Foreign Exchange Rates

DStv Advert_020324

DStv Advert_020324

SBT Tanzania Advert_291123

Friday 19 April 2024

NMB PESA AKAUNTI YAWAVUTIA WAKAGUZI WA NDANI AFRIKA, ARUSHA

Mkaguzi Mkuu wa Ndani wa Benki ya NMB, Benedicto Baragomwa (kushoto), akizungumza na Mkurugenzi wa Halmashauri ya Wilaya ya Monduli, Happiness Laizer pembezoni mwa Mkutano wa 10 wa Shirikisho la Taasisi za Wakaguzi wa Ndani Afrika (AFIIA) uliofanyika katika Kituo cha Kimataifa cha Mikutano cha Arusha (AICC). Katikati ni Meneja Mahusiano Huduma za Serikali wa NMB Kanda ya Kaskazini, Peter Masawe.

Ubunifu wa bidhaa bora wa Benki ya NMB pamoja na uwekezaji wenye tija inaoufanya kuwahudumia wateja kwa ufanisi vimekuwa kivutio kikubwa kwenye mkutano wa wakaguzi wa ndani wa Afrika unaofikia tamati leo jijini Arusha.


Wafanyakazi kwenye banda la benki hiyo katika viwanja vya Ukumbi wa AICC unapofanyika mkutano huo wamesema moja ya vitu vinavyowavutia wajumbe wanaowatembelea ni bidhaa ya NMB Pesa Akaunti kutokana na hasa urahisi na wepesi wa kuifungua.


NMB inatumia huduma hiyo, ambayo ni moja ya mikakati ya kufungua akaunti mpya za wateja milioni 1.5 mwaka huu, kutekeleza ajenda yake ya kuwajumuisha Watanzania zaidi kifedha na kupeleka huduma zake vijijini.


Aidha maafisa wa NMB walisema wajumbe wanaotembelea banda lao wanavutiwa pia na gharama nafuu ya TZS 1,000 ya kuifungua akaunti ya NMB Pesa pamoja na uwezo wake wa kumwezesha inayehimiliki kukopa hadi TZS 500,000 kwa kutumia simu ya mkononi kupitia huduma ya Mshiko Fasta.


Kwa mujibu wa Meneja wa tawi la NMB Clock Tower Arusha, Bw Praygod Mphuru, benki hiyo ni moja ya wadhamini wa mkutano huo wa siku tatu uliofunguliwa rasmi Jumatano na Makamu wa Rais, Dr Philip Mpango.


Mkutano huo ulitanguliwa na kikao maalumu cha siku mbili ambacho nacho maafisa waandamizi wa NMB walishiriki kikamilifu kwa ajili ya kubalishana uzoefu, kujifunza vitu vipya na kwenda sambamba na mabadiliko yanayotokea katika tasnia ya usimamizi wa ndani duniani.

Mikutano hiyo miwili imeudhuriwa na takribani wajumbe 2000 wengi wakiwa Watanzania na wengine wakitoka katika nchi 26 za Afrika pamoja na mataifa kadhaa nje ya bara hili.

“Tunautumia pia mkutano huu kwa ukubwa wake kama fursa ya kuonyesha umahili wetu wa kutoa huduma bora, ubunifu mkubwa wa bidhaa na jinsi tunavyowekeza vilivyo katika teknolojia mpya za kisasa,” Bw Mphuru alibainisha.

