Foreign Exchange Rates

DStv Advert_020324

DStv Advert_020324

SBT Tanzania Advert_291123

Monday 8 August 2022

UJERUMANI YAIPATIA TANZANIA MSAADA WA SH. BILIONI 23.7

Katibu Mkuu Wizara ya Fedha na Mipango, Bw. Emmanuel Tutuba (kulia) na Balozi Ujerumani nchini Tanzania Mhe. Regine Hess, wakisaini mkataba wa msaada wenye thamani ya Euro milioni 10 sawa na shilingi bilioni 23.7 kwa ajili ya utekelezaji wa Mradi wa kukabiliana na migongano kati ya wanyamapori na binadamu, Mradi wa kuwezesha upatikanaji wa haki za wanawake na watoto na Mradi wa kuandaa maandiko ya kitaalamu ya miradi, jijini Dar es Salaam.
Katibu Mkuu wa Wizara ya Fedha na Mipango, Bw. Emmanuel Tutuba (kulia) na Balozi Ujerumani nchini Tanzania Mhe. Regine Hess, wakibadilishana hati ya mkataba wa msaada wenye thamani ya Euro milioni 10 sawa na shilingi bilioni 23.7 kwa ajili ya utekelezaji wa Mradi wa kukabiliana na migongano kati ya wanyamapori na binadamu, Mradi wa kuwezesha upatikanaji wa haki za wanawake na watoto na Mradi wa kuandaa maandiko ya kitaalamu ya miradi, jijini Dar es Salaam.

Serikali ya Tanzania na Serikali ya Shirikisho la Jamhuri ya Ujerumani zimetiliana saini mkataba wa msaada wenye thamani ya Euro milioni 10 sawa na shilingi bilioni 23.7 kwa ajili ya utekelezaji wa Mradi wa kukabiliana na migongano kati ya wanyamapori na binadamu, Mradi wa kuwezesha upatikanaji wa haki za wanawake na watoto na Mradi wa kuandaa maandiko ya kitaalamu ya miradi.

Mkataba huo umesainiwa jijini Dar es Salaam, kati ya Katibu Mkuu wa Wizara ya Fedha na Mipango Bw. Emmanuel Tutuba kwa niaba ya Serikali ya Tanzania na Balozi wa Ujerumani nchini Tanzania Mhe. Regine Hess kwa niaba ya Serikali ya Shirikisho la Jamhuri ya Ujerumani.
Katibu Mkuu wa Wizara ya Fedha na Mipango, Bw. Emmanuel Tutuba (kulia) na Balozi Ujerumani nchini Tanzania Mhe. Regine Hess wakionesha hati ya mkataba wa msaada wenye thamani ya Euro milioni 10 sawa na shilingi bilioni 23.7 kwa ajili ya utekelezaji wa Mradi wa kukabiliana na migongano kati ya wanyamapori na binadamu, Mradi wa kuwezesha upatikanaji wa haki za wanawake na watoto na Mradi wa kuandaa maandiko ya kitaalamu ya miradi, jijini Dar es Salaam.

Akizungumza katika hafla hiyo, Bw. Tutuba alisema kuwa Mradi wa kukabiliana na migongano kati ya wanyamapori na binadamu umetengewa kiasi cha Euro milioni 6 ambacho kitatumika kupunguza vifo vinavyosababishwa na wanyamapori kwa jamii zinazozunguka baadhi ya hifadhi za wanyamapori na kuepusha uharibifu wa bayoanuai katika hifadhi za wanyamapori.


Katibu Mkuu wa Wizara ya Fedha na Mipango, Bw. Emmanuel Tutuba na Balozi Ujerumani nchini Tanzania Mhe. Regine Hess wakipongezana baada ya kusaini mkataba wa msaada wenye thamani ya Euro milioni 10 sawa na shilingi bilioni 23.7, jijini Dar es Salaam. Kulia ni Naibu Katibu Mkuu wa Wizara ya Maliasili na Utalii Bw. Juma Selemani Mkomi, na Naibu Katibu Mkuu Wizara ya Katiba na Sheria Dkt. Khatibu Kazungu wa na kushoto ni Mkuu wa Ushirikiano wa Ujerumani na Tanzania Dkt. Katrin Bornemann.

Bw. Tutuba aliongeza kuwa Mradi wa kuwezesha upatikanaji wa haki za wanawake na watoto utatekelezwa kwa kiasi cha kwa Euro milioni 3 ambacho kitachangia kuboresha upatikanaji wa haki za wanawake na watoto.

“Utekelezaji wa mradi huu utasaidia kuondoa ubaguzi wa kijinsia na unyanyasaji kwa wanawake na watoto na kuongeza usawa wa kijinsia nchini”, alisema Bw. Tutuba.
Katibu Mkuu wa Wizara ya Fedha na Mipango, Bw. Emmanuel Tutuba, akizungumza wakati wa halfa ya utiaji saini mkataba wa msaada wenye thamani ya Euro milioni 10 sawa na shilingi bilioni 23.7 kwa ajili ya utekelezaji wa Mradi wa kukabiliana na migongano kati ya wanyamapori na binadamu, Mradi wa kuwezesha upatikanaji wa haki za wanawake na watoto na Mradi wa kuandaa maandiko ya kitaalamu ya miradi, jijini Dar es Salaam.

