwa benki yake kwa makusudi ilizindua taasisi yake ya NMB Foundation ilikuchangia maendeleo endelevu.

Alisema Benki yake kwa makusudi iliamua kutenga asilimia moja ya faida yake kila mwaka kuchangia maendeleo nchini kote kwenye sekta za elimu, afya, kilimo, mazingira, uwezeshaji na matukio ya dharura.

Zaipuna alisema benki yake itaendelea kushirikana na wadau mbali mbali wa maendeleo ikiwemo serikali ilikuleta maendeleo chanya na endelevu.

Tuesday 21 June 2022

FURAHIA MSIMU MPYA WA KIPINDI CHA MASKANI POA



Usichukulie Poa Vitu vya Poa ndani ya @dstvtanzania pekee!

Furahia msimu mpya wa kipindi bora namba moja kwa vijana Maskani Poa kinacholetwa kwako na baba Levo na Shilole kila Ijumaa saa 3:00 usiku ndani ya Maisha Magic Poa, 144 kwa TShs 9,900 tu.

Piga *150*53# kulipia kifurushi chako mapema usipitwe na burudani hii.

#DStvEwaaaah

Monday 20 June 2022

BUSINESS PICTORIAL

Ministry of Foreign Affairs and East African Cooperation Permanent Secretary, Ambassador Joseph Sokoine (right) exchanges a Memorandum of Understanding with the CRDB Bank Managing Director, Abdulmajid Nsekela, for the bank to develop a Diaspora Digital Hub for Tanzanian's living abroad, to enable them access various services they may need from Tanzania. The system will include Government service providers such as NIDA, Immigration, TIC and other service providers whose services are needed by the Diaspora. 

Tanzania Association of Microfinance Institute (TAMFI) Executive Director, Winnie Terry (right), Tanzania Institute of Bankers (TIOB) Executive Director, Patrick Mususa (left) and Tanzania Bankers Association (TBA) Executive Director, Tusekelege Mwaikasu (centre) in a souvenir photo shortly after TAMFI and TIOB signed a Memorandum of Understanding (MOU) for partnership in Dar es Salaam recently.
The Tanzania Commercial Bank PLC (TCB) Board Chairman, Dr. Edmund Mndolwa briefs journalists during the 30th Annual General Meeting of the bank over the weekend. Second right is Chief Executive Officer of TCB, Sabasaba Moshingi.

TANZANIA COMMERCIAL BANK YAPATA FAIDA YA BILIONI 19.7

 
Mwenyekiti wa bodi ya Tanzania Commercial Bank Dkt. Edmund Mndolwa (katikati), akizungumza na wanahabari wakati akitangaza kupata faida ya shilingi bilioni 19.7 kwa mwaka ulioishia 31 Desemba 2021 hatua inayo tajwa kuwa ya mafanikio na kuimarika kwa benki hiyo ambayo ni muunganiko wa iliyokuwa Benki ya TPB na TIB Corporate Bank.

Afisa Mtendaji Mkuu wa Tanzania Commercial Bank, Sabasaba Moshingi akizungumza wakati wa hafla ya kutangaza faida ya shilingi bilioni 19.7 kwa mwaka ulioishia 31 Desemba 2021.

 Mwenyekiti wa bodi ya Tanzania Commercial Bank Dkt. Edmund Mndolwa (katikati), akizungumza na wanahabari wakati akitangaza kupata faida ya shilingi bilioni 19.7 iliyopata benki hiyo. Wa pilikulia ni Afisa Mtendaji Mkuu wa Tanzania Commercial Bank, Sabasaba Moshingi pamoja na maafisa wengine wa benki hiyo.

Tanzania Commercial Bank (TCB) imetangaza kupata faida ya shilingi Bilioni 19.7 kwa mwaka ulioishia 31 Desemba 2021 hatua inayotajwa kuwa ya mafanikio na kuimarika kwa benki hiyo ambayo ni muunganiko wa iliyokuwa Benki ya TPB na TIB Corporate Bank.

Mwenyekiti wabodi ya Tanzania Commercial Bank Dkt. Edmund Mndolwa ametoa taarifa hiyo katika mkutano wa mwaka wa wanahisa wa benki hiyo uliofanyika jijini Dar esSalaam na kusema kuwa faida hiyo ni kabla ya kodi.

Faida iliyopatikana mwaka 2021 inatajwa na uongozi wa benki kuwa ni kubwa kufuatia ile ya mwaka 2020 ambayo haijawahi kufikiwa tangu kuanzishwa kwa Benki ya TCB takriban miaka 95 iliyopita.

Amepongeza uongozi pamoja na wafanyakazi wa Tanzania Commercial Bank kwa kuchangia mafanikio hayo licha ya changamoto za mdororo wa uchumi uliosababishwa na wimbi la ugonjwa wa UVOKO-19 ambao pia umeathiri uchumi wa mataifa mengi duniani.

Friday 17 June 2022

MASTERCARD AND ECOBANK GROUP PARTNER TO DIGITIZE AGRICULTURAL VALUE CHAINS IN AFRICA AND EMPOWER MILLIONS OF SMALLHOLDER FARMERS THROUGH DIGITAL AND FINANCIAL INCLUSION

Paul-Harry Aithnard, Regional Executive Director of UEMOA Ecobank (left), Solomon Quaynor, Vice President for Private Sector, Infrastructure and Industrialisation, African Development Bank Group (centre) and Michael Froman, Vice Chairman and President, Strategic Growth for MasterCard (right)
  • Mastercard and Ecobank Group will deploy Mastercard Farm Pass, an award-winning, innovative solution that helps connect smallholder farmers to financial and agricultural ecosystems
  • Mastercard Farm Pass will be rolled out leveraging the 33 countries where Ecobank has banking operations, helping millions of smallholder farmers gain digital access to markets, quality inputs, financial services, and real-time pricing information
Abidjan, Cote d’Ivoire – 14 June 2022: Mastercard and Ecobank Group have partnered to connect millions of smallholder farmers in Sub-Saharan Africa to Mastercard’s Farm Pass – a digital platform that makes it safer and easier for farmers to sell their produce at a fair price.

Under the partnership, Ecobank will extend the reach and impact of the Mastercard Farm Pass platform leveraging its Pan-African network of 33 countries. Many smallholder farmers in Sub-Saharan Africa face several challenges. These include limited access to markets, working capital to finance activities or secure quality inputs, and relevant financial tools to pay and get paid efficiently. This has led to insecurity, inefficiencies, and a waste of resources and food, preventing farmers from running sustainable businesses.

Farm Pass brings together various agri-sector stakeholders from the supply and demand sides, in one agricultural marketplace, amplifying the collective positive impact on farming communities. Smallholder farmers can sell their produce at a better price, access quality inputs and farming information, get paid and pay digitally and develop a financial profile that can unlock financing opportunities for working capital and inputs.