Foreign Exchange Rates

DStv Advert_020324

DStv Advert_020324

SBT Tanzania Advert_291123

Wednesday 17 July 2019

PROF. KABUDI AKUTANA NA MABALOZI WA NCHI ZA SADC

Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Prof. Palamagamba John Kabudi (Mb.) amekutana na kufanya mazungumzo na Mabalozi wa nchi wanachama wa Jumuiya ya Maendeleo Kusini mwa Afrika (SADC) waliopo hapa nchini.
Katika mazungumzo hayo Prof. Palamagaba John Kabudi amewafahamisha hatua iliyofikiwa katika maandalizi ya Mkutanao wa wakuu wa nchi na Serikali wa nchi za Jumuiya ya Maendeleo Kusini mwa Afrika (SADC) uliyopangwa kufanyika nchini mwezi Agosti 2019

Kwa upande wa waheshimiwa Mabalozi hao walifurahishwa kwa hatua ya maandalizi iliyofikiwa, na kuelezea furaha yao kuhusu uamuzi wa Serikali kuwashirikisha mapema katika maandalizi hayo.

Sehemu ya Mabalozi wa Nchi za Afrika na wanachama wa Jumuiya ya SADC wakimsikiliza Prof. Palamagamba John Kabudi (hayupo pichani).
Sehemu nyingine ya watumishi kutoka Balozi za Afrika zilizopo nchini.
Prof. Palamagamba John Kabudi akifafanua jambo kwa Waheshimiwa Mabalozi alipokutana nao.
Balozi wa Afrika Kusini Mhe. Thamsanga Mseleku akielezea jambo katika mkutano na Waziri Prof. Palamagamba John Kabudi.
Continue Reading >>>

No comments:

Post a Comment