Foreign Exchange Rates

DStv Advert_020324

DStv Advert_020324

SBT Tanzania Advert_291123

Thursday 4 May 2023

BENKI YA NBC YAZINDUA KAMPENI MPYA YA "SHINDA MECHI ZAKO NA NBC"

Mkuu wa Bidhaa za NBC, Abel Kaseko akiongea na waandishi wa habari wakati wa uzinduzi wa kampeni mpya inayojulikana kama "Shinda Mechi Zako na NBC". Kampeni ya "Shinda Mechi Zako na NBC", inalenga kuongeza thamani kwa wateja wa NBC na kukuza ukuaji wao wa kifedha na uchumi wa nchi. Kampeni ina lengo la kuwafikia wateja binafsi, waajiriwa, wamiliki wa biashara ndogo, mawakala na wengine wanaotumia huduma za benki za kimtandao kupitia NBC. Pembeni yake ni Mkuu wa Masoko ya NBC, David Raymond Hafla ya uzinduzi huu imefanyika jijini Dar es salaam.

 Mkuu wa Masoko ya NBC, David Raymond (wa kwanza kushoto) na Mkuu wa Bidhaa za NBC, Abel Kaseko (wa tatu kushoto) wakiwa katika picha ya pamoja na waandishi na wachambuzi wa michezo kutoka vituo mbalimbali vya redio na luninga wakati wa uzinduzi wa kampeni mpya inayojulikana kama "Shinda Mechi Zako na NBC". Kampeni ya "Shinda Mechi Zako na NBC", inalenga kuongeza thamani kwa wateja wa NBC na kukuza ukuaji wao wa kifedha na uchumi wa nchi. Kampeni ina lengo la kuwafikia wateja binafsi, waajiriwa, wamiliki wa biashara ndogo, mawakala na wengine wanaotumia huduma za benki za kimtandao kupitia NBC. Hafla ya uzinduzi huu imefanyika jijini Dar es salaam.   

3, Mei, 2023: Benki ya Taifa ya Biashara (NBC) imezindua kampeni mpya inayojulikana kama "Shinda Mechi Zako na NBC". Kampeni ya "Shinda Mechi Zako na NBC", inalenga kuongeza thamani kwa wateja wa NBC na kukuza ukuaji wao wa kifedha na uchumi wa nchi. Kampeni ina lengo la kuwafikia wateja binafsi, waajiriwa, wamiliki wa biashara ndogo, mawakala na wengine wanaotumia huduma za benki za kimtandao kupitia NBC. 

Kwa kutambua changamoto mbalimbali zinazowakabili watu wa kada mbali mbali, Benki ya NBC imepanga kuwasaidia kutatua changamoto hizo kupitia ushauri na huduma za kifedha ambazo ni suluhisho za changamoto hizo na mechi na hivyo kuja na jina “Shinda mechi zako na NBC”.


Kupitia kampeni hii NBC imetumia baadhi ya wachezaji nyota wa ligi kuu ya NBC. Kupitia kampeni hii, wateja wataweza kunufaika na gharama nafuu za miamala kama vile kuweka standing order bure kabisa, kulipia kwa kadi huduma za mtandaoni kwa punguzo la bei, na upatikanaji wa mikopo binafsi na ya biashara hadi milioni 150 ndani ya masaa 48. 

Aidha, wateja wanaweza kupata faida ya hadi asilimia 7% kwenye akaunti zao za NBC Malengo. Wateja pia wanaweza kupata mkopo wa kumalizia nyumba kwa gharama nafuu ili kukamilisha ndoto zao za ujenzi wa nyumba. Kampeni ya "Shinda Mechi Zako na NBC" inalenga kuimarisha ustawi wa kifedha wa wateja wa NBC na kusaidia juhudi za serikali katika kutoa huduma za kifedha, kukuza uchumi wa watanzania. 

NBC inaamini kuwa kampeni hii itawapa wateja faida kubwa na kuboresha thamani na uzoefu wa benki yao. Akiongea wakati wa uzinduzi wa kampeni hiyo,, Mkuu wa Bidhaa za NBC, Abel Kaseko alisema, "Tuna furaha kuzindua kampeni ya 'Shinda Mechi Zako na NBC', ambayo ipo kwa ajili ya kuwapa nguvu wateja wetu na kuwasaidia kufikia malengo yao ya kifedha kwa kuongeza thamani na uzoefu wao wa benki. Kampeni hii itawapa wateja wetu huduma za KIbenki zenye gharama nafuu na rahisi, na pia kusaidia kukuza uchumi wao." 


Kwa upande wake Mkuu wa Masoko ya NBC, David Raymond, alisema, "Tuna furaha kuzindua kampeni ya 'Shinda Mechi Zako na NBC' kwani ni sehemu ya ahadi yetu ya kuendelea kutoa huduma nafuu na rahisi za kibenki zinazokidhi mahitaji ya wateja wetu. Tunaamini kuwa huduma hizi zitawasaidia wateja wetu kutimiza malengo yao ya kiuchumi na kijamii na pia kuchangia katika ukuaji wa uchumi binafsi na wa taifa kwa ujumla." 


Pamoja na malengo mengine, Kampeni inalenga kukuza upatikanaji wa huduma za kifedha na kuhamasisha zaidi watanzania kutumia huduma za benki. Pia ni sehemu ya ahadi kubwa ya NBC ya kusaidia juhudi za serikali ya Tanzania katika kukuza uchumi jumuishi. 

 

        

No comments:

Post a Comment