Foreign Exchange Rates

Absa Loan Campaign_160426

Absa Loan Campaign_160426

CRDB Bank Advert_070325

Friday, 5 June 2026

ACCESS BANK GROUP YASAINI MKATABA WA DOLA MILIONI 500 NA IFC KUPANUA UPATINAKANAJI WA PATO LA NDANI AFRIKA

Mwenyekiti wa Access Holdings, Aigboje Aig-Imoukhuede (kulia), pamoja na Mkurugenzi Mtendaji wa Shirika la Fedha la Kimataifa (IFC), Makhtar Diop, wakitia saini makubaliano ambapo IFC—ambalo ni tawi la sekta binafsi la Kundi la Benki ya Dunia—italipatia Kundi la Access Bank kiasi cha dola milioni 500. Mtaji huo unalenga kuimarisha masoko ya mitaji ya sarafu za ndani na kupanua upatikanaji wa mikopo ya bei nafuu kwa biashara kote barani Afrika, hatua inayoleta manufaa ya moja kwa moja kwenye masoko ambayo benki hiyo inafanya kazi, ikiwemo Tanzania.

Dar es Salaam, Tanzania | 3 Juni 2026

Ushirikiano huu muhimu unaoungwa mkono na Benki ya Dunia unawanufaisha moja kwa moja wateja wa Access Bank Tanzania pamoja na jumuiya ya wafanyabiashara nchini Tanzania.

Dar es Salaam Jumanne 2 Juni 2026 Access Bank Group, ambayo ni mmiliki wa benki ya Access Bank Tanzania, imesaini makubaliano ya dola milioni 500 na Shirika la Fedha la Kimataifa (IFC), ambayo ni tawi ya sekta binafsi yaKundi la Benki ya Dunia. Ushirikiano huo unalenga kuimarisha masoko ya mitaji ya sarafu za ndani na kupanua upatikanaji wa bei nafuu kwa biashara kote barani Afrika, na inaleta manufaa ya moja kwa moja kwa masoko ambayo Access Bank inafanya kazi, ikiwa ni pamoja na Tanzania.

Kwa biashara nchini Tanzania, makubaliano haya yanalenga kutatua changamoto za ubadilishaji wa fedha za kigeni. Kampuni zinapolazimika kukopa kwa sarafu za kigeni, mabadiliko ya viwango vya kubadilishia fedha yanaweza kupunguza faida, kuvuruga mipango ya kifedha, na hatimaye kukandamiza uwekezaji. Kupitia suluhisho hili la upatikanaji wa mikopo ya sarafu ya ndani—kiwango ambacho kinawezekana kwa upekee wa ushirikiano kati ya Access Bank na IFC—wateja wa Access Bank Tanzania, kuanzia wajasiriamali wadogo (SMEs) hadi makampuni makubwa, sasa wataweza kupata mikopo yenye gharama nafuu na inayotabirika ili kusaidia ukuaji wao wa muda mrefu.

Makubaliano haya na IFC ni hatua muhimu kwetu, lakini manufaa yake makubwa yataonekana hapa nchini Tanzania,” alisema Imani John, Mkurugenzi Mtendaji wa Access Bank Tanzania. 

Wateja wetu, iwe wanaendesha biashara ndogo au wanasimamia shughuli za makampuni makubwa, wanahitaji huduma za kifedha ambazo hazitawaweka katika changamoto ya mabadiliko ya thamani ya sarafu. Ushirikiano huu unaimarisha uwezo wetu wa kutoa huduma hizo, huku tukiungwa mkono na uaminifu pamoja na ushawishi wa Kundi la Benki ya Dunia.”

Access Bank Tanzania kwa sasa inahudumia wateja katika miji ya Dar es Salaam, Mwanza, Arusha, na Dodoma. Ikiwa na mawakala 936 wa Access Wakala na vituo 98 vya BancEasy Satellite, benki hiyo inarahisisha upatikanaji wa huduma za kifedha kwa wananchi ambao hapo awali walikuwa hawajafikiwa na sekta ya kibenki.

