Foreign Exchange Rates

DStv Advert_090724

DStv Advert_090724

SBT Tanzania Advert_291123

Monday 17 August 2020

VODACOM M-KULIMA INAVYOWEZESHA WAKULIMA KUPATA HUDUMA MBALIMBALI

Mrajisi wa vyama vya Ushirika, Dkt. Benson Ndiege, akizungumza kwenye banda la Vodacom katika viwanja vya Nyakabindi kwenye maonesho ya nanenane, wakati wa uzinduzi wa mfumo wa M-Kulima unaowawezesaha wakulima kuwasiliana na kufanya miamala kwa kutumia mtandao wa Vodacom. Pembeni ni naibu Mrajisi, Charles Malunde na Mkuu wa mauzo wa Vodacom Tanzania PLC Kanda ya Ziwa, Ayubu Kalufya (kulia).
Mkuu wa Mauzo Vodacom Tanzania PLC Kanda ya Ziwa, Ayubu Kalufya akizungumza wakati wa uzinduzi wa mfumo wa M-Kulima unaowawezesha wakulima kuwasiliana na kufanya miamala, mfumo huo umezinduliwa kwenye viwanja vya Nyakabindi mkoani Simiyu kwenye maonesho ya nane nane. Mrajisi wa vyama vya Ushirika Dk Benson Ndiege (kushoto) Naibu Mrajisi Charles Malunde.
Wakulima wakifuatilia hotuba za uzinduzi wa mfumo wa Vodacom M-Kulima unaowawezesha kufanya miamala na kuwasiliana kwa urahisi, mfumo huo umezinduliwa kwenye viwanja vya nane nane Nyakabindi mkoani Simiyu
Wafanyakazi wa Vodacom Tanzania PLC wakiwa katika picha ya pamoja na Mrajisi baada ya uzinduzi wa M-Kulima. 

No comments:

Post a Comment