Foreign Exchange Rates

DStv Advert_020324

DStv Advert_020324

SBT Tanzania Advert_291123

Wednesday 10 October 2018

DKT. MAHIGA ASHIRIKI MKUTANO WA TICAD


Kufuatia mwaliko wa Mhe. Taro Kono, Waziri wa Mambo ya Nje wa Japan, Mhe. Balozi Dkt. Augustine Mahiga (Mb.), Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki ameshiriki Mkutano wa Kimataifa wa Tokyo kuhusu Maendeleo ya Afrika, (Tokyo International Conference for African Development-TICAD). Mkutano huo umeanza tarehe 6-7 Oktoba, 2018, Tokyo, Japan.

Mkutano huo ambao umewashirikisha Mawaziri wa Mambo ya Nje wa Afrika, pamoja na masuala mengine, unajadili maazimio ya Mkutano wa Tano na wa Sita wa TICAD iliyofanyika mwaka 2013 na 2016, pamoja na kuandaa agenda za Mkutano wa Wakuu wa nchi wa TICAD VII unaotegemea kufanyika Yokohama, mwezi Agosti, 2019.

Masuala yaliyojadiliwa ni pamoja; Changamoto tangu kukamilika kwa TICAD VI mwaka 2016; Mageuzi ya kiuchumi na ukuaji shirikishi; Kuimarisha sekta ya Afya, Amani na Usalama katika jamii na; kuimarisha mawasiliano barani Afrika na duniani kote. Maeneo haya yanaenda sambamba na Agenda 2030 ya Umoja wa Mataifa na Agenda 2063 ya Umoja wa Afrika.

No comments:

Post a Comment