Kwa biashara za Kitanzania zinazokua, zinazopanua shughuli zake ndani na nje ya nchi, au zinazovutia uwekezaji, upatikanaji wa huduma za kifedha zinazotegemewa na zenye gharama nafuu ni jambo muhimu katika kufanikisha malengo hayo. 

Ushiriki wa IFC katika ushirikiano huu hauleti mtaji pekee, bali pia unaleta uzoefu wa miongo kadhaa katika kuendeleza masoko ya fedha kwenye uchumi unaokua duniani. 

Kwa wateja wa Access Bank Tanzania, hii ina maana ya kuwa na mshirika wa kibenki ambaye hayupo karibu nao hapa nchini pekee, bali pia ameunganishwa na fursa za kimataifa. Hatua hii inatuwezesha kutoa suluhisho za kifedha, maarifa ya masoko, na huduma za kuvuka mipaka ambazo hapo awali zilikuwa vigumu kufikiwa na biashara nyingi katika soko hili.

Ushirikiano wetu na IFC hauongozwi tu na upatikanaji wa mtaji, bali pia na uzoefu wetu wa miaka mingi katika kuendeleza masoko ya fedha kwenye mataifa mbalimbali. Hatua hii inawapa wateja wa Access Bank Tanzania suluhisho thabiti na fursa za kimataifa ambazo hapo awali zilikuwa ngumu kufikiwa.

Makubaliano haya yanaashiria hatua nyingine muhimu katika ukuaji endelevu wa Access Bank Tanzania. Benki hii, ambayo imejishindia tuzo ya Global Brand Frontier Awards 2025 kama Benki Bora ya Ununuzi, Ujumuishaji na Upanuzi wa Soko nchini Tanzania, ina rekodi thabiti ya kugeuza mikakati ya kibiashara kuwa matokeo chanya kwa wateja wake. 

Kupitia ushirikiano huu wa kimataifa na IFC, Access Bank Tanzania inaingia katika hatua mpya ikiwa na zana, ufikiaji, na usaidizi thabiti wa kitaasisi ili kuwezesha malengo ya kiuchumi ya biashara na jamii inazozihudumia.

Kuhusu Access Bank Tanzania

Access Bank Tanzania, kampuni tanzu ya Access Bank PLC, ni benki kamili ya kibiashara iliyopewa leseni na Benki ya Tanzania na imejitolea kuendesha ukuaji jumuishi kote nchini. Kwa matawi katika Dar es Salaam, Mwanza, Arusha, na Dodoma, na mtandao mpana wa mawakala 936 wa Access Wakala na maduka 98 ya BancEasy, Benki inatoa huduma za kibenki zinazofaa na salama kwa watu binafsi, SMEs, na makampuni nchi nzima. Kwa kutumia mfumo mpana wa kikanda wa Kundi, teknolojia, na usimamizi imara,Access Bank Tanzania inatoa suluhisho za kibenki za kidijitali na za jadi za kiwango cha dunia kutoka kwa huduma za kibenki za kibinafsi na biashara hadi huduma za kampuni na uwekezaji, huku ikipanua ushirikishwaji wa kifedha na kuwawezesha wateja katika jamii ambazo hazijafikiwa vya kutosha.

Kulingana na ajenda pana zaidi ya uendelevu ya Access Bank Group, Access Bank Tanzania inajumuisha mazoea ya kuwajibika na maadili katika shughuli zake zote. Benkiimejitolea kukuza maendeleo ya kiuchumi ambayo si tu yenye faida bali pia yenye athari za kijamii na kuwajibika kwa mazingira. Katikati ya shughuli zake ni maadiliyanayobainisha chapa ya Access: Uongozi, Ubora, Wafanyakazi Wenye Nguvu, Shauku kwa Wateja, na Ubunifu.

Pata maelezo zaidi kwa: tanzania.accessbankplc.co.tz

Mawasiliano ya Vyombo vya Habari 

Tamala Maerere
Access Bank Tanzania 
Tamala.Maerere@accessbankplc.com

No comments:

Post a Comment