Foreign Exchange Rates

DStv Advert_020324

DStv Advert_020324

SBT Tanzania Advert_291123

Thursday 20 June 2019

BENKI YA CRDB YATOA GAWIO LA TZS 9.9 BILIONI KWA SERIKALI

Waziri wa Fedha na Mipango, Dkt. Philip Mpango (katikati) akiwa ameshikilia mfano wa hundi yenye thamani ya zaidi ya Shilingi 6.7 bilioni ikiwa ni Gawio la Serikali kutoka Benki ya CRDB. Jumla ya Gawio ni TZS 9.9 bilioni kwa Serikali Kuu, Halmashauri, Taasisi na Mashirika ya Umma ambayo ni Mifuko ya Hifadhi ya Jamii (PSSF, NSSF, GEPF na ZSSF) - TZS 2.6 bilioni, TAMISEMI (Halmashauri za Mbinga, Lindi, Shinyanga) - TZS 133.7 milioni, Mfuko wa Bima ya Afya ya Taifa (NHIF) - TZS 243.5 milioni, Chama cha Ushirika cha Wakulima wa Tumbaku Tabora - TZS 228 milioni. Wengine pichani kutoka kushoto ni Balozi wa Denmark nchini, Einar Jensen, Mwenyekiti wa Bodi ya Wakurugenzi wa Benki ya CRDB, Ally Laay, Mkurugenzi Mtendaji wa Benki ya CRDB, Abdulmajid Nsekela pamoja na Naibu Katibu Mkuu Wizara ya Fedha na Mipango Dkt. Khatibu Kazungu. Hafla hiyo imefanyika Juni 15, 2019 katika ukumbi wa Hazina, jijini Dodoma.
Waziri wa Fedha na Mipango, Dkt. Philip Mpango akikabidhi mfano wa hundi yenye thamani ya zaidi ya Shilingi 2.5 bilioni kwa wawakilishi wa Mifuko ya Hifadhi ya Jamii (PSSF, NSSF, GEPF na ZSSF), iliyotolewa na Benki ya CRDB.
Mwakilishi wa TAMISEMI (Halmashauri za Mbinga, Lindi, Shinyanga). 
Mwakilishi wa Mfuko wa Taifa wa Bima ya Afya (NHIF).
Mkurugenzi Mtendaji wa Benki ya CRDB, Abdulmajid Nsekela akimkabidhi mfano wa hundi mwakilishi wa Chama cha Ushirika cha Wakulima wa Tumbaku Tabora.
Waziri wa Fedha na Mipango, Dkt. Philip Mpango akizungumza wakati akitoa hotuba yake katika hafla fupi ya kupokea Gawio la TZS 9.9 bilioni kwa Serikali Kuu, Halmashauri, Taasisi na Mashirika ya Umma, lililotolewa na Benki ya CRDB, Juni 15, 2019 katika ukumbi wa Hazina, jijini Dodoma.
Mkurugenzi Mtendaji wa Benki ya CRDB, Abdulmajid Nsekela akizungumza katika hafla hiyo.
Mwenyekiti wa Bodi ya Benki ya CRDB, Ally Laay (kulia) akiteta jambo na Mkurugenzi Mtendaji wa Benki hiyo, Abdulmajid Nsekela.
















No comments:

Post a Comment