DKT. NCHEMBA: TANZANIA IMEPIGA HATUA KIUCHUMI NA KIDEMOKRASIA

Waziri wa Fedha, Mhe. Dkt. Mwigulu Lameck Nchemba Madelu (Mb) (wa nne kulia), Afisa Mtendaji Mkuu wa Shirika la Marekani la Changamoto za Milenia (MCC), Bi. Alice Albright (wa tano kulia), Naibu Afisa Mtendaji Mkuu wa Shirika la Marekani la Changamoto za Milenia (MCC), Bi. Chidi Blyeden (wa tano kushoto), Katibu Mkuu Wizara ya Fedha, Dkt. Natu El-maamry Mwamba (wa tatu kulia), Katibu Mkuu Ofisi ya Rais Fedha na Mipango, Dkt. Juma Malik Akil (wa nne kushoto), Katibu Mtendaji wa Tume ya Mipango, Bw. Lawrence Mafuru (wa kwanza kulia), Mratibu wa Tanzania wa Mradi wa MCC Dkt. Hamisi Mwinyimvua (wa pili kulia), Kiongozi wa Timu ya MCC nchini Tanzania Bw. Nilan Fernando (kushoto), Kamishna wa Idara Fedha za Nje Wizara ya Fedha, Bw. Rished Bade na Makamu wa Rais wa MCC anayeshughulikia Sera na ukaguzi, Bi. Alicia Mandaville, mara baada ya kumalizika kwa Mkutano wao uliofanyika Makao Makuu ya Shirika hilo jijini Washington D.C, ambapo walijadiliana ushirikiano wa shirika hilo na Tanzania katika programu za awali (threshold programs) zitakazolenga katika mageuzi ya kisera na kitaasisi ili kupunguza umasikini na kuchochea ukuaji wa uchumi, kando ya mikutano ya Majira ya Kipupwe (Spring Meetings) ya Benki ya Dunia na Shirika la Fedha la Kimataifa (IMF) inayoendelea nchini Marekani.
Waziri wa Fedha, Mhe. Dkt. Mwigulu Lameck Nchemba Madelu (Mb), akisalimiana na Afisa Mtendaji Mkuu wa Shirika la Marekani la Changamoto za Milenia (MCC), Bi. Alice Albright, baada ya kukutana na kufanya mazungumzo Makao Makuu ya Shirika hilo, jijini Washington D.C, kando ya mikutano ya Majira ya Kipupwe (Spring Meetings) ya Benki ya Dunia na Shirika la Fedha la Kimataifa (IMF). inayoendelea nchini Marekani, ambapo walijadiliana namna ya kuimarisha ushirikiano kati ya Shirika hilo na Tanzania katika programu za awali (threshold programs) zitakazolenga kufanya mageuzi ya kisera na kitaasisi ili kupunguza umasikini na kuchochea ukuaji wa uchumi.
Waziri wa Fedha, Mhe. Dkt. Mwigulu Lameck Nchemba Madelu (Mb) (kulia), akiagana na Naibu Afisa Mtendaji Mkuu wa Shirika la Marekani la Changamoto za Milenia (MCC), Bi. Chidi Blyeden, baada ya kumalizika kwa Mkutano wao uliofanyika Makao Makuu ya Shirika hilo, jijini Washington DC.
Ujumbe wa Tanzania ulioongozwa na Waziri wa Fedha, Mhe. Dkt. Mwigulu Lameck Nchemba Madelu (Mb) (kulia), ukiwa katika mkutano na Uongozi wa Shirika la Marekani la Changamoto za Milenia (MCC), ambapo walijadiliana masuala ya ushirikiano Shirika hilo na Tanzania katika programu za awali (threshold programs).
Katibu Mkuu Wizara ya Fedha, Dkt. Natu El-maamry Mwamba, akizungumza jambo wakati wa Mkutano wa Ujumbe wa Tanzania ulioongozwa na Waziri wa Fedha, Mhe. Dkt. Mwigulu Lameck Nchemba Madelu (Mb) na Uongozi wa Shirika la Marekani la Changamoto za Milenia (MCC).
Katibu Mtendaji wa Tume ya Mipango, Bw. Lawrence Mafuru, akizungumza jambo wakati wa Mkutano wa Ujumbe wa Tanzania ulioongozwa na Waziri wa Fedha, Mhe. Dkt. Mwigulu Lameck Nchemba Madelu (Mb) (hayupo pichani) na Uongozi wa Shirika la Marekani la Changamoto za Milenia (MCC).
Uongozi wa Shirika la Marekani la Changamoto za Milenia (MCC), ukifuatilia kwa umakini majadiliano kati yake na Ujumbe wa Tanzania ulioongozwa na Waziri wa Fedha, Mhe. Dkt. Mwigulu Lameck Nchemba Madelu (Mb) (hayupo pichani), katika Mkutano wao uliofanyika Makao Makuu ya Shirika hilo jijini Washington D.C.
Naibu Afisa Mtendaji Mkuu wa Shirika la Marekani la Changamoto za Milenia (MCC), Bi. Chidi Blyeden, akizungumza jambo wakati wa Mkutano wa Uongozi wa Shirika hilo na Ujumbe wa Tanzania.

Na Benny Mwaipaja, Washington D.C.

Waziri wa Fedha, Mhe. Dkt. Mwigulu Lameck Nchemba, amelihakikishia Shirika la Marekani la Changamoto za Milenia (Millennium Challenge Corporation-MCC) kwamba Tanzania imepiga hatua kubwa katika masuala ya haki za binadamu, utawala bora, demokrasia na usimamizi imara wa uchumi wa nchi.

Dkt. Nchemba amesema hayo alipoongoza ujumbe wa Tanzania, kukutana na kufanya mazungumzo na uongozi wa juu wa Shirika hilo, ukiongozwa na Makamu wake wa Rais Mhe. Alicia Mandaville, Jijini Washington D.C nchini Marekani, ambapo pande hizo mbili zilijadili namna ya kuharakisha utekelezaji wa mpango wa kusaidia mageuzi ya kisera na kitaasisi ili kutatua vikwazo vya ukuaji uchumi, kupitia ruzuku itakayotolewa na Shirika hilo.

Alisema kuwa hatua hiyo si tu kwamba ni utekelezaji wa vigezo vilivyowekwa na Shirika hilo ili Tanzania iweze kunufaika na mpango huo unaolenga kutoa misaada ya kiufundi, bali ni nia ya dhati ya Serikali ya Awamu ya Sita inayoongozwa na Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan, Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, ya kulinda uhuru wa watu.

Dkt. Nchemba aliihakikishia MCC kwamba Tanzania iko tayari kushirikiana na Serikali ya Marekani katika mpango huo na kuuomba uongozi huo kuuamini mchakato huo na ikiwezekana kuipatia nchi mradi mkubwa wa COMPACT II, utakao iwezesha nchi kupata fedha za kutekeleza miradi ya kimkakati katika sekta za usafirishaji, nishati, na maji.

EXCITING CAREER OPPORTUNITIES AT NMB BANK PLC


We are a leading bank, committed to your growth and welfare. Join our team of best talents in the market, together we will continue to impact and transform lives through meaningful work, innovative products and solutions while driving the sustainability agenda. 

