Foreign Exchange Rates

DStv Advert_020324

DStv Advert_020324

SBT Tanzania Advert_291123

Tuesday 28 May 2019

BALOZI SEIF ALI IDD AWAONGOZA WATEJA WA BENKI YA CRDB KATIKA IFTAR ILIYOANDALIWA ZANZIBAR

Makamu wa Pili wa Rais wa Serikali ya Mapinduzi Zanzibar, Balozi Seif Ali Idd akilakiwa na Mkurugenzi Mtendaji wa Benki ya CRDB, Abdulmajid Nsekela (kushoto) wakati alipowasili katika hafla ya Iftar iliyoandaliwa na Benki ya CRDB kwa Wateja wake, iliyofanyika hive karibuni kwenye hoteli ya Velde, Unguja Zanzibar. Kulia ni Mkuu wa Mkoa wa Mjini Magharibi, Ayoub Mohammed Mahmoud. 
Mkurugenzi Mtendaji wa Benki ya CRDB, Abdulmajid Nsekela (katikati) akimtambulisha kwa Makamu wa Pili wa Rais wa Serikali ya Mapinduzi Zanzibar, Balozi Seif Ali Idd (wa pili kulia), Naibu Mkurugenzi Mtendaji wa Benki hiyo, Dkt. Joseph Witts wakati alipowasili katika hafla ya Iftar iliyoandaliwa na Benki ya CRDB kwa Wateja wake, iliyofanyika hivi karibuni kwenye hoteli ya Velde, Unguja Zanzibar. Kulia ni Mkuu wa Mkoa wa Mjini Magharibi, Ayoub Mohammed Mahmoud na kushoto ni Mkurugenzi wa Huduma Mbadala wa Benki ya CRDB, Philip Alfred.
Makamu wa Pili wa Rais wa Serikali ya Mapinduzi Zanzibar, Balozi Seif Ali Idd akisalimiana na Mkurugenzi wa Huduma Mbadala wa Benki ya CRDB, Philip Alfred (kushoto) wakati alipowasili katika hafla ya Iftar iliyoandaliwa na Benki ya CRDB kwa Wateja wake, iliyofanyika hivi karibuni kwenye hoteli ya Velde, Unguja Zanzibar. Kulia ni Mkuu wa Mkoa wa Mjini Magharibi, Ayoub Mohammed Mahmoud.
Makamu wa Pili wa Rais wa Serikali ya Mapinduzi Zanzibar, Balozi Seif Ali Idd, Mkuu wa Mkoa wa Mjini Magharibi, Ayoub Mohammed Mahmoud pamoja na Mkurugenzi Mtendaji wa Benki ya CRDB, Abdulmajid Nsekela wakielekea sehemu maalum iliyokuwa imetengwa kwaajili ya ibada ya Magharibi. 
Makamu wa Pili wa Rais wa Serikali ya Mapinduzi Zanzibar, Balozi Seif Ali Idd akizungumza jambo na Mkurugenzi Mtendaji wa Benki ya CRDB, Abdulmajid Nsekela kabla ya kufanyika kwa ibada ya Magharibi, katika hafla ya Iftar iliyoandaliwa na Benki ya CRDB kwa Wateja wake, iliyofanyika hivi karibuni kwenye hoteli ya Velde, Unguja Zanzibar.






No comments:

Post a Comment