Foreign Exchange Rates

DStv Advert_020324

DStv Advert_020324

SBT Tanzania Advert_291123

Saturday 11 August 2018

RAIS DKT. JOHN POMBE MAGUFULI AKUTANA NA KUFANYA MAZUNGUMZO NA MGENI WAKE RAIS WA UGANDA YOWERI MUSEVENI IKULU JIJINI DAR ES SALAAM. AGOSTI 9, 2018

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akimpokea mgeni wake Rais Yoweri Kaguta Museveni wa Uganda katika Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Julius Nyerere alipowasili nchini kwa ziara ya kikazi ya siku moja. Agosti 9, 2018.
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akimkaribisha mgeni wake Rais Yoweri Kaguta Museveni wa Uganda Ikulu kwaajili ya mazungumzo mara baada ya kuwasili nchini kwa ziara ya kikazi ya siku moja. Agosti 9, 2018.
Rais wa Uganda Yoweri Museveni akizungumza na wanahabari (hawapo pichani) mara baada ya kikao chake na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli Ikulu jijini Dar es Salaam.
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akizungumza jambo na mgeni wake Rais wa Uganda Yoweri Museveni mara baada ya kutoka kwenye chumba cha mkutano wa Wanahabari Ikulu jijini Dar es Salaam.
Bofya hapa kwa picha zaidi

No comments:

Post a Comment