We are renowned for investing, nurturing and transforming careers. Our commitment to diversity, equity and inclusion has led us to become the first financial institution in Africa to attain the most coveted EDGE Certification (EDGE Assess). We are more than a bank.

The following vacancies are currently available;
  • Insights & Customer Journey Manager - Head Office (Closing date; 23 April 2024)
  • Relationship Manager; Mortgage Financing - Highlands Zone (Closing date; 30 April 2024)
  • Senior Audit Associate; Data Analytics - Head Office (Closing date; 22 April 2024)
  • Senior Manager; Affluent - Head Office (Closing date; 23 April 2024)
  • Senior Manager; Corporate Banking - Head Office (Closing date; 26 April 2024)
  • Senior Manager; Mass Liabilities - Head Office (Closing date; 26 April 2024)

IMPACT BUSINESS BREAKFAST, 24 APRIL 2024 - HYATT REGENCY DAR ES SALAAM


BERNICE FERNANDES APPOINTED AS BOARD MEMBER FOR GLOBAL ENTREPRENEURSHIP FESTIVAL


In a significant development, Bernice Fernandes, a prominent figure in Tanzania's entrepreneurial landscape, has been appointed as a Board Member for the esteemed Global Entrepreneurship Festival. The festival, renowned as the world's largest entrepreneurship event, is poised to attract over 20 million viewers globally, with 12 concurrent events scheduled to unfold.

Set against the backdrop of the Entrepreneurship Village (E-Village) in Ondo State, Nigeria—a burgeoning hub often likened to Africa's Silicon Valley—the festival promises a convergence of global business titans, political leaders, and aspiring entrepreneurs.



Under the esteemed patronage of Nigeria's President, His Excellency Bola Ahmed Tinubu, and the distinguished presence of Africa's wealthiest woman, Folorunso Alakija, the festival garners unprecedented momentum. Noteworthy luminaries such as the CEO of Reebok, the Director General of the World Trade Organization, and the President of the African Development Bank, among others, are slated to grace the event with their insights.

The festival's agenda is as diverse as it is compelling, featuring a plethora of activities ranging from startup pitch competitions to a women's congress, leadership forums, trade fairs, and innovation showcases. With elements like hackathons, fashion shows, and concerts, the festival promises a dynamic blend of business and cultural exchange.

At the helm of this global initiative stands Bernice Fernandes, Founder and CEO of the Accelerate Business Group and the Accelerate Women's Initiative in Tanzania. Armed with an impressive academic pedigree—including an MBA in Entrepreneurship, a Masters in International Business, and a Bachelors in Finance from the United States—Bernice is eminently qualified to serve on international boards.

Accelerate Business Group is a business advisory firm for growth, providing strategic consulting, corporate training, coaching as well as facilitation services.

Accelerate Women's Initiative hosts executive conferences, masterclasses as well as a powerful networking platform for women in business. 

VODACOM YAZINDUA SIMUJANJA MAALUMU KWA WATEJA WENYE ULEMAVU

Balozi wa Pakistani nchini, Siraj Ahmad Khan (kushoto), Mkurugenzi wa Biashara wa Vodacom Tanzania, Linda Riwa (katikati) na Afisa Mtendaji Mkuu wa kampuni ya Digit, Abdul Rehman Mahmood (kulia) wakiwa kwenye picha ya pamoja wakati wa uzinduzi wa simu maalum iitwayo 'Smart Kitochi+' kwa ajili ya watu wenye ulemavu wa kuona na kusikia huku ikiongeza matumizi ya dijitali nchini. Hafla hiyo ilifanyika jana jijini Dar es Salaam.

Dar es Salaam – Aprili 18, 2024: Ili kuimarisha ushirikishwaji na kuongeza matumizi ya huduma na bidhaa za kidijitali nchini, kampuni ya teknolojia na mawasiliano ya Vodacom Tanzania PLC imezindua simujanja ya kidijitali inayoitwa 'Smart Kitochi +' ambayo imeundwa ikiwa na vipengele muhimu kwa ajili ya wateja wasiosikia na wasioona.


Akizungumza katika hafla ya uzinduzi jijini Dar es Salaam, Mkurugenzi wa Biashara wa kampuni hiyo, Bi. Linda Riwa, amesema kuwa uzinduzi huu ni sehemu ya juhudi endelevu za kampuni hiyo za kukuza ushirikishwaji huku ikiunga mkono serikali katika azma yake ya kuchochea matumizi ya bidhaa na huduma za kidigitali.


"Tunafurahia mapinduzi haya ya kuleta bidhaa na huduma za kidigitali na za kibunifu kwa wateja wetu wenye mahitaji mbalimbali kote nchini. Leo, tunazindua simu ya kipekee ya kidijitali inayoitwa 'Smart Kitochi+' ambayo mbali na sifa kama kioo kikubwa na cha kugusa, uwezo mkubwa wa kuhifadhi na betri inayodumu muda mrefu, simu hii pia itawanufaisha wateja wetu wenye ulemavu wa kusikia na kuona,” anasema Linda.


“Simu hii inajumuisha teknolojia ya kugusa na sauti, ikiruhusu wateja wenye changamoto hizi kupata huduma zetu bila kutegemea msaada wa mtu mwingine. Haya ni mapinduzi muhimu katika sekta ya utoaji huduma za mawasiliano, ikizingatiwa kuwa serikali inahimiza watoa huduma kuzingatia ushirikishwaji katika utoaji wa huduma kwa wateja,” aliongeza Linda.


