Foreign Exchange Rates

DStv Advert_020324

DStv Advert_020324

SBT Tanzania Advert_291123

Sunday 25 March 2018

BENKI YA NBC YAAHIDI KUENDELEA KUTOA HUDUMA BORA KWA WATEJA WAKE

Mkurugenzi Mtendaji wa NBC, Theobald Sabi (kushoto), akizungumza katika hafla ya wateja ambapo pia aliwatambulisha baadhi ya wakurugenzi wa benki hiyo (kushoto kwake), jijini Dar es Salaam hivi karibuni. Alisema lengo la hafla hiyo ni kukutana na wateja kuzungumza nao na kupata mrejesho kuhusu huduma wanazowapa.
Mkurugenzi wa Huduma kwa Wateja Binafsi wa NBC, Filbert Mponzi akizungumza katika hafla hiyo ambapo pamoja na mambo mengine alizungumzia jinsi NBC ilivyojipanga kutoa huduma bora kwa wateja wake katika mwaka 2018. Alisema wamezindua kampeni iitwayo Karibu Nyumbani ikilenga kuwarudisha nyumbani katika Benki ya NBC wateja wao wa zamani ili waweze kufurahi huduma zao.
Mkurugenzi wa Huduma za Biashara wa NBC, Elvis Nduguru akizungumza na wateja wa benki hiyo katika hafla waliyowaandalia jijini Dar es Salaam hivi karibuni. Alisema NBC kitengo cha biashara kimejipanga kuboresha huduma zake hususan huduma za malipo kwa njia ya kadi (POS).
Mmoja wa wateja wa NBC, Sadock Magai, akitoa neno la shukrani kwa niaba ya wateja wenzake katika hafla hiyo.
Mteja wa NBC na mmoja wa wanasiasa wakongwe nchini, Steven Masato Wassira (kulia), akizungumza na baadhi ya wafanyakazi wa NBC katika hafla hiyo.
Baadhi ya wateja wa NBC waliohudhuria katika hafla hiyo ambayo Mkurugenzi Mtendaji wake, Theobald Sabi alisema benki hiyo iliyodumu kwa zaidi ya miaka 50 imejizatiti katika kuhudumia wateja wake kwa ufanisi na weledi mkubwa.
Baadhi ya wateja wa NBC wakimsikiliza Mkurugenzi Mtendaji wa NBC, Theobald Sabi (hayupo pichani), wakati akizungumza nao. Bwana Sabi alizitaja baadhi ya huduma zao mpya ikiwa na pamoja na Klabu za Biashara (NBC Business Club) kwa ajili ya wafanyabiashara wadogo na wakati kuwasaidia kukuza biashara zao, akaunti ya vikundi na nyingine nyingi.
Baadhi ya wateja na wafanyakazi wa NBC wakiselebuka katika hafla hiyo.
Viongozi mbalimbali wa Idara ya Wateja Binafsi ya NBC wakipozi mbele ya wateja wao katika hafla hiyo. Wa tatu kutka kushoto mstari wa nyuma ni Mkuu wa Idara hiyo, Filbert Mponzi.
Viongozi mbalimbali wa Idara ya Biashara ya NBC wakipozi mbele ya wateja wao katika hafla hiyo. Wa tatu utoka kushoto mstari wa mbele ni Mkuu Idara hiyo, Elvis Ndunguru.

No comments:

Post a Comment