Foreign Exchange Rates

DStv Advert_020324

DStv Advert_020324

SBT Tanzania Advert_291123

Monday 4 June 2018

BENKI YA CBA YAFUTURISHA WATEJA WAKE DAR ES SALAAM

Afisa Mtendaji Mkuu wa Benki ya Biashara Afrika Tawi la Tanzania (CBA Tanzania), Dr. Gift Shoko akizungumza na baadhi ya wateja wakubwa wa benki hiyo jijini Dar es Salaam mwishoni mwa wiki, wakati benki hiyo ilipoandaa futari mahsusi. Kati ya mengi aliyoeleza, Shoko aliwahakikishia wateja wa benki hiyo jitihada madhubuti na endelevu zinazoendelea kufanywa na benki ya CBA kwa kuboresha huduma na bidhaa zake wakati wote. Hafla hiyo ilihudhuriwa na Waziri wa Nchi, Ofisi ya Makamu wa Rais (Muungano na Mazingira) January Makamba kama mgeni rasmi.
Waziri wa Nchi, Ofisi ya Makamu wa Rais (Muungano na Mazingira) January Makamba (kushoto) na Ofisa Mtendaji Mkuu wa benki ya CBA, Dk Gift Shoko (wa tatu kushoto) wakiwaogoza wateja wa benki hiyo kupakua futari iliyoandaliwa na benki hiyo kwenye hafla iliyofanyika Dar es Salaam hivi karibuni.
Waziri wa Nchi, Ofisi ya Makamu wa Rais (Muungano na Mazingira) January Makamba, akizungumza kwenye hafla hiyo. 

Picha ya pamoja.

No comments:

Post a Comment