Uzinduzi wa simu hii ni ingizo la kipekee sokoni ukilinganisha na matoleo mengine, ikiwa na uwezo wa kuchochea ushirikishwaji katika matumizi ya huduma za mawasiliano ya kidigitali. Pia ina ubora wa hali ya juu ikiwa na kioo kikubwa na cha kugusa (2.8”), uwezo mkubwa wa kuhifadhi vitu kwenye 8GB na betri inayodumu muda mrefu ya 3000mAh.

Toleo hili jipya la 'Smart Kitochi+' ni sehemu ya juhudi za Vodacom kuwapeleka wateja wake kwenye matumizi ya kidigitali, ikiwa ni pamoja na mtandao wa 4G, ambao bado una watumiaji wachache ikilinganishwa na idadi ya watumiaji wa simu za mkononi nchini Tanzania.

"Tunajivunia kuwa mtandao unaoongoza nchini, tukitoa huduma za kidigitali za ubunifu kwa zaidi ya wateja milioni 21. Kuwa na idadi kubwa ya wateja pekee haitoshi; tunataka wateja wetu wanufaike na mapinduzi ya kidigitali yanayoendelea na ubunifu mkubwa tunaoingiza kwenye bidhaa zetu. Kwa kuanzisha bidhaa za kisasa kama 'Smart Kitochi+' tunaamini tutachochea wateja wengi zaidi kuhama kutoka kwenye mfumo wa 2G na kuanza kufurahia huduma mbalimbali za kidigitali zinazotolewa na mtandao wetu wa kasi wa 4G na 5G uliosambaa nchini na hatimaye kuongeza matumizi ya simujanja ambayo kwa sasa ni asilimia 32," alifafanua Bi. Linda.

Thursday 18 April 2024

FA CUP SEMI-FINALS MAN CITY vs CHELSEA NDANI YA DStv COMPACT

 

TIGO YAZINDUA FIBER KWA AJILI YA INTANETI YA NYUMBANI NA OFISINI

Mkuu wa Kitengo cha Tigo Biashara, John Sicilima akiwaelezea waandishi wa habari (hawapo pichani) kuhusu huduma mpya ya Tigo Fiber kwa ajili ya matumizi ya nyumbani na maofisini. Kulia ni Mkuu wa Chapa na Mawasaliano Tigo, Anna Loya.
  • Mji wa Mbweni jijini Dar es Salaam kuwa mnufaika wa kwanza wa huduma hii ya intaneti
Dar es Salaam, Aprili 16, 2024: Kampuni inayoongoza kwa mtindo wa maisha ya kidijitali nchini Tanzania, Tigo, imezindua huduma ya mtandao ya kwanza ya aina yake ya Fiber to Home na Fiber to Office ambayo imeundwa kuwezesha watumiaji na wafanyabiashara kupata huduma za uhakika, na intaneti yenye spidi nyumbani na Ofisini.

Huduma hii muhimu inasisitiza dhamira ya Tigo ya kusaidia mabadiliko ya kidijitali nchini Tanzania kwa kusambaza teknolojia na huduma za kisasa zinazomnufaisha kila mtumiaji nyumbani na maeneo ya biashara.

Akizungumzia dhamira ya Tigo ya kuleta mabadiliko katika hali ya kidijitali nchini Tanzania, Mkurugenzi Mtendaji wa Tigo Tanzania, Kamal Okba alisema, “Tunajivunia kuwa kampuni ya kwanza ya mawasiliano kuzindua mtandao wa Fiber hadi Nyumbani na Ofisini nchini Tanzania. Hii inaimarisha nafasi yetu kama viongozi katika mageuzi ya mtindo wa maisha ya kidijitali na wakati huo huo ikichangia katika utekelezaji wa ajenda ya kidijitali ya Tanzania.”

Naye Mkuu wa Chapa (Brand) na Mawasiliano Tigo, Anna Loya, alisema, “Tuna dhamira ya ubunifu na kuridhika kwa wateja, tumewekeza kwa kiasi kikubwa katika kusambaza teknolojia ya kisasa ya fiber ili kutoa uzoefu usio na kifani wa muunganisho. kuwezesha biashara na kaya na tija na ushirikiano ulioimarishwa. Huduma mpya ya Tigo Fiber inaahidi kasi ya mtandao ya kasi zaidi, huduma zisizo na kifani na usaidizi kwa wateja ili kuleta mapinduzi katika namna Watanzania wanavyoungana na kujihusisha na ulimwengu wa kidijitali.”

