Foreign Exchange Rates

DStv Advert_010224

DStv Advert_010224

SBT Tanzania Advert_291123

Monday 24 June 2019

UNILEVER YAKAMILISHA KAMPENI YA TOA MKONO WA UKARIBU KWA KUSAIDIA YATIMA NA WAZEE WASIOJIWEZA

Meneja Bidhaa ya Omo ya Kampuni ya Unilever, Upendo Mkusa (kushoto) akimkabidhi msaada wa sabuni, Sukari na Nguo Mkurugenzi wa Kituo cha Kulelea Watoto yatima cha Children's Home Msimbazi, Sista Etienne katika kuhitimisha Kampeni ya Kampuni hiyo ya Toa Mkono wa Ukarimu iliyofanyika Kipindi cha mwezi wa Ramadhani uliomalizika hivi karibuni. Makabidhiano hayo yalifanyika kituoni hapo jijini Dar es Salaam mwishoni mwa wiki.
Meneja wa Bidhaa ya Omo wa Kampuni ya Unilever, Upendo Mkusa (katikati) akimkabidhi msaada wa sabuni, sukari na nguo Ofisa Mfawidhi wa Makazi ya wazee wasiojiweza ya Nunge, Jacklina Kanyamwenge katika kuhitimisha kampeni ya kampuni hiyo ya ‘Toa Mkono wa Ukarimu’ iliyofanyika kipindi cha Mwezi wa Ramadhani. Makabidhiano hayo yalifanyika kituoni Nunge, Kigamboni nje kidogo ya Jiji la Dar es Salaam mwishoni mwa wiki. Wanaoshuhudia ni Christabella Msangi na Nurdin Ally walioambata na meneja huyo. 
Mmoja wa wazee wanaoishi katika Makazi ya wazee wasiojiweza ya Nunge, Vumilia Chambusho (kulia), akipokea msaada wa baadhi ya vyakula, nguo na sabuni kutoka kwa Meneja Bidhaa ya Omo wa Kampuni ya Unilever, Upendo Mkusa (watatu kushoto) vilivyotolewa na Unilever katika kuhitimisha kampeni ya kampuni hiyo ya ‘Toa Mkono wa Ukarimu’ iliyofanyika kipindi cha Mwezi wa Ramadhani. Makabidhiano hayo yalifanyika kituoni hapo, Nunge, Kigamboni nje kidogo ya Jiji la Dar es Salaam mwishoni mwa wiki. Wanaoshuhudia ni Christabella Msangi na Nurdin Ally walioambata na meneja huyo.
Meneja wa Bidhaa ya Omo wa Kampuni ya Unilever, Upendo Mkusa (kushoto) akisalimiana na baadhi ya wazee wanaoishi katika Makazi ya wazee wasiojiweza ya Nunge baada ya kukabidhi msaada wa sabuni, sukari na nguo vilivyotolewa na Unilever katika kuhitimisha kampeni ya kampuni hiyo ya ‘Toa Mkono wa Ukarimu’ iliyofanyika kipindi cha Mwezi wa Ramadhani. Makabidhiano hayo yalifanyika kituoni Nunge, Kigamboni nje kidogo ya Jiji la Dar es Salaam mwishoni mwa wiki.

No comments:

Post a Comment