Blog Rebranding Teaser_030826
Stanbic Bank Banner_070826
Absa Loan Campaign_160426
Tuesday, 15 October 2024
DKT. NCHEMBA ATETA NA MKUU WA KAMPUNI YA HEINEKEN JIJINI DODOMA
Na. Benny Mwaipaja, Dodoma.
Waziri wa Fedha, Mhe. Dkt. Mwigulu Lameck Nchemba Madelu (Mb), amekutana na kufanya mazungumzo na Mkuu wa Masuala ya Ushirikiano wa Kimataifa wa Kampuni ya vinywaji vya Heineken, Bw. Frank Ford, aliyemtembelea Ofisini kwake, Jengo la Treasury Square, jijini Dodoma, akiambatana na Afisa Masoko wa Kampuni hiyo. Bi. Lilian Pascal, ambapo walijadili kuhusu maendeleo ya kampuni hiyo iliyowekeza hapa nchini na namna inavyochangia katika pato la Taifa na Uchumi wa nchi kwa ujumla.
Kikao hicho kilihudhuriwa pia na Naibu Katibu Mkuu Wizara ya Fedha anayesimamia Sera za Uchumi, Bw. Elijah Mwandumbya na Kamishna Msaidizi, Idara ya Sera, Bw. William Mhoja, pamoja na Maafisa wengine waandamizi wa Wizara ya Fedha.
Subscribe to:
Post Comments (Atom)






No comments:
Post a Comment