DKT. NCHEMBA ATETA NA UONGOZI WA IMF KUHUSU UTEKELEZAJI WA BAJETI

Waziri wa Fedha, Mhe. Dkt. Mwigulu Lameck Nchemba (Mb) (katikati), Mkurugenzi Mtendaji wa Kundi la Kwanza la Nchi za Afrika la Shirika la Fedha la Kimataifa (IMF) (The Executive Director of the IMF– Africa Group 1 Constituency (AfG1), Bw. Willie Nakunyada (wapili kushoto), Katibu Mkuu Wizara ya Fedha, Dkt. Natu El-maamry Mwamba (wa pili kulia), Katibu Mkuu Ofisi ya Rais Fedha na Mipango Zanzibar, Dkt. Juma Malik Akil (wa kwanza kushoto), na Gavana wa Benki Kuu ya Tanzania, Bw. Emmanuel Tutuba (wa kwanza kulia) wakiwa katika picha ya pamoja baada ya kikao chao wakati wa mikutano ya Majira ya Kipupwe (Spring Meetings) ya Benki ya Dunia na Shirika la Fedha la Kimataifa (IMF) yenye kauli mbiu ya “Vision to Impact” inayoendelea jijini Washington D.C, nchini Marekani. Katika kikao hicho tathmini ya mwenendo wa uchumi wa Tanzania ilijadiliwa pamoja na utekelezaji wa program ya IMF chini ya mpango wa "Extended Credit Facility-(ECF)" inayofanikisha utekelezaji wa Sera za kiuchumi na upatikanaji wa mikopo nafuu kwa nchi kutoka kwa washirika wa maendeleo.
Waziri wa Fedha, Mhe. Dkt. Mwigulu Lameck Nchemba (Mb), akizungumza jambo wakati akiongoza ujumbe wa Tanzania katika kikao na Mkurugenzi Mtendaji wa Kundi la Kwanza la Nchi za Afrika la Shirika la Fedha la Kimataifa (IMF) (The Executive Director of the IMF– Africa Group 1 Constituency (AfG1), Bw. Willie Nakunyada, wakati wa mikutano ya Majira ya Kipupwe (Spring Meetings) ya Benki ya Dunia na Shirika la Fedha la Kimataifa (IMF).
Mkurugenzi Mtendaji wa Kundi la Kwanza la Nchi za Afrika la Shirika la Fedha la Kimataifa (IMF) (The Executive Director of the IMF– Africa Group 1 Constituency (AfG1), Bw. Willie Nakunyada, akizungumza jambo wakati wa kikao chake na Waziri wa Fedha, Mhe. Dkt. Mwigulu Lameck Nchemba (Mb), aliyeongoza ujumbe wa Tanzania, wakati wa mikutano ya Majira ya Kipupwe (Spring Meetings) ya Benki ya Dunia na Shirika la Fedha la Kimataifa (IMF).
Waziri wa Fedha, Mhe. Dkt. Mwigulu Lameck Nchemba (Mb) (katikati), akisikiza jambo wakati wa kikao na Mkurugenzi Mtendaji wa Kundi la Kwanza la Nchi za Afrika la Shirika la Fedha la Kimataifa (IMF) (The Executive Director of the IMF– Africa Group 1 Constituency (AfG1), Bw. Willie Nakunyada. Wengine katika picha ni Katibu Mkuu Wizara ya Fedha, Dkt. Natu El-maamry Mwamba (kulia) na Katibu Mkuu Ofisi ya Rais Fedha na Mipango Zanzibar, Dkt. Juma Malik Akil (kushoto).
Ujumbe wa Tanzania (kulia) ukiongozwa na Waziri wa Fedha, Mhe. Dkt. Mwigulu Lameck Nchemba (Mb) (wanne kulia), ukiwa katika kikao na Mkurugenzi Mtendaji wa Kundi la Kwanza la Nchi za Afrika la Shirika la Fedha la Kimataifa (IMF) (The Executive Director of the IMF– Africa Group 1 Constituency (AfG1), Bw. Willie Nakunyada, wakati wa mikutano ya Majira ya Kipupwe (Spring Meetings) ya Benki ya Dunia na Shirika la Fedha la Kimataifa (IMF) yenye kauli mbiu ya “Vision to Impact” inayoendelea jijini Washington D.C, nchini Marekani. Wengine katika picha ni Katibu Mkuu Wizara ya Fedha, Dkt. Natu El-maamry Mwamba (wa tatu kulia), Katibu Mkuu Ofisi ya Rais Fedha na Mipango Zanzibar, Dkt. Juma Malik Akil (wa tano kulia), Gavana wa Benki Kuu ya Tanzania, Bw. Emmanuel Tutuba (wapili kulia) na Kamishna wa Idara ya Fedha za Nje Wizara ya Fedha, Bw. Rished Bade (wa sita kulia).
Waziri wa Fedha, Mhe. Dkt. Mwigulu Lameck Nchemba (Mb) (Kulia), akiagana na Mkurugenzi Mtendaji wa Kundi la Kwanza la Nchi za Afrika la Shirika la Fedha la Kimataifa (IMF) (The Executive Director of the IMF– Africa Group 1 Constituency (AfG1), Bw. Willie Nakunyada.

Na Benny Mwaipaja, Washington D.C.

Waziri wa Fedha, Mhe. Dkt. Mwigulu Lameck Nchemba (Mb), ameliambia Shirika la Fedha la Kimataifa (IMF) kwamba utekelezaji wa Bajeti Kuu ya Serikali unaathiriwa na hali mbaya ya hewa inayosababishwa na mabadiliko ya tabianchi ambapo kiasi kikubwa cha fedha ambacho kingeelekezwa kwenye utekelezaji wa miradi ya maendeleo ya wananchi kinaelekezwa kukabiliana na athari za mafuriko yaliyotokea katika maeneo mbalimbali nchini Tanzania kufuatia mvua za el nino zinazoendelea kunyesha.