Aidha alisema kuwa, Mradi wa tatu ni kwa ajili ya kuandaa maandiko ya kitaalamu ya miradi, ambapo kiasi cha Euro milioni 1, zitatumika kufanya pembuzi yakinifu za miradi inayotekelezwa kwa fedha za misaada kutoka Serikali ya Shirikisho la Jamhuri ya Ujerumani.

“Msaada huu ni sehemu ya ahadi ya misaada ya jumla ya Euro milioni 71 sawa na shilingi bilioni 188.65 iliyotolewa na Shirikisho hilo, katika majadiliano yaliyofanyika baina ya pande hizi mbili, jijini Dar es Salaam tarehe 25 Novemba 2021 kwa ajili ya utekelezaji wa miradi mbalimbali ya kimaendeleo ” alifafanua Bw. Tutuba.
Balozi wa Ujerumani nchini Tanzania Mhe. Regine Hess, akizungumza wakati wa halfa ya utiaji saini mkataba wa msaada wenye thamani ya Euro milioni 10 sawa na shilingi bilioni 23.7 kwa ajili ya utekelezaji wa Mradi wa kukabiliana na migongano kati ya wanyamapori na binadamu, Mradi wa kuwezesha upatikanaji wa haki za wanawake na watoto na Mradi wa kuandaa maandiko ya kitaalamu ya miradi, jijini Dar es Salaam.

“Nawahakikishia kuwa Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania chini ya uongozi wa Mheshimwa Samia Suluhu Hassan, itafuata taratibu na kanuni zote za kisheria na kuhakikisha kwamba miradi hii inatekelezwa kwa ufanisi na kufikia malengo yaliyokusudiwa” aliongeza Bw. Tutuba.

Bw. Tutuba amemshukuru Balozi wa Ujerumani nchini Tanzania Mhe. Regine Hess kwa niaba ya Shirika la Kimataifa la Maendeleo la Ujerumani kwa msaada huo mkubwa.
Kamishna Msaidizi wa Fedha za Nje Wizara ya Fedha na Mipango Bw. Melckzedek Mbise (kushoto) na Kaimu Mkurugenzi wa Shirika la Maendeleo la Ujerumani Bw. David Lahl wakifuatilia hotuba ya Katibu Mkuu Wizara ya Fedha na Mipango, Bw. Emmanuel Tutuba (hayupo pichani) wakati wa hafla ya utiaji saini, jijini Dar es Salaam.

Kwa Upande wake Balozi wa Ujerumani nchini Tanzania Mhe. Regine Hess, amesema kuwa Serikali ya Ujerumani itaendelea kushirikiana na Serikali ya Tanzania katika utekelezaji wa miradi mbalimbali ya maendeleo

Naye Naibu Katibu Mkuu wa Wizara ya Katiba na Sheria, Dkt. Khatibu Kazungu, aliahidi kusimamia fedha hizo ili kuhakikisha mradi unatekelezwa kwa ufanisi na kwa wakati.
Katibu Mkuu Wizara ya Fedha na Mipango, Bw. Emmanuel Tutuba (katikati) na Balozi wa Ujerumani nchini Tanzania Mhe. Regine Hess, wakiwa katika picha ya pamoja na watumishi wa Wizara ya Fedha na Mipango baada ya halfa ya utiaji saini. Kutoka kulia ni Naibu Katibu Mkuu wa Wizara ya Maliasili na Utalii Bw. Juma Selemani Mkomi, na Naibu Katibu Mkuu wa Wizara ya Katiba na Sheria Dkt. Khatibu Kazungu na kushoto ni Mkuu wa Ushirikiano wa Ujerumani na Tanzania Dkt. Katrin Bornemann, jijini Dar es Salaam.

Kwa upande wa Naibu Katibu Mkuu wa Maliasili na Utalii, Bw. Juma Selemani Mkoni, alisema kuwa Wizara hiyo imekua ikinufaika na misaada mbalimbali kutoka Serikali ya Shirikisho la Jamhuri ya Ujerumani ambapo kwa kipindi cha miaka mitano (2017 -2022) wizara hiyo imepokea kiasi cha Sh. Bilioni 350.

Tanzania imenufaika na misaada kutoka Serikali ya Shirikisho la Jamhuri ya Ujerumani katika maeneo mbalimbali ikiwemo Sekta ya maji, Sekta ya nishati, matumizi endelevu ya maliasili na utunzaji wa mazingira, usimamizi bora wa fedha za umma na fedha za kuandaa maandiko ya miradi.

No comments:

Post a Comment