Foreign Exchange Rates

DStv Advert_020324

DStv Advert_020324

SBT Tanzania Advert_291123

Wednesday 13 October 2021

RC MAKALLA: HUDUMA BORA KWA WATEJA NA UNAFUU WA RIBA KATIKA MABENKI NI VIVUTIO KWA WATEJA

Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam Amos Makala (katikati) na Afisa Mtendaji Mkuu wa China Dasheng Bank, Guydon Chihwalo (kushoto) wakikata keki kuashiria uzinduzi wa Wiki ya Huduma kwa wateja. Kulia ni mfanyakazi wa benki hiyo, Tumakwezi Sayi.
Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam Amos Makala akizungumza jambo katika hafla hiyo.
  • Azindua Wiki ya Huduma kwa wateja China Dasheng Bank.
Mkuu wa Mkoa wa Dar es salaam Mhe. Amos Makalla amezindua Wiki ya Huduma kwa wateja ya China Dasheng Bank ambapo ametoa wito kwa Taasisi za Kifedha nchini kutoa huduma bora kwa wateja wao.

RC Makalla pia ametoa wito kwa Taasisi hizo kubuni bidhaa zinazoendana na wakati husika ikiwa ni pamoja na mikopo yenye riba nafuu.

Aidha RC Makalla ameipongeza Benki ya China Dasheng iliyoanzishwa miaka miwili iliyopita kwa kutengeneza faida ya Shilingi bilioni 5 na kuwa na mtaji wa bilioni 112.

Hata hivyo RC Makalla ametoa wito kwa benki hiyo kutanua huduma za matawi mikoani na nchini China ili kuwasaidia Wafanyabiashara wanaoendesha Biashara nchini China.

Pamoja na hayo RC Makalla amesema Serikali itaendelea kuboresha mazingira ya biashara ili kuvutia Uwekezaji na amewahakikishia usalama.

No comments:

Post a Comment