Msemaji wa Jeshi la Polisi, Kamishna Msaidizi wa Polisi (ACP) Barnabas Mwakalukwa akiwa na Mkuu wa Idara ya Masoko na Mawasiliano wa Benki ya Exim Tanzania, Stanley Kafu (kushoto) wakionesha moja kati ya jezi zilizodhaminiwa na benki hiyo kwaajili ya Mashindano ya Shirikisho la Majeshi ya Polisi Kusini mwa Afrika (EAPCCO) yaliyotarajiwa kuanza jana kwenye viwanja vya Chuo Kikuu cha Dar es Salaam. Mashindano hayo yanayoshirikisha nchi 14 yatahusisha michezo ya Mpira wa Miguu, Netiboli, Mpira wa wavu, Kulenga shabaha, Kareti, Judo na Taekondo na yanatarajiwa kumalizika mwishoni mwa wiki hii. Wengine ni Abdul Nkondo (kulia), Meneja msaidizi wa idara ya masoko na mawasiliano wa Benki ya Exim Bank Tanzania na PC Daniel Mashaka (kushoto). |
No comments:
Post a Comment