Dkt. Nchemba ameyasema hayo alipoongoza ujumbe wa Tanzania katika kikao na Mkurugenzi Mtendaji wa Kundi la Kwanza la Nchi za Afrika wa Shirika la Fedha la Kimataifa (IMF), Bw. Willie Nakunyada, kando ya mikutano ya Majira ya Kipupwe (Spring Meetings) ya Benki ya Dunia na Shirika la Fedha la Kimataifa (IMF) inayoendelea jijini Washington D.C, nchini Marekani.

Alisema kuwa wakati wa utekelezaji wa Bajeti inayoendelea ya mwaka 2023/2024 mabadiliko ya tabianchi yameathiri mtiririko wa utoaji wa fedha kwenda kwenye miradi ambayo ingesaidia kwa kiasi kikubwa kuchachua shughuli za kiuchumi badala yake zinatumika kurekebisha miundombinu iliyoharibiwa na mafuriko ikiwemo madaraja, barabara, na miundombinu mingine ya huduma za jamii.

TWO DECADES AGO, TELEVISION WAS A SYMBOL OF WEALTH


By Manish Jangra, Country Head, Samsung Electronics Tanzania.

Dar es Salaam - If you ask me to name the most common electrical appliance that Tanzanians had at home over the past two decades, I will tell you that it was the television.

You might be surprised, but that's largely the reality compared to the current situation where almost every household activity is done with a home appliance.

If you asked anyone during that time why they didn’t buy an electric stove, kettle, refrigerator, washing machine, blender, or air conditioner, they would tell you that it was a luxury to have them and that they increased electricity expenses, thus the cost of living.

But the situation has changed significantly; many people are considering different ways to simplify their daily lives, by doing multiple things within a short time.

According to Statista, in 2024, revenue in the household appliances market in Tanzania reached 3.03 billion US dollars. This market is estimated to grow annually by 5.54% (CAGR 2024-2028).

By 2024, online sales are expected to contribute 1.1% of all revenue in the household appliances market in Tanzania. In addition, the household appliances market is expected to experience a growth of 3.9% in 2025.

KAMPUNI YA SUKARI YA KILOMBERO YATOA MSAADA WILAYA YA KILOMBERO


Morogoro-Kilombero, 17 Aprili 2024; Kampuni ya sukari ya kilombero imetangaza ushiriki wake katika kutoa msaada wa kibinadamu kwa jamii inayoishi wilaya ya Kilombero, ambayo imeathiriwa vibaya na matukio ya mafuriko yanayoendelea nchini kote yaliyo sababishwa na mvua kubwa.


Hafla hii ya utoaji msaada imefanyika katika ofisi ya Mkuu wa Wilaya ya Kilombero, ambapo kampuni imetoa mchango wa tani sita za mahitaji muhimu ya chakula, ikiwa ni pamoja na maharage, unga wa mahindi, na mchele. Mchango huu unatarajiwa kusaidia zaidi ya kaya 500 zilizoathiriwa na mafuriko.


Wakati wa kukabidhi mchango huo, wenye thamani ya Shilingi za Tanzania milioni 15, Bwana Victor Byemelwa, Meneja wa Mawasiliano na Uhusiano na Wadau wa Kampuni ya Kilombero Sugar, Amesema msaada huo ni sehemu ya Programu ya Misaada ya Maafa ya kampuni. "Kilombero Sugar inaahidi kujali ustawi wa jamii yetu. Mchango wa leo unadhihirisha utayari na uadilifu wetu kwa jamii tunayoihudumia. Tumetoa msaada kwa zaidi ya familia 500, Kwa kulenga mahitaji yanayohitajika kwa haraka zaidi.


Zaidi ya hayo, Bwana Byemelwa amewahimiza wadau wengine kuunga juhudi za serikali za kusaidia jamii zilizoathiriwa na mafuriko ya hivi karibuni,Pia amesisitiza umuhimu wa hatua za pamoja dhidi ya mabadiliko ya hali ya hewa. Hii ikithibitisha tena dhamira ya Kampuni ya Kilombero Sugar kwa uhifadhi wa mazingira.

DSE ENTERPRISE ACCELERATION PROGRAM (DEAP)


We are now receiving applications for this upcoming 2024 DEAP cohort. 

Send your applications to deapenquiries@dse.co.tz stating the following;
  1. Business name
  2. Short description of the business
  3. Asset value
  4. Name of the business representative
  5. Mobile number & email address
  6. Business location
  7. Industry
Selected applicants will be fully sponsored to attend the DEAP.

Wednesday 17 April 2024

JSG TRAVELLERS BAGS OUTSTANDING & EXCELLENT BUSINESS TRAVEL AWARD

JSG Travellers Managing Director, Venancia J. Msita (centre) receives the prestigious award at the ceremony in Accra, Ghana.

JSG Travellers has been honored with the Outstanding & Excellent Business Travels Award at the The Sophisticated, High-Networth & Excellence (SHE) Global Awards, annual business ceremony to honour successful women change-makers, held in Accra, Ghana on 12th - 13th April, 2024.


With Ghana positioning itself as a beacon of peace and provider of enabling business ecosystem for investment as well as the home of tourism and hospitality, the organisers choose Accra as the best destination in Africa to host the fifth edition.


The theme for this year’s celebration, ‘The Queen of Sustainability’, underscores the need to live sustainably in ramifications without causing damage to the climate; and seeks to recognise businesswomen impacting the United Nations (UN) Sustainable Development Goals (SDGs) positively through their activities.


The glittering ceremony honoured heroines under four broad categories – Achievers awards, Women in the Corporate Sector awards, Female Entrepreneurs and Young Female Leaders awards.


A heartfelt thank you to JSG Travellers Managing Director, Venancia J. Msita, for her exemplary leadership. We're dedicated to exceeding expectations and delivering unparalleled service to our clients. Let's continue to soar together under the JSG flag!

Special thanks to Tanzania Women CEO’s Roundtable Management for their valuable contribution as well as recommendations during vetting processes!

TANZANIA YATETA NA UONGOZI WA IDARA YA SERA ZA KIBAJETI - IMF-FAD

Waziri wa Fedha, Dkt. Mwigulu Lameck Nchemba Madelu (Mb), akizungumza wakati ujumbe wa Tanzania ulipokutana na kufanya mazungumzo na Uongozi wa Idara ya Sera ya Kibajeti ya Shirika la Fedha la Kimataifa (IMF-FAD), Kando ya Mikutano ya Majira ya Kipupwe (Spring Meetings) ya Benki ya Dunia na Shirika la Fedha la Kimataifa IMF, inayoendelea Jijini Washington D.C nchini Marekani, ambapo pamoja na mambo mengine wamejadili namna ya kuimarisha ushirikiano kwa kutoa misaada ya kiufundi ili kuboresha mifumo na sera za kodi na ukusanyaji wa mapato ya Serikali.
Katibu Mkuu Wizara ya Fedha, Dkt. Natu El-maamry Mwamba, akizungumza wakati ujumbe wa Tanzania ulioongozwa na Waziri wa Fedha, Dkt. Mwigulu Lameck Nchemba Madelu (Mb) (hayupo pichani), ulipokutana na kufanya mazungumzo na Uongozi wa Idara ya Sera ya Kibajeti ya Shirika la Fedha la Kimataifa (IMF-FAD), Kando ya Mikutano ya Majira ya Kipupwe (Spring Meetings) ya Benki ya Dunia na Shirika la Fedha la Kimataifa IMF, inayoendelea Jijini Washington D.C nchini Marekani.
Ujumbe wa Tanzania (kulia) ukiongozwa na Waziri wa Fedha, Dkt. Mwigulu Lameck Nchemba Madelu (Mb) (katikati) wakiwa katika mazungumzo na Uongozi wa Idara ya Sera ya Kibajeti ya Shirika la Fedha la Kimataifa (IMF-FAD) (kushoto), Kando ya Mikutano ya Majira ya Kipupwe (Spring Meetings) ya Benki ya Dunia na Shirika la Fedha la Kimataifa IMF.
Naibu Mkurugenzi wa Idara ya Sera ya Kibajeti ya Shirika la Fedha la Kimataifa (IMF-FAD), Bw. Abdelhak Senhadji, akizungumza jambo wakati ujumbe wa Tanzania ulioongozwa na Waziri wa Fedha, Dkt. Mwigulu Lameck Nchemba Madelu (Mb) (hayupo pichani), ulipokutana na kufanya mazungumzo na Uongozi wa Idara hiyo, Kando ya Mikutano ya Majira ya Kipupwe (Spring Meetings) ya Benki ya Dunia na Shirika la Fedha la Kimataifa IMF.
Waziri wa Fedha, Dkt. Mwigulu Lameck Nchemba Madelu (Mb), (kushoto mstari wa mbele), akimsikiliza Katibu Mtendaji wa Tume ya Mipango, Bw. Lawrence Mafuru (kulia mstari wa mbele) wakati wa mazungumzo na Uongozi wa Idara ya Sera ya Kibajeti ya Shirika la Fedha la Kimataifa (IMF-FAD), Kando ya Mikutano ya Majira ya Kipupwe (Spring Meetings) ya Benki ya Dunia na Shirika la Fedha la Kimataifa IMF, inayoendelea Jijini Washington D.C nchini Marekani. Wengine katika picha ni Katibu Mkuu Wizara ya Fedha, Dkt. Natu El-maamry Mwamba (katikati mstari wa mbele) na Viongozi waandamizi wa Wizara ya Fedha, Mamlaka ya Mapato Tanzania - TRA na Shirika la Fedha la Kimataifa-IMF walioketi mstari wa nyuma.

Na. Joseph Mahumi, WF, Washington.

Waziri wa Fedha Mhe. Dkt. Mwigulu Nchemba (Mb), ameongoza Ujumbe wa Tanzania ulipokutana na kufanya mazungumzo na Uongozi wa Idara ya Sera ya Kibajeti ya Shirika la Fedha la Kimataifa (IMF-FAD), Kando ya Mikutano ya Majira ya Kipupwe (Spring Meetings) ya Benki ya Dunia na Shirika la Fedha la Kimataifa IMF, inayoendelea Jijini Washington D.C nchini Marekani ambapo pamoja na mambo mengine wamejadili namna ya kuimarisha ushirikiano kwa kutoa misaada ya kiufundi ili kuboresha mifumo na sera za kodi na ukusanyaji wa mapato ya Serikali.

Mkutano huo umehudhuriwa pia na Katibu Mkuu Wizara ya Fedha, Dkt. Natu El-maamry Mwamba, Katibu Mkuu Ofisi ya Rais Fedha na Mipango Zanzibar, Dkt. Juma Malik Akil, Kamishna Msaidizi wa Mamlaka ya Mapato Tanzania- TRA, Bw. Mcha Hassan Mcha, Viongozi waandamizi wa Wizara ya Fedha na Shirika la Fedha la Kimataifa-IMF.

NCHI ZA AFRIKA KUNUFAIKA NA UANACHAMA WAKE KWENYE NCHI 20 TAJIRI DUNIANI

Katibu Mkuu Wizara ya Fedha, Dkt. Natu El-maamry Mwamba, akizungumza wakati wa Mkutano wa Mawaziri wa Fedha na Magavana wa Benki Kuu za Afrika, waliojadili maeneo ya kipaumbele ambayo nchi za Afrika zinahitaji kuyasukuma kama agenda mahususi katika mikutano ya Kundi la nchi 20 Tajiri Duniani (G20) baada Umoja wa Africa kupewa kiti katika kundi hilo. Mkutano huo umefanyika katika Ofisi za Kamisheni ya Umoja wa Afrika, kando ya mikutano ya Kipupwe ya Benki ya Dunia na Shirika la Fedha la Kimataifa (IMF), Jijini Washington D.C, Marekani.
Gavana wa Benki Kuu ya Tanzania, Bw. Emmanuel Tutuba, akifuatilia Mkutano wa Mawaziri wa Fedha na Magavana wa Benki Kuu za Afrika, waliojadili maeneo ya kipaumbele ambayo nchi za Afrika zinahitaji kuyasukuma kama agenda mahususi katika mikutano ya Kundi la nchi 20 Tajiri Duniani (G20) baada Umoja wa Africa kupewa kiti katika kundi hilo. 
Katibu Mkuu Wizara ya Fedha, Dkt. Natu El-maamry Mwamba (Kulia), akiteta jambo na Waziri wa Fedha na Mipango ya Maendeleo ambaye pia ni Gavana Mstaafu wa Benki Kuu ya Lesotho, Dkt. Adelaide Retselisitsoe Matlanyane, wakati wa Mkutano wa Mawaziri wa Fedha na Magavana wa Benki Kuu za Afrika, waliojadili maeneo ya kipaumbele ambayo nchi za Afrika zinahitaji kuyasukuma kama agenda mahususi katika mikutano ya Kundi la nchi 20 Tajiri Duniani (G20).
Katibu Mkuu Wizara ya Fedha, Dkt. Natu El-maamry Mwamba (katikati), akifuatilia Mkutano wa Mawaziri wa Fedha na Magavana wa Benki Kuu za Afrika, waliojadili maeneo ya kipaumbele ambayo nchi za Afrika zinahitaji kuyasukuma kama agenda mahususi katika mikutano ya Kundi la nchi 20 Tajiri Duniani (G20). 
Baadhi ya Mawaziri wa Fedha na Magavana wa Benki Kuu za Afrika, wakiwa katika mkutano uliowakutanisha Mawaziri na Magavana hao.

Na Benny Mwaipaja, Washington D.C.

TANZANIA imeishauri Kamisheni ya Umoja wa Afrika (AUC), kutumia kikamilifu fursa ya kiti cha uwakilishi wa Umoja wa Afrika katika Kundi la nchi Ishirini Tajiri Duniani (G20), kutetea maslahi ya nchi za Afrika ili ziweke kukabiliana na changamoto mbalimbali zinazokwaza maendeleo ya nchi hizo ikiwemo madeni makubwa, maradhi, kilimo kisicho na tija, mabadiliko ya tabia nchi, uharibifu wa mazingira pamoja na matumizi hafifu ya teknolojia.

Ushauri huo umetolewa na Katibu Mkuu Wizara ya Fedha, Dkt. Natu El-maamry Mwamba, kwa niaba ya Waziri wa Fedha, Dkt. Mwigulu Lameck Nchemba, wakati wa Mkutano wa Mawaziri wa Fedha na Magavana wa Benki Kuu za nchi za Afrika, uliofanyika Kando ya Mikutano ya Kipupwe ya Benki ya Dunia na Shirika la Fedha la Kimataifa (IMF), iliyoanza rasmi jana Jijini Washington D.C nchini Marekani.

Dkt. Mwamba alisema kuwa Tanzania inaona kuwa nafasi hiyo ni muhimu kwa kuwa itachangia kutimiza malengo yake pamoja na ya nchi za Afrika kutekeleza na kusimamia vipaumbele vyake vya kuimarisha uchumi na huduma za kijamii kwa wananchi.

Aliyataja maeneo manne ya kimkakati yanayotakiwa kupewa msukumo mkubwa katika G20, ikiwemo maendeleo endelevu ya kiuchumi, uhimilivu wa madeni na Sekta ya fedha, Ulinzi wa mazingira na kukabiliana na mabadiliko ya Tabianchi, Maendeleo ya kilimo, Usalama wa chakula, afya, biashara na uwekezaji.

Dkt. Mwamba alifafanua kuwa nchi za Afrika zinahitaji kusaidiwa kuwa na miundombinu ya kijani, nishati jadidifu, matumizi ya teknolojia za kidigiti vitakavyochochea ukuaji wa uchumi jumuishi utakaozinufaisha nchi zote za Bara la Afrika.