Foreign Exchange Rates

DStv Advert_020324

DStv Advert_020324

SBT Tanzania Advert_291123

Monday 15 January 2018

VODACOM TANZANIA YAMKABIDHI MUDATHIR YAHAYA TSH MILIONI 1 NA TUZO


Afisa Udhamini na Matukio wa Vodacom Tanzania, Ibrahim Kaude akimpongeza Mudathiri Yahaya kwa kuibuka mchezaji bora wa mwezi Novemba 2017. Anayeshuhudia katikati ni Meneja Fedha wa Bodi ya Ligi, Ibrahim Mwayella. Makabidhiano hayo yamefanyika leo wakati timu yake ya Singida United ikifanya mazoezi Uwanja wa Uhuru, Dar es Salaam kujiandaa na mechi yao ya Alhamisi dhidi ya Simba kwenye Ligi Kuu ya Vodacom (VPL) Tanzania Bara.    
Mudathiri Yahaya akipokea tuzo ya mchezaji bora wa mwezi Novemba 2017 wa Ligi Kuu ya Vodacom (VPL) Tanzania Bara msimu wa 2017/2018 kutoka kwa Afisa Udhamini na Matukio wa Vodacom Tanzania, Ibrahim Kaude. Anayeshuhudia katikati ni Meneja Fedha wa Bodi ya Ligi, Ibrahim Mwayella. Makabidhiano hayo yamefanyika leo wakati timu yake ya Singida United ikifanya mazoezi Uwanja wa Uhuru, Dar es Salaam kujiandaa na mechi yao ya Alhamisi dhidi ya Simba kwenye Ligi Kuu ya Vodacom (VPL) Tanzania Bara.    

Kampuni ya simu za mkononi nchini, Vodacom Tanzania, wadhamini wakuu wa Ligi Kuu ya soka Tanzania Bara wamemkabidhi kiungo wa Singida United ya Singida Tsh milioni 1 na tuzo kwa kuibuka Mchezaji Bora wa Mwezi Novemba 2017 wa Ligi Kuu ya Vodacom (VPL) Tanzania Bara msimu wa 2017/2018. Makabidhiano hayo yamefanywa na Afisa Udhamini na Matukio wa Vodacom Tanzania, Ibrahim Kaude na Meneja Fedha wa Bodi ya Ligi, Ibrahim Mwayella wakati timu hiyo ikifanya mazoezi Uwanja wa Uhuru, Dar es Salaam kujiandaa na mechi yao ya Alhamisi dhidi ya Simba kwenye Ligi Kuu ya Vodacom (VPL) Tanzania Bara.

Mudathir alitwaa tuzo hiyo baada ya kuwashinda wenzake wawili, Beki Asante Kwasi wa Lipuli ya Iringa na Mshambuliaji Danny Usengimana pia wa Singida United, alioingia nao fainali ya kuwania nafasi hiyo. Mchezaji huyo alitoa mchango mkubwa kwa Singida United mwezi huo ikipata pointi saba katika michezo mitatu iliyocheza na kupanda katika msimamo wa ligi kutoka nafasi ya sita iliyokuwepo mwezi Oktoba hadi ya nne.

Akizungumza baada ya kukabidhiwa zawadi hizo ikiwemo Dekoda kutoka Azam TV Mudathir amesema “Kikubwa ambacho kimebadilika na kimemfanya niibuke mchezaji bora ni kocha Hans kumwamini kwasababu mtu akikuamini unafanya kile ulichonacho kwa juhuzi zaidi”

Mudathir Yahya anakuwa mchezaji wa kwanza mzawa kushinda tuzo ya mchezaji bora katika Ligi Kuu ya Vodacom (VPL) Tanzania Bara msimu wa 2017/2018. Mwezi Agosti mshindi alikuwa ni Emmanuel Okwi wa Simba, Septemba akawa ni Shafik Batambuze wa Singida United na mwezi Oktoba akashinda Obrey Chirwa wa Young Africans.

No comments:

